Mchanganuo wenye Faida kwa ufugaji Kuku wa Mayai

ASHA NGEDELE

JF-Expert Member
Jul 5, 2011
784
326
Habari zenu wafugaji na maafisa kilimo na ufugaji.

Biashara zote zimegoma kwahio nataka niingize mtaji kufuga kuku wa mayai. Sina experience lakini kwenye mchanganuo wangu wa biashara nimeweka cost ya kumlipa mtaalam wa kusimamia mradi na kuhakikisha kuku wanapata chanjo zote, uwiano sahihi wa chakula na utaalamu wote pamoja na ujenzi wa banda sahihi.

Changamoto yangu kubwa ni kwamba kila hesabu nazopiga, mwisho wa siku napata HASARA na sioni faida.

Naomba uzoefu kutoka kwa wafugaji (wanaoweka rekodi za gharama na mauzo) nijifunze wanafaidika vipi na ufugaji huu.

Naomba kuwashirikisha mchanganuo wangu unaonifanya kuona ufugaji wa Layers hauna faida bali hasara.

1. Gharama
Kuku akianza kutaga, anahitaji chakula 130gm kwa siku ambayo ni sawa na 4kg kwa kuku kwa mwezi
Maana ake ni Tzs4,000 kwa kuku kwa mwezi (kwa bei ya sh1,000 kwa kilo ya chakula)

Kwa mradi wa kuku 1,000 ni 4,000,000 chakula pekee kwa mwezi (wiki nne) bado madawa, chanjo, chakula kabla hawajaanza kutaga (Starter na Grower), kijana wa kazi, mtaalamu, vifaranga na gharama zingine.

Gharama za ujenzi wa banda, cages, vifaa vya kulishia kuku sitazijumuisha hapa sababu kihasibu ni 'capital in nature'.

2. Mauzo

Breed nzuri zaidi zinatoa 250 mayai kwa mwaka maana ake kwa siku wanataga mayai 0.7 (250/360=69%).
Kwahio kuku elfu 1,000 (kama wote watataga, kitu ambacho sio kweli) watatoa mayai 700 kwa siku ambayo ni sawa na trei 23 kwa siku.

Kwa bei Tzs5,000 kwa trei unapata Tz117,000. Kwa mwezi mauzo jumla TZS 3,500,000. Sijatoa gharama zinazoambatana na mauzo hapo.

Kwa mwezi mfugaji ana uhakika wa hasara ya (TZS400,000) ambapo kama kuku watataga kwa miezi 18 mfululizo jumla ya Hasara itakua (TZS7,200,000).

Naomba ushauri tafadhali.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi wa wafugaji nnaowafahamu wanajitegenezea vyakula wenyewe hawanunui "readymade" wanadai inapunguza sana gharama.
 
Wengi wa wafugaji nnaowafahamu wanajitegenezea vyakula wenyewe hawanunui "readymade" wanadai inapunguza sana gharama.
Ooh kumbe kuna alternative. Nlidhani kutengeza chakula ya kuku ni rocket science ndio mana wanauza bei sana. Asante kwa huu ushauri. Naamini maafisa vilimo wana huu utaalamu wa nini na nini kinachanganywa kwenye msosi wa Kuku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa wastani, Kuku mmoja mpaka kutaga anatumia Tsh 16,000/ hizo ni gharama za kunuhudumia hadi anaanza kutaga. Sasa kwa kuku 100 maana yake ni around Tsh 1,600,000/ kwa kuku 1000 ni around Tsh 16,000,000/

Hii ni hesabu rahisi sana.

Pia huwa kwenye gharama tunapiga sana kwenye msosi make ni 80 hadi 80% ya total coast.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaweza anza wakataga siku 7 zote kwa wiki, na wiki inayo fuata akataga siku 5 na wiki inayo fuata akataga siku 6 na inayo fuata alataga siku 7, na inayo fuata alataga siku 7.

Kwenye Cage wanaweza kuwa wanataga siku zote.

Kuna sababu za kibiolojia kwa nini huwa siku zingine ana miss kutaga
Kuku wa mayai kwa wiki wanataga Mara tano na bei ya tray ya chini kabisa ni 6000

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante. Hii inajumuisha gharama ya vifaranga?
Na je, kwa kuku 1,000 monthly cost ni kiasi gani kulipigia gharama za chakula n.k?
Kwa wastani, Kuku mmoja mpaka kutaga anatumia Tsh 16,000/ hizo ni gharama za kunuhudumia hadi anaanza kutaga. Sasa kwa kuku 100 maana yake ni around Tsh 1,600,000/ kwa kuku 1000 ni around Tsh 16,000,000/

Hii ni hesabu rahisi sana.

Pia huwa kwenye gharama tunapiga sana kwenye msosi make ni 80 hadi 80% ya total coast.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari, mi naomba kujuzwa na wataalamu,kuhusu namna gani naweza kutambua kifaranga jike na dume wakiwa na umri wa wiki moja?
 
Kwa wastani, Kuku mmoja mpaka kutaga anatumia Tsh 16,000/ hizo ni gharama za kunuhudumia hadi anaanza kutaga. Sasa kwa kuku 100 maana yake ni around Tsh 1,600,000/ kwa kuku 1000 ni around Tsh 16,000,000/

Hii ni hesabu rahisi sana.

Pia huwa kwenye gharama tunapiga sana kwenye msosi make ni 80 hadi 80% ya total coast.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu muelezee mleta mada namna ambayo atapata faida pia

Maana hiyo ndiyo ilikua dhumuni ya yeye kuja na huu uzi
 
Habari zenu wafugaji na maafisa kilimo na ufugaji.

