Katika kile kinachoonekana kukwama kwa mpango wa awali wa kuivuruga cdm makada wawili wa chama hicho habibu mchange na juliana shonza wanatarajiwa kujiunga na CCM ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa harakati walizoshindwa za kuibomoa cdm wakiwa ndani na sasa wameamua kuhamia kama sio kuhamishiwa CCM na wale waliokuwa wakiwatumia wakiwa CHADEMA. mpango huo unaoratibiwa hapa makao makuu ya CCM lumumba una baraka za viongozi wakuu wa CCM na unatarajiwa kutekelezwa muda sio mrefu kutoka sasa katika siku na sehemu maalumu itakayopangwa.aidha,vijana hawa wameahididwa nafasi za uongozi ndani ya uvccm na hasa kitengo cha propaganda na ubunge wa viti maalumu.
Kwa kuanzia vijana hawa watazunguka mikoa ya Kanda ya Ziwa ambako kuna mbunge mmoja wa CHADEMA(jina tunalo) ameanza kuwasafishia njia huko kwa kudai kuwa CHADEMA haina mvuto huko.lengo kuu la safari hzi ni kumchafua Dr Slaa kwa kumshambulia binafs(personal attacks) ili kuidhoofisha CHADEMA.
Habari zaidi nitaendelea kuzitoa kadri zinavyoendelea kuvuja hapa makao makuu,lumumba.