Mchango wa Rais Mkapa katika Mwalimu Nyerere Foundation

Hivi kama kweli Mkapa alikuwa karibu sana na Nyerere - kama anavyotaka watu waamini - alifanya nini katika kuijenga na kuiunga mkono taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa miaka yake kumi alipokuwa Rais? Na hata leo hii amefanya nini - hata kuichangia muda na raslimali zake kuijenga? Maana karibu wengi ambao waliwahi kuwa karibu sana na Nyerere wamekuwa ni wadau wakubwa wa taasisi hiyo.

Isije kuwa ukaribu huu ulikuwepo wakati Nyerere alipokuwa hai tu lakini pia haukuwa ukaribu wa kifikra wa kumfanya akubaliane na malengo na nia za MNF.

Kuhusu Kikwete naelewa kwa nini hayuko karibu na MNF lakini Mkapa kwa kweli sijui.

Alimjengea nyumba nzuri butiama kabla ya hapo alikuwa hana nyumba ya uhakika. Kwani mchango mpaka uupeleke ninyi mnakotaka?
 
Kikubwa zaidi aliacha mjane wa baba wa taifa anyang'anywe eneo msasani na swahiba wake na mkapa aliyekua anapiga matofali
 
Wahenga walisema "shukurani ya punga ni mateke", hivi bila mwalimu kuzunguka huku na kule mzee wa wangu kumpigia debe huyu 'akaaye hapa' nani angemjua na hata kumpa kura yake. Nakumbuka gazeti moja lilijaribu kuwauliza watu mkapa ni nani na wengi walimjua zaidi Keneth Mkapa wa Yanga kuliko huyo aliyekuja kuwa rahisi. "Pole Mwalimu huko uliko, kikulacho ndugu yangu!"
 
Mkapa aliwapa MNF kiwanja pale makutano ya Shaban Robert na Sokoine Drive bahati mbaya design ya jengo lao haliruhusiwi kwa vile ni karibu na ikulu. Sasa mbona BoT na lile jirani ocean road hosp ni marefu kiasi hicho, TISS wanatakiwa kujibu!

Ila bado ukweli unabaki kuwa Mkapa ni mnafiki mkubwa kuliko hata kina Kingunge.......
 
Alimjengea nyumba nzuri butiama kabla ya hapo alikuwa hana nyumba ya uhakika. Kwani mchango mpaka uupeleke ninyi mnakotaka?
Nani alimjengea nani nyumba Butiama? Kumbe wewe MkamaP ni mwongo na mpuuzi kiasi hichi? hiyo nyumba ya Butiama imejengwa na wanajeshi. Ilianza kujengwa enzi za Mwinyi and Mkapa had nothing to do with it. Kumbe ukipenda kinyesi unaona ni kachumbari? Na hata kabla ya hiyo nyumba kuna nyumba aliyojengewa na Machel na kuna nyumba aliyojijengea mwenyewe alipomaliza masomo. Acha ubabaishaji. Abhajita chitakubheyaga!
 
Mkapa aliwapa MNF kiwanja pale makutano ya Shaban Robert na Sokoine Drive bahati mbaya design ya jengo lao haliruhusiwi kwa vile ni karibu na ikulu. Sasa mbona BoT na lile jirani ocean road hosp ni marefu kiasi hicho, TISS wanatakiwa kujibu!

Ila bado ukweli unabaki kuwa Mkapa ni mnafiki mkubwa kuliko hata kina Kingunge.......
RealMan
Hiyo ya kwamba jengo haliruhusiwi kwa sababu ya ukaribu na Ikulu limeletwa na Kikwete. Kuna jengo pale Ocean Road ni refu kuliko Ikulu, alipoulizwa Kikwete juu yake akasema litabomolewa. Wewe na mimi tunajua kuwa hilo jengo halitabomolewa.
 
Kwa miaka 10 Mkapa hakuhakikisha taasisi ambayo Mwalimu aliianzisha inakuwa viable na inajitegemea. Angeweza kabisa kuifanya iwe ni taasisi ya kujivunia kwani inabeba jina la Mwalimu na malengo yake ni makubwa sana kwa taifa letu. Kikwete naye ni hivyo hivyo. Mimi nina uhakika wakitokea Watanzania ambao wako tayari kuipa uongozi na mchango mkubwa viongozi hawa watakuwa wa kwanza kutafuta ujiko hapo.
 
Kwa miaka 10 Mkapa hakuhakikisha taasisi ambayo Mwalimu aliianzisha inakuwa viable na inajitegemea. Angeweza kabisa kuifanya iwe ni taasisi ya kujivunia kwani inabeba jina la Mwalimu na malengo yake ni makubwa sana kwa taifa letu. Kikwete naye ni hivyo hivyo. Mimi nina uhakika wakitokea Watanzania ambao wako tayari kuipa uongozi na mchango mkubwa viongozi hawa watakuwa wa kwanza kutafuta ujiko hapo.

Ina umuhimu gani mkubwa kwa taifa letu? nijuze tafadhali?
 