Biashara zote zimegoma kwahio nataka niingize mtaji kufuga kuku wa mayai. Sina experience lakini kwenye mchanganuo wangu wa biashara nimeweka cost ya kumlipa mtaalam wa kusimamia mradi na kuhakikisha kuku wanapata chanjo zote, uwiano sahihi wa chakula na utaalamu wote pamoja na ujenzi wa banda sahihi.

Changamoto yangu kubwa ni kwamba kila hesabu nazopiga, mwisho wa siku napata HASARA na sioni faida.

Naomba uzoefu kutoka kwa wafugaji (wanaoweka rekodi za gharama na mauzo) nijifunze wanafaidika vipi na ufugaji huu.

Naomba kuwashirikisha mchanganuo wangu unaonifanya kuona ufugaji wa Layers hauna faida bali hasara.

1. Gharama
Kuku akianza kutaga, anahitaji chakula 130gm kwa siku ambayo ni sawa na 4kg kwa kuku kwa mwezi
Maana ake ni Tzs4,000 kwa kuku kwa mwezi (kwa bei ya sh1,000 kwa kilo ya chakula)

Kwa mradi wa kuku 1,000 ni 4,000,000 chakula pekee kwa mwezi (wiki nne) bado madawa, chanjo, chakula kabla hawajaanza kutaga (Starter na Grower), kijana wa kazi, mtaalamu, vifaranga na gharama zingine.

Gharama za ujenzi wa banda, cages, vifaa vya kulishia kuku sitazijumuisha hapa sababu kihasibu ni 'capital in nature'.

2. Mauzo

Breed nzuri zaidi zinatoa 250 mayai kwa mwaka maana ake kwa siku wanataga mayai 0.7 (250/360=69%).
Kwahio kuku elfu 1,000 (kama wote watataga, kitu ambacho sio kweli) watatoa mayai 700 kwa siku ambayo ni sawa na trei 23 kwa siku.

Kwa bei Tzs5,000 kwa trei unapata Tz117,000. Kwa mwezi mauzo jumla TZS 3,500,000. Sijatoa gharama zinazoambatana na mauzo hapo.

Kwa mwezi mfugaji ana uhakika wa hasara ya (TZS400,000) ambapo kama kuku watataga kwa miezi 18 mfululizo jumla ya Hasara itakua (TZS7,200,000).

Naomba ushauri tafadhali.



Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi ni kweli kuku 1000 watatoa mayai 700, ikiwa mmoja anatoa mayai 250 kwa mwaka, rejea hesabu zako kwanza mkuu
 
kwa uzoefu wangu kuku wa mayai ukifuga kuanzia kuku miatano utapata faida nzuri hata kama chakula cha kuku unanunua.

ni muhimu kufanya hesabu kabla ya mradi lakini wakati mwingine too much mahesabu kwa miradi ya kawaida inaweza kukufanya ukate tamaa unachotakiwa kufanya we anza kufuga changamoto zingine utatua mbele ya safari, ebu jiuleze kama kuku wa mayai ni hasara mbona kuna watu miaka na miaka wanafuga na hawajafirisika? jibu wanaona inawalipa.

watu wengi wenye elimu ndogo hufanikiwa kimaisha kwa sababu hawanaga muda wa kushuka mahesabu zaidi huwa wa uthubutu tu liwalo na liwe. mahesabu tuachie mainjinia.

anza kufuga kidogo huku ukitatua changamoto na kujifunza mbinu kutoka kwa wazoefu, kumbuka zipo mbinu zinatumika lakini siyo rasmi na uwezi shauriwa hata na bwana mifugo lakini mbinu hizo zinasaidia, kwa mfano mbinu ya kuzimua au kuchanganya pumba ya mpunga au ya mahindi na chakula cha dukani ili kupunguza cost. mbinu kama hizi na nyingine nyingi utazipata kwa wahenga tu na siyo vitabuni wala kwa afisa mifugo
 
kwa uzoefu wangu kuku wa mayai ukifuga kuanzia kuku miatano utapata faida nzuri hata kama chakula cha kuku unanunua.

ni muhimu kufanya hesabu kabla ya mradi lakini wakati mwingine too much mahesabu kwa miradi ya kawaida inaweza kukufanya ukate tamaa unachotakiwa kufanya we anza kufuga changamoto zingine utatua mbele ya safari, ebu jiuleze kama kuku wa mayai ni hasara mbona kuna watu miaka na miaka wanafuga na hawajafirisika? jibu wanaona inawalipa.

watu wengi wenye elimu ndogo hufanikiwa kimaisha kwa sababu hawanaga muda wa kushuka mahesabu zaidi huwa wa uthubutu tu liwalo na liwe. mahesabu tuachie mainjinia.

anza kufuga kidogo huku ukitatua changamoto na kujifunza mbinu kutoka kwa wazoefu, kumbuka zipo mbinu zinatumika lakini siyo rasmi na uwezi shauriwa hata na bwana mifugo lakini mbinu hizo zinasaidia, kwa mfano mbinu ya kuzimua au kuchanganya pumba ya mpunga au ya mahindi na chakula cha dukani ili kupunguza cost. mbinu kama hizi na nyingine nyingi utazipata kwa wahenga tu na siyo vitabuni wala kwa afisa mifugo
Safi sana muhimu kuanza mengine utajifunza mbele ya safari kupitia wajuzi waliokutangulia katika ufugaji.
 
Back
Top Bottom