Mchango kwa Mh Lema - Waziri Kivuli Mambo ya Ndani

FJM

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
8,081
6,198
Alhamisi tarehe 28/07/11 Wizara ya Mambo ya ndani itawasilisha hoja/bajeti yake bungeni. Wizara hii inasimamia uhamiaji, polisi, magereza na hata usalama barabarani. Akiwa kama Waziri kivuli naomba Mh Lema aulize/asimamie yafuatayo:

1. Ajali za barabarani
Ajali za barabarani zimekuwa zinaongezeka siku hadi siku na hasa kwa mabasi yanayotoa usafiri wa kwenda mikoani. Idadi ya watu waliokufa kutokana na ajali hizo inatisha. Sasa Lema atoe hoja kwamba serikali ianzishe DATABASE kwa ajili ya kuweka record sawa majina ya kampuni yanayomiliki mabasi na ajali zake. Mabasi kama Abood, Sumry na Hood yanaonekana kuwa ajali nyingi za kustusha. Kama kampuni inapata ajali na watu kupoteza maisha basi kampuni hiyo isiruhusiwe kutoa huduma ya usafiri hadi pale serikali na hasa wizara itakapofanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa hatua zote za usalama zinaheshimiwa.

Haiingii akilini kwamba kampuni moja ya mabasi inapata ajali mara mbili ndani ya mwezi mmoja, watu wanapoteza maisha lakini bado mabasi yake mengine yako barabarani huku serikali imekaa kimya!

2. Ubora wa mabasi ya abiria
Huko nyuma serikali ilikuwa imetoa muda kwa wamiliki wa mabasi makubwa (kama sikosei ilikuwa 6 months) ili waondokane na tabia cha kuchanga bodi na engine za FUSO. Hili ni jambo la muhimu sana maana linahusu usalama wa maisha ya abiria lakini bila maelezo hakuna chochote kilichofanyika. Kuna ma-lobbyists wameibana serikali na sasa mabasi mengi yanatumia engine za Fuso. Kwangu mimi naona wenye mabasi ya engine za Fuso wanajali zaidi faida kuliko uhai wa abiria lakini kinachosikitisha ni kwa serikali kunyamaza huku watanzania wanakufa. Basi la kubeba abiria lazima limitize masharti yote ya ki-usalama na sharti moja kubwa ni ubora wa engine yake. Lazima liwe na engine ya basi la abiria na si vinginevyo.

3. Uhamiaji
Tanzania imekuwa kama shamba la bibi kwa kuwa na raia wa kigeni wanafanya kazi ambazo watanzania wanaweza kufanya. Maswali hapa:
- Idadi ya raia wa kigeni walioko Tanzania ni ngapi?
- Vibali au visa kwa wageni wanafanya kazi nchini zinapatikanaje?
- Wale wamachinga wa Kichina walioko Kariakoo wamepataje vibali vya kuingia?
- Kuna maduka ya wahindi (airport Dar es Salaam, KIA na Zanzibar) wameajiri wauza wahindi toka India kuja kuuza maduka. Kuna vyumba za kupanga _commercial residents zinazomilikiwa na wahindi ukichunguza wafanyakazi utakuta wanatoka India. Hivi ni kweli Mtanzania hawezi kusimamia usambazaji wa maji (kwa malori) kwenye hizi maflats ya wahindi?

4. Diplomatic passport
Ni watu gani wanatakiwa wawe na Diplomatic passport na sasa hivi ni wangapi ambao wana hizo passport?
(kuna watu wengi tu huku mtaani wana Diplomatic passport)


5. Magereza
Hali ya mahabusu na wafungwa inatisha! Kuna watu wamebambikiwa kesi wako rumande kwa miaka. Ukitembelea magereza unaweza kuzimia kwa uchungu. kuna watanzania (wasio na hatia) na wengine ni watoto wako mahabusu for years!
Hapa Lema ahimize kuundwe timu maalum ya kuchunguza hali ya jela, na mahabusu na pia kupata taarifa kamili juu ya maabusu wanaosubiri kesi kwa miaka!
 
