Mch. Rwakatare avunjiwa nyumba

Mch. Rwakatare avunjiwa nyumba

Soma post yako niliyorespond kwake. Naona unaandika vitu halafu unasahau.


Nimeshangaa kidogo unavyonitakia shule njema (sijui una maanisha nini?) pili, nadhani umeisoma juu juu post yangu maana ulichojibu sicho nilichokiandika kabisa. Hakuna sehemu nimesema huwezi kuhoji authority (iwe mahakama, wizara au manispaa) ila nimekwambia wewe kuwa kama huna details za court jugdement sidhani kama unaweza kusema kwa authority kuwa hili swala liliamuliwa in favour ya Lwakatare. It's fine umesema tuna argue on basis ya taarifa za gazeti. Lakini ni taarifa za gazeti hili hili ndo limeandika kuwa huyu mama yeye ndo alizuiwa kwa amri ya Baraza la Ardhi asiendelee na ujenzi wowote. Kilichoandikwa ni kuwa kesi ipo mahakamani na hiyo stop order sijui mwenzetu umeitoa wapi. Ndo maana tunakuuliza kama upo jirani na mgogoro huu na una hizo taarifa za ziada ziweke hapa. Unless, naona umeamua kumtetea mvunjaji wa sheria. Inawezekana una maslahi naye.
 
Rungu la Sheria limetua kwa Mch.Gertrude Rwakatare,Mchungaji Kiongozi wa 'Mlima wa Moto'.Ni nyumba yake iliyokuwa Mbezi Beach. Alijenga katika eneo la mjane alilolivamia. Hatimaye sheria imechukua mkondo wake. Mjane alilia kwa furaha. Nyumba hiyo ilisajiliwa kwa jina la mtoto wa Mch.Rwakatare. Uboboaji huo ulifanywa chini ya ulinzi mkali wa askari waliokuwa wamesheheni silaha za moto.

Wakati wa ubomoaji,alijitokeza mtu mmoja aliyedai kuwa ni Wakili wa mwenye nyumba akiwa na nyaraka za kimahakama zinazodaiwa kuweka zuio la kubobolewa kwa nyumba hiyo.Hatahivyo,alipuuzwa na ubomoaji kuendelea kama ulivyopangwa. Kweli sheria ni msumeno!

Chanzo: ITV



CHANZO: Mwananchi

Mkuu sema mwizi wa umeme kavunjiwa nyumba zake, mheshimiwa mwenye uchungu na nchi yake huwa anafanya mambo yake kiuadilifu na kufuata sheria na taratibu zote za nchi. Hilo gume gume rwakatare lilihonga wanawake chain za dhahabu ili apate viti maalum apate kufanya dhulma anazozifanya. Shame on her!


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Ubishi wa kisheria utatufikisha mbali kwa sababu tafasiri yako, shria uliyonukuu na kilichofanyika havifanani. Hatujaaambiwa alipwewa notice ya kuondoka na vitu vyake. Kilichosemwa ni amri ya kuvunja. Usiwe mbishi kama hujaelewa. Unajua sheria siku zote haifuati utashi wako bali huangalia haki. Fahamu commissioner hayuko juu ya sheria, na anapaswa kuifuata siyo sheria imfuate.

Wengi hapa wanafurahia na kuchukua sehemu kwa ajili ya wivu wala si kwa hoja dhidi ya mama rakwatare.

Wewe ungekuwa ni mpembuzi ungeitafuta kwanza hii sheria usome. Sasa hapa unataka kuleta ubishi wakati hujasoma hichi kipengele kimeandikwaje. Sheria sio novel, inaandikwa kwa misingi ya natural justice. Lazima sheria inamtaka apewe notice, then aondoe au avunje kwa ridhaa yake akikaidi commissioner kapewa mamlaka ya kuondoa. Ndugu huwezi kuwa na facts kama hutosoma. Hakuna hata sehemu moja nimesema commissioner yupo juu ya sheria, nakushangaa unavyonilisha maneno. Narudia tena, nakushangaa unavyomtetea huyu mama ambaye yeye ndo alikiuka amri ya baraza la ardhi. Na sijui hiyo court order unayosema ilitolewa imeitoa wapi, maana gazeti hilo unalolisema wameandika kesi ipo mahakamani.
 
Unaelewa maana ya Win win situation kama nilivyosema?

win-win
| Definition | Thesaurus | Translations
Also found in: Acronyms, Wikipedia
win-win (w n w n )
adj.
Of or being a situation in which the outcome
benefits each of two often opposing groups.

~~~~~~
Hapa tupo katika lengo la kujenga,kutoa ushauri positive,mie najua gharama za ujenzi,najua uchungu wa ardhi,kumpoka mjane kiwanja sio vizuri pia kubomoa nyumba kisa uvamizi nayo haijakaa vizuri kama mama hataki kuuza basi alipe 800m ya nyumba alizotumia rwakatare kujenga kama hana basi wauze mama mjane apate chake,rwakatare apte 800m yake na serikali ilambe kodi hiyo ndio win win situation,usiwe mtu wa kubwabwaja toa michango ya kujenga!!!

Sikubaliani na non sensw yako!!! Kwahiyo wewe unaenda safari, nakuja nawatoa vijana wako ndani mwako. Nasema hii nyumba ni yangu. Then unakuja unakuta ulinzi mkali. Unaenda mahakamani. Then wanasema nyumba ni yako kisheria. So, i mean time mimi nikaongeza ongeza hapo. Je utanilipa? Nikuachie nyumba yako? Hakuna laws