Kwa miaka 10 Mkapa hakuhakikisha taasisi ambayo Mwalimu aliianzisha inakuwa viable na inajitegemea. Angeweza kabisa kuifanya iwe ni taasisi ya kujivunia kwani inabeba jina la Mwalimu na malengo yake ni makubwa sana kwa taifa letu. Kikwete naye ni hivyo hivyo. Mimi nina uhakika wakitokea Watanzania ambao wako tayari kuipa uongozi na mchango mkubwa viongozi hawa watakuwa wa kwanza kutafuta ujiko hapo.
Mwanakijiji,
Siyo hivyo tu, alifikia hatua ya kumpigia Museveni simu kumwomba aache kumpa Butiku fedha za kuendesha taasisi.
Wachangiaji wakubwa wa taasisi hiyo wamekuwa ni Museveni, Kagame na Mandela.
 
Je Mkapa amefika mara ngapi Butiama kumuona mama Maria tokea kifo cha baba wa Taifa? Kwa kujinadi kwake kuwa amekuwa karibu kabisa na familia ya mwalimu kwa kipindi cha miaka 25 na jinsi mwalimu alivyotumia nguvu na rasilimali kibao kumuingiza magogoni ningetegemea angekuwa anapiga hodi mara kwa mara Butiama kumsalimia mama Maria, Je amekuwa akifanya hivyo? kama mara ngapi hivi tokea baba wa taifa aondolewe na mauti? Guilty Conciousness?????!!!!!!
 
Nani alimjengea nani nyumba Butiama? Kumbe wewe MkamaP ni mwongo na mpuuzi kiasi hichi? hiyo nyumba ya Butiama imejengwa na wanajeshi. Ilianza kujengwa enzi za Mwinyi and Mkapa had nothing to do with it. Kumbe ukipenda kinyesi unaona ni kachumbari? Na hata kabla ya hiyo nyumba kuna nyumba aliyojengewa na Machel na kuna nyumba aliyojijengea mwenyewe alipomaliza masomo. Acha ubabaishaji. Abhajita chitakubheyaga!

Tulia wewe, ktk idhini ya nani na ktk uongozi wa nani? na tena kama hujui mwl alikuwa amekataa kujengewa nyumba. Acha kukurupuka wewe Mkapa yupo sahihi mnukuu mwenyewe
 
Topical,
Kwako, nadhani haina umuhimu wowote kwa taifa kama vile Julius Nyerere hakuwa na umuhimu wowote.

Lakini si mtanzania niambie nyie mnaojua umuhimu wake kwa Taifa, ili tujue kama kuna haja ya taifa kutoa fedha zake hapo..

Wanaharakati wapenzi wa nyerere wanatosha au vipi? mbona mnapenda sana kuandika proposals za kutoa pesa za umma kwa mambo ya kijinga??
 
Lakini si mtanzania niambie nyie mnaojua umuhimu wake kwa Taifa, ili tujue kama kuna haja ya taifa kutoa fedha zake hapo..

Wanaharakati wapenzi wa nyerere wanatosha au vipi? mbona mnapenda sana kuandika proposals za kutoa pesa za umma kwa mambo ya kijinga??
Sasa ndugu yangu unasema ni mambo ya kijinga halafu unataka tukuambie nini? Wazungu wanasema kauli yako hiyo ni non starter.
 
Lakini si mtanzania niambie nyie mnaojua umuhimu wake kwa Taifa, ili tujue kama kuna haja ya taifa kutoa fedha zake hapo..

Wanaharakati wapenzi wa nyerere wanatosha au vipi? mbona mnapenda sana kuandika proposals za kutoa pesa za umma kwa mambo ya kijinga??


Hivi nani kasema watoe fedha za umma?
 
Tulia wewe, ktk idhini ya nani na ktk uongozi wa nani? na tena kama hujui mwl alikuwa amekataa kujengewa nyumba. Acha kukurupuka wewe Mkapa yupo sahihi mnukuu mwenyewe
Hapana, Mwalimu hakukataa kujengewa nyumba. Alikataa ukubwa wa nyumba. Hiyo ndiyo iliyokuwa back and forth kati yake na jeshi, lakini nyumba imeanza kujengwa enzi za Mwinyi.
 
Hapana, Mwalimu hakukataa kujengewa nyumba. Alikataa ukubwa wa nyumba. Hiyo ndiyo iliyokuwa back and forth kati yake na jeshi, lakini nyumba imeanza kujengwa enzi za Mwinyi.

Ungekuwa muungwana zaidi kutuambia hiyo nyumba ilikamilika mwaka gani? na enzi za mwinyi ilianza kujengwa mwaka gani? ungejenga hoja vizuri.
 
Sasa ndugu yangu unasema ni mambo ya kijinga halafu unataka tukuambie nini? Wazungu wanasema kauli yako hiyo ni non starter.

Mnatetea kitu hata hamjui faida moja ..hata kuitaja tu? kazi..

Wazungu wanahusika vipi kwenye mjadala mkuu..acheni excuses..nitajie umuhimu wake kwa taifa?
 
Back
Top Bottom