swali la ziada ningependa kujua Tanzania kama nchi imejiandaje kukabiliana na tukio kama lilo tokea hivi karibuni nchini Norway.
maana inabidi tujifunze kutoka kwa wenzetu.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Haya ni madini ya ukwel mr lema kaz ni kwako naunga mkono hoja mi naisubiri hiyo kesho.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mauaji ya raia yanayofanywa na polisi kama ilivyotokea Arusha, Mara, Mbeya, Morogoro na Dar.
Aulize pia huo mfumo wa intelijensia ya polisi kwa maandamano tu na kufumbia macho uchakachuaji na ulaji mali ya umma?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
2. Ubora wa mabasi ya abiria
Huko nyuma serikali ilikuwa imetoa muda kwa wamiliki wa mabasi makubwa (kama sikosei ilikuwa 6 months) ili waondokane na tabia cha kuchanga bodi na engine za FUSO. Hili ni jambo la muhimu sana maana linahusu usalama wa maisha ya abiria lakini bila maelezo hakuna chochote kilichofanyika. Kuna ma-lobbyists wameibana serikali na sasa mabasi mengi yanatumia engine za Fuso. Kwangu mimi naona wenye mabasi ya engine za Fuso wanajali zaidi faida kuliko uhai wa abiria lakini kinachosikitisha ni kwa serikali kunyamaza huku watanzania wanakufa. Basi la kubeba abiria lazima limitize masharti yote ya ki-usalama na sharti moja kubwa ni ubora wa engine yake. Lazima liwe na engine ya basi la abiria na si vinginevyo.

![/QUOTE] Mie hoja yangu ipo pale tutakapoifanya Tanzania kama tutajifananisha kuwa ni mabasi ya kukizi haja wakati barabara hazikizi viwango, kwa mara niliposikia kuwa mabasi yenye Chasisi za malori zilifungiwa nilihisi hiyo ilikuwa siasa tu! Hatukuambiwa kitaalamu kwanini fuso ikibeba mizigo ambayo ni mizito zaidi ya idadi ya abiria haipati ajali, Hiyo yaweza kuwa injini, abayo inawezakutumika kwa gari lolote sasa pengine tungehusisha bodi zaidi ya engine. Nadhani Mh. Lema asizungumze kuhusu hili kwani halikufanyiwa uchunguzi wa kina, ni hoja iliyotolewa na Bwana Kombe ilikuwa kupunguza maswali, hayo yalikuwa ni majibu rahisi, haitofautiani sana, na Kuweka chombo cha kudhibiti mafuta, alafu unaengeza kodi kwa mafuta ya taa yanayotumiwa na wengi wenyekipato cha chini, kwa madai ya kukomesha uchakachuaji wa mafuta. Je walio ajiriwa EURA walipwa kwa misingi ipi? Kwa mimi naona chasisi ya malori ni bora zaidi kutokana na viwango vya barabara na pia kwa ubebaji abiria kupita kiasi!! labda aingie mtaalam aielezee kiundani zaidi. naamini kuwa Ajali za barabarani hutokana na uzembe wa madereva wenyewe kutoheshimu Alama za barabara, na pia pande zingine hakuna vibao vya kuashiria Alama hizo za nyakati!!
 
Alhamisi tarehe 28/07/11 Wizara ya Mambo ya ndani itawasilisha hoja/bajeti yake bungeni. Wizara hii inasimamia uhamiaji, polisi, magereza na hata usalama barabarani. Akiwa kama Waziri kivuli naomba Mh Lema aulize/asimamie yafuatayo:

1. Ajali za barabarani
Ajali za barabarani zimekuwa zinaongezeka siku hadi siku na hasa kwa mabasi yanayotoa usafiri wa kwenda mikoani. Idadi ya watu waliokufa kutokana na ajali hizo inatisha. Sasa Lema atoe hoja kwamba serikali ianzishe DATABASE kwa ajili ya kuweka record sawa majina ya kampuni yanayomiliki mabasi na ajali zake. Mabasi kama Abood, Sumry na Hood yanaonekana kuwa ajali nyingi za kustusha. Kama kampuni inapata ajali na watu kupoteza maisha basi kampuni hiyo isiruhusiwe kutoa huduma ya usafiri hadi pale serikali na hasa wizara itakapofanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa hatua zote za usalama zinaheshimiwa.

Haiingii akilini kwamba kampuni moja ya mabasi inapata ajali mara mbili ndani ya mwezi mmoja, watu wanapoteza maisha lakini bado mabasi yake mengine yako barabarani huku serikali imekaa kimya!

