Yaani jamani Tanzania tuna bahati mbaya sana. Watoto wanafeli, hospitali hazina dawa, wamama wanajifungulia sakafuni, maji ni tabu, bei za bidhaa hazikamatiki, wananchi wanauana kwa sababu za dini.....matatizo yoooote hayo bado CCM wanaona mikakati bora inayofaa kwa sasa ni kurubuni vijana wasio na msimamo!
Hivi wazungu wakitudharau sisi waafrika na hasa sisi Watanzania watakuwa wanakosea? I just can not imagine, kwa mfano, Waziri mkuu wa Uingereza na team yake waanze kujikita kwenye siasa za mamluki kwenye hali ambayo 94% ya watahiniwa wamefeli! People will eat them alive!
Niweke tu kwenye lugha ya kiungwana, wanasiasa vijana wa CCM wanatakiwa waliletee heshma hili Taifa. Kwa sasa ni kama kichwa cha mwendawazimu, tofauti na wanavyodani. Tumekuwa kama kituko hata ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Matokeo ya watoto wetu ndiyo kabisa yanalifanya hili Taifa lionekane kama limeondoa Oxygen tank!
Hivyo basi, wanasiasa hawa vijana wa CCM wajitahidi kuonDokana na hizi siasa za ki-soviet, zilizochuja na kurudi kwenye ulimwengu wa sasa illi waindoe Tanzania kwenye hili tope la aibu.
Badala ya kujikita kwenye siasa za ki-mamluki, wangekaa chini na kutafuta ni jinsi gani ya kufikisha maji kwa wananchi, ni namna gani ya kuinua huduma za afya, elimu na hali duni ya maisha kwa jumla. Kuendelea na hii mikakati ya kiuwendawazimu, ya kurubuni vijana, ni madharau kwa watanzania, na mbaya zaidi ni kutaka kulimaliza kabisa hili taifa. Hii haikubaliki hata kidogo. Ifike mahali wanasiasa vijana wa CCM waambiwe enough is enough. Nchi inakwenda vibaya.