Mchakato Mahakama ya Mafisadi waanza

Mchakato Mahakama ya Mafisadi waanza

Wale watuhumiwa wa ESCROW wote waliochota Mkombozi bank pamoja na STANBIC nao ni wahusika wa hii mahakama.

Tuanze nao, maana tumejua wa Mkombozi tu lakini waliochota STANBIC vyombo husika vipo kimya hawajulikani na pia hatua zilizochukuliwa hata kwa hawa wa Mkombozi hazipo wazi.

Tunaomba serikali ichukue hatua kwani ni pesa za UMMA zile.

Hii iliwanyima Kura mlipekua mkashindwa kujua pesa stanbic imetokaje.
 
Dr.Magufuli alipolizungumzia suala hili wakati wa kampeni nilidhani anatania.

Lakini amerudia tena ahadi ya kuanzisha MAHAKAMA YA MAFISADI bungeni na kusisitiza kwamba ameazimia kutimiza ahadi hiyo.

Kwa msingi huo basi, kinachofuatia sasa ni serikali kupeleka mswada wa uanzishwaji mahakama ya mafisadi bungeni. Baada ya wabunge kujadili na kupitisha mswada huo, Raisi atausaini kuwa sheria.

Sasa hivi tayari tunayo sheria ya UHUJUMU UCHUMI ambayo basically ndiyo sheria ya ku-deal na mafisadi.

Kwa mtizamo wangu, ili sheria ya kuanzisha mahakama ya mafisadi iwe tofauti na sheria tulizonazo sasa hivi, itabidi iwe na maboresho niliyoyataja hapo juu, na zaidi iwe na chombo chenye MENO cha kuchunguza makosa na rushwa, uhujumu uchumi, na ufisadi, pamoja na kushtaki.

Mapendekezo yangu ni matatu:

Kwanza, PCCP iwe HURU kuchunguza na kupeleka mashtaka mahakamani bila kuingiliwa;
Pili, kinga ya Rais iondolewe ili asitokee fisadi yeyote yule akasingizia kwamba alielekezwa na rais;
Tatu, PCCB iwe na uwezo wa kuchunguza na kushtaki makosa na ufisadi hata uliofanyika kabla ya kuundwa kwa mahakama hii mpya.

cc Pasco, Mzee Mwanakijiji, Mag3, MsemajiUkweli, Nyenyere, Nyani Ngabu, The Boss, Nguruvi3
 
Mheshimiwa Rais,siasa ziweke pembeni fanya kazi,hizi porojo zilizotumika kwenye campaign hazifai tena,kasi yako ni nzuri ,if I may ask,it cost how much kuazisha hiyo mahakama,? Je inamaana mahakama zilizopo zinashindwa hukumu mafisadi? Nini ni opportunity cost kuazisha mahakama mpya au kuzipa meno mahakama zilizopo na wewe kuruhusu Dpp awashitaki wote mafisadi,? Ni kweli unatuambia mahakama zetu zimefail hukumu jinai? No bora ufukuze judge mkuu,Dpp,mkurugenz wa takukuru kama wanakukwamisha kuwapeleka mahakamani hao mafisadi kuliko hizi terms za mchakato wa mahakama ya mafisadi,maana hata ungeazisha mahakama kumi mpya bado zitakuwa chini ya watu wale wale
 
ikiwa tayari wapiti profile za mapresida wastafu atakayekutwa mchafu zaidi awe mfano kwa taifa.
 
Watu hawaelewi mahakama hii haitahangaika na kesi za zamani itadeal na kesi mpya tu.
 
Are we dealing with retrospective/retroactive law?

Ninapenda kusikia kwanza mchakato wake ili niweze kutoa neno lenye mantiki kuhusiana na Mahakama ya Mafisadi.

Yes, Ili kufanikisha adhima ya Rais Magufuli, taasisi kama PCCB na DPP lazima ziwe huru na zenye viongozi wazalendo.

Kubwa zaidi, kwa siasa zetu, nani atamfunga paka kengele kwenye hoja ya kinga ya Rais kwa sababu kubadilisha kifungu cha Katiba ya nchi kinahitaji 2/3 ya wabunge wakubali.

CHADEMA ambao hapo nyuma walituaminisha ni wapambanaji wa maslahi ya wananchi, tumewaona walichokifanya wakati wa kuteuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA. Wamedhihirisha ni wachumia tumbo tu.

Kwa sasa wabunge wa CHADEMA/UKAWA wamoja na wabunge wengi wa CCM katika kuongezewa pesa za vikao naza kununua magari.
 
kinga ya rais ipo kikatiba, mahakama haiwezi kuvunja katiba
 
Mahakama na prosecutors wawe huru bila kuingiliwa na Rais
kila kesi kama wana ushahidi waende mahakamani moja kwa moja
kusiwepo na nguvu ya kuifuta kesi nje ya mahakama...

Rais asiwe na nguvu ya kuamua kesi ipi iende na ipi isiende
 
Are we dealing with retrospective/retroactive law?

Ninapenda kusikia kwanza mchakato wake ili niweze kutoa neno lenye mantiki kuhusiana na Mahakama ya Mafisadi.

Yes, Ili kufanikisha adhima ya Rais Magufuli, taasisi kama PCCB na DPP lazima ziwe huru na zenye viongozi wazalendo.

Kubwa zaidi, kwa siasa zetu, nani atamfunga paka kengele kwenye hoja ya kinga ya Rais kwa sababu kubadilisha kifungu cha Katiba ya nchi kinahitaji 2/3 ya wabunge wakubali.

CHADEMA ambao hapo nyuma walituaminisha ni wapambanaji wa maslahi ya wananchi, tumewaona walichokifanya wakati wa kuteuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA. Wamedhihirisha ni wachumia tumbo tu.

Kwa sasa wabunge wa CHADEMA/UKAWA wamoja na wabunge wengi wa CCM katika kuongezewa pesa za vikao naza kununua magari.

..PCCB lazima wapewe meno ya kuchunguza hata Ikulu na Raisi.

..maadamu unaamini kwamba CDM ni wachumia tumbo wasiokuwa na maana yoyote, basi CCM wanapaswa kuzibwa ombwe lililotokea kwa kubeba dhima ya kuwa chama kinachopinga ufisadi.

..CCM ndiyo wenye 2/3, kwa hiyo "all eyes on them." lazima wao ndiyo wawe mstari wa mbele ktk kupitisha sheria itakayounda mahakama yenye nguvu na uwezo wa kushughulika na ufisadi.

..kama Wabunge watakuwa na kigugumizi ktk kuondoa kinga ya Raisi , basi Dr.Magufuli aingilie kati kusisitiza kinga ya kushtakiwa iondolewe kwake yeye pamoja na Maraisi waliomtangulia.

cc The Boss
 
Last edited by a moderator:
Kwa kasi hii inavyokwenda sero zitajaa sasa, hivi naomba jaji mkuu harakisha hii mahakama ya mafisadi sero mwishowe zitajaa manake kila siku watu wanaswekwa ndani. Majizi mengi mno na hayasikii hadi yatupwe korokoroni. Ukichelewa chelewa nawewe utarukiwa na uchafu kutoka kwenye majipu.
 
Awateue wale majaji waliopata mgawo wa Escrow wasimamie mahakama hii ya mafisadi!!!!!!!
 
Kuna sababu kwa nini Mwakyembe ameteuliwa kuwa Waziri wa Sheria, kwa waliokuwa wanakejeli kila siku kwamba ,,kama kweli Lowasa ni fisadi ni kwa nini ashitakiwi?" sasa kiu yao itakaushwa, naam, fisadi Lowasa atashitakiwa na atatiwa pingu hivi karibuni, msiwe na hofu, ile msianze tena kulia lia hapa kwamba anaonewa kwa sababu ni chadema!
 
Back
Top Bottom