2. Ubora wa mabasi ya abiria
Huko nyuma serikali ilikuwa imetoa muda kwa wamiliki wa mabasi makubwa (kama sikosei ilikuwa 6 months) ili waondokane na tabia cha kuchanga bodi na engine za FUSO. Hili ni jambo la muhimu sana maana linahusu usalama wa maisha ya abiria lakini bila maelezo hakuna chochote kilichofanyika. Kuna ma-lobbyists wameibana serikali na sasa mabasi mengi yanatumia engine za Fuso. Kwangu mimi naona wenye mabasi ya engine za Fuso wanajali zaidi faida kuliko uhai wa abiria lakini kinachosikitisha ni kwa serikali kunyamaza huku watanzania wanakufa. Basi la kubeba abiria lazima limitize masharti yote ya ki-usalama na sharti moja kubwa ni ubora wa engine yake. Lazima liwe na engine ya basi la abiria na si vinginevyo.

3. Uhamiaji
Tanzania imekuwa kama shamba la bibi kwa kuwa na raia wa kigeni wanafanya kazi ambazo watanzania wanaweza kufanya. Maswali hapa:
- Idadi ya raia wa kigeni walioko Tanzania ni ngapi?
- Vibali au visa kwa wageni wanafanya kazi nchini zinapatikanaje?
- Wale wamachinga wa Kichina walioko Kariakoo wamepataje vibali vya kuingia?
- Kuna maduka ya wahindi (airport Dar es Salaam, KIA na Zanzibar) wameajiri wauza wahindi toka India kuja kuuza maduka. Kuna vyumba za kupanga _commercial residents zinazomilikiwa na wahindi ukichunguza wafanyakazi utakuta wanatoka India. Hivi ni kweli Mtanzania hawezi kusimamia usambazaji wa maji (kwa malori) kwenye hizi maflats ya wahindi?

4. Diplomatic passport
Ni watu gani wanatakiwa wawe na Diplomatic passport na sasa hivi ni wangapi ambao wana hizo passport?
(kuna watu wengi tu huku mtaani wana Diplomatic passport)


5. Magereza
Hali ya mahabusu na wafungwa inatisha! Kuna watu wamebambikiwa kesi wako rumande kwa miaka. Ukitembelea magereza unaweza kuzimia kwa uchungu. kuna watanzania (wasio na hatia) na wengine ni watoto wako mahabusu for years!
Hapa Lema ahimize kuundwe timu maalum ya kuchunguza hali ya jela, na mahabusu na pia kupata taarifa kamili juu ya maabusu wanaosubiri kesi kwa miaka!
Mie hoja yangu ipo pale tutakapoifanya Tanzania kama tutajifananisha kuwa ni mabasi ya kukizi haja wakati barabara hazikizi viwango, kwa mara niliposikia kuwa mabasi yenye Chasisi za malori zilifungiwa nilihisi hiyo ilikuwa siasa tu! Hatukuambiwa kitaalamu kwanini fuso ikibeba mizigo ambayo ni mizito zaidi ya idadi ya abiria haipati ajali, Hiyo yaweza kuwa injini, abayo inawezakutumika kwa gari lolote sasa pengine tungehusisha bodi zaidi ya engine. Nadhani Mh. Lema asizungumze kuhusu hili kwani halikufanyiwa uchunguzi wa kina, ni hoja iliyotolewa na Bwana Kombe ilikuwa kupunguza maswali, hayo yalikuwa ni majibu rahisi, haitofautiani sana, na Kuweka chombo cha kudhibiti mafuta, alafu unaengeza kodi kwa mafuta ya taa yanayotumiwa na wengi wenyekipato cha chini, kwa madai ya kukomesha uchakachuaji wa mafuta. Je walio ajiriwa EURA walipwa kwa misingi ipi? Kwa mimi naona chasisi ya malori ni bora zaidi kutokana na viwango vya barabara na pia kwa ubebaji abiria kupita kiasi!! labda aingie mtaalam aielezee kiundani zaidi. naamini kuwa Ajali za barabarani hutokana na uzembe wa madereva wenyewe kutoheshimu Alama za barabara, na pia pande zingine hakuna vibao vya kuashiria Alama hizo za nyakati!!
 
