Mchakamchaka ya CUF chali, yageuka chama cha press conference

Mchakamchaka ya CUF chali, yageuka chama cha press conference

Seif al Islam

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2011
Posts
2,156
Reaction score
640
Ni jambo ambalo wabashiri wa mambo na wafuatiliaji wa siasa za upinzani hapa Tanzania tulilibashiri mapemaaa.
Hili si jingine bali ni kudorora na baadae kufa kifo cha asili kwa kile kilichoitwa na CUF kuwa oparesheni mchakachaka hadi 2015 ikiwa na kauli mbiu ya dira ya mabadiliko yaani vision for change(V4C).

Oparesheni hii iliyoanzishwa kimamluki na bila utafiti wala dira inayoeleweka ililenga hasa kuiga(imitation) na pia kudhoofisha kile kinachoitwa movement for change(M4C) iliyoasisiwa kwa ustadi mkubwa na CHADEMA na kupata mwitikio chanya kutoka kwa wananchi.

Kuonyesha namna ambavyo ilikosa dira, oparesheni hii ilianzia huko Arusha (ngome ya CHADEMA) ambako pamoja na kukosa msisimko wowote wa maana CUF walifanya maigizo ya kuwapokea waliowaita vigogo wa CHADEMA na baada ya hapo mikutano na oparesheni zile zilififia(kama tulivyobashiri) na sasa sioni kama ntakuwa sijatenda haki kama nikisema wazi kuwa movement ile ya kimamluki imekufa kifo cha asili (natural death) cha kujifunza hapa ni kimoja tuu kuwa watanzania wamechoka maigizo ya CCM na vibaraka wao. Wanataka kuona mtu au chama kinachoonyesha mwelekeo wa kuwakomboa kwelikweli na sio kuwapotezea muda.
 
Chama cha maandamano na wapanga mipango ya ugaidi je mbona hukisemi?
 
RIP CUF, Rip Mkigoma,Rip Katani...wananchi tuliwapendeni sana ila Mungu amewapendeni zaidi. RIP CUF!
 
V4C ni moja ya mbinu za kuwazingua wananchi tu kama vile ilivyo bendera ya ADC (Sawa na Bendera ya CDM) na sasa naona wanamtumia dogo Jerry Silaa (Jina linashabihiana) kuzunguka kwenye mikutano yao.

Unajua watz kama tungekuwa tunajitambua kwa kweli CCM wanatufanya sisi wajinga 100%. Wanadha wakiweka vitu flan simila basi kuna watu hata kumi wanaweza kuingia mkenge...
 
chama hiki kimebaki na mtu mmoja tu mpambanaji -- Mtatiro:

Mtatiro why don't you join the winning team?
 
Naunga mkono hoja yako. Kwanza watambue CUF halijafa na haliwezi kufa kamwe wakibisha waje mikoa yote ya Pwani na Kusini waone jinsi CDM kivyo dharauliwa (kimekosa wa kukiunga mkono) binafsi mimi ni mpinzani, lakini nikheri ya CCM kuliko CDM.
Haya mkuu,ila yetu macho,maana hata Igunga mlisema hivyohivyo ila kura 12,000 zikashuka hadi 2,000!
 
Anae sema CUF imekufa huyo atakua na hitlafu kwenye akilizake. Kwanza anatakiwa atambue kua mpinzani wa kweli ni CUF wengine ni vishuruala tu. Angalia historia ya CUF na misuko suko iliyo ipata kama mpinzani angalia vifungo walio pitia viongozi wake akina Maali Seiph, Juma Hadj Duni wote washapinda ubavu mmoja kwasababu ya harakati zao za kuitetea HAKI ona Profesor alivyo chezea kipigo pale keko yote ni harati za kweli. Sasa kiongozi gani ndani ya CDM aliye pata misuko suko japo kupigwa kofi tu. Hapo utagu ndua kua CDM ni chombo kilicho undwa kunyamazisha upinzani, ni isia zilizo anzia kanisani na kupokewa na waumini wake kama mkombozi wao.
 
HAKIIII "sawaaaaa" HAKI SAWA KWA NANIII? "kwawoteeee" NAASIE PENDA HAKIII? .......................
 
Prof Lipumba na Mtatiro naona ni watu right ambao wapo kwenye chama wrong.
Sijui kwa nini hadi leo hawajagundua hilo!!
 
anae sema cuf imekufa huyo atakua na hitlafu kwenye akilizake. Kwanza anatakiwa atambue kua mpinzani wa kweli ni cuf wengine ni vishuruala tu. Angalia historia ya cuf na misuko suko iliyo ipata kama mpinzani angalia vifungo walio pitia viongozi wake akina maali seiph, juma hadj duni wote washapinda ubavu mmoja kwasababu ya harakati zao za kuitetea haki ona profesor alivyo chezea kipigo pale keko yote ni harati za kweli. Sasa kiongozi gani ndani ya cdm aliye pata misuko suko japo kupigwa kofi tu. Hapo utagu ndua kua cdm ni chombo kilicho undwa kunyamazisha upinzani, ni isia zilizo anzia kanisani na kupokewa na waumini wake kama mkombozi wao.

haya yote yamewasaidiaje watanzania kuondokanaa na ukandamizaji wa ccm?
 
Anae sema CUF imekufa huyo atakua na hitlafu kwenye akilizake. Kwanza anatakiwa atambue kua mpinzani wa kweli ni CUF wengine ni vishuruala tu. Angalia historia ya CUF na misuko suko iliyo ipata kama mpinzani angalia vifungo walio pitia viongozi wake akina Maali Seiph, Juma Hadj Duni wote washapinda ubavu mmoja kwasababu ya harakati zao za kuitetea HAKI ona Profesor alivyo chezea kipigo pale keko yote ni harati za kweli. Sasa kiongozi gani ndani ya CDM aliye pata misuko suko japo kupigwa kofi tu. Hapo utagu ndua kua CDM ni chombo kilicho undwa kunyamazisha upinzani, ni isia zilizo anzia kanisani na kupokewa na waumini wake kama mkombozi wao.

yani kufunga ndoa na ccm ndo upinzani wa wakweli acha kulazimisha fikra za mabua
 
CHADEMA bana, yaani mnailinganisha CHADEMA na CUF kwa mikakati? This is laughable!

V4C inaendelea mikoani kama kawaida wakati CHADEMA wameshughulishwa na mambo yasiyowajenga kama: Issue ya Lwaka na Ludo.

CHADEMA ina uhai kwenye mtandao sio kwa wananchi on the ground.

By the way kwanini mnashambulia CUF badala ya CCM?
 
Back
Top Bottom