"Hatukuambiwa kitaalamu kwanini fuso ikibeba mizigo ambayo ni mizito zaidi ya idadi ya abiria haipati ajali, Hiyo yaweza kuwa injini, abayo inawezakutumika kwa gari lolote sasa pengine tungehusisha bodi zaidi ya engine. Nadhani Mh. Lema asizungumze kuhusu hili kwani halikufanyiwa uchunguzi wa kina, ni hoja iliyotolewa na Bwana Kombe ilikuwa kupunguza maswali,....naamini kuwa Ajali za barabarani hutokana na uzembe wa madereva wenyewe kutoheshimu Alama za barabara, na pia pande zingine hakuna vibao vya kuashiria Alama hizo za nyakati!!"


Nina mtamazamo tofauti kidogo hasa baada ya kuongea na baadhi ya haya mabasi. Ni hivi, Fuso zina uwezo wa kubeba mizigo mizito kutokana na engine zake hilo halina ubishi. Lakini pale unachukuwa engine ya Fuso na kutumia kwenye mabasi then unapakia watu uzito unakuwa kidogo matekeo yake mabasi haya yakiwa kwenye mwendo mkali yanaweweseka. Uzito wa abiria ni tofauti kabisa na uzito lets say cement, nondo etc. Na hapa ndio wananiambia hawa madereva kuna 'ujanja' wakati wenye mabasi wanaongea na serikali. Hivi inaingia akilini kweli kuwa watengeza mabasi na hata nchi nyingine wanatumia engine kuendena na matumizi lakini sisi Tanzania TUMUVUMBUA kuwa kuna mis-match kwenye hizo engine na mabasi? Na kama ni kweli kwanini basi kuna ajali nyingi ya basi hizi zenye kuchakachua? Kwa nini kwa mfano Dar express haipati ajali kama Abood au Summry? Pia fuatilia ajali za FUSO - ni nyingi mno!

Nakiri mimi sio dereva wa basi la abiria lakini niliyoandika ni baada ya kuongea na madereva wa baadhi ya mabasi haya na nilifanya hivyo maana ajali zimekuwa ni nyingi mno.


Kuhusu madereva, nakubali kuwa kuna uzembe na pengine uwezo wa madereva ni mdogo! Lakini kuna tatizo la msingi. Dereva mmoja anaendesha basi toka Dar es Salaam mpaka Mbeya au Dar es Salaam mpaka Arusha! Binafsi nilishashughudia dereva anasinzia! I was horrified. Mtu mmoja anakabidhiwa roho za watu zaidi ya 30 bila kuzingatia umbali wa safari. Najua hapa wamiliki watasema wakiweka madereva wawili gharama zitaongezeka na hivyo nauli kupanda. lakini kwa sasa watu wanalipa wa uhai wao!.

Halafu kuna mchezo wa wamiliki kuwapa 'bonus' madereva wanofika mapema!

Pia kuna jambo jingine nimekonyozwa na vijana wa kupakia mizigo pale Ubungo (wale wenye vitoroli) kwamba madereva wengi wanaweka KONYAGI kwenye chupa za maji kwa hiyo njiani utamuona dereva anakunywa maji kumbe ni Konyagi.
 
Swala la mauaji ya nyamongo na arusha ni muhimu serikali kulitolea tamko,pia wamachinga wa kichina na uhamiaji kwa ujumla maelezo yanahitajika.
 
hapo kwenye uhamiaji unaweza kutokwa na mchozi kabisa
Kuna wachina flan wanajenga kiwanda Mbagala, wanawatumikisha watoto wadogo kwenye huo ujenzi. Walikurupushwa na wizara ya kazi 12 kati ya 16 hawana vibali halali vya kuishi wala kufanya kazi nchini
 
Swala la mauaji ya nyamongo na arusha ni muhimu serikali kulitolea tamko,pia wamachinga wa kichina na uhamiaji kwa ujumla maelezo yanahitajika.

Kwenye show-rooms (sehemu za kuuza magari) kuna kabisa moja nahisi ni Pakistan. Hivi hao nao ni wawakezeji? Watanzania hawana uwezo wa kuendesha show rooms? Eneo la Namanga wamejazana na 'uniform' zao za kiteleban.
 
Back
Top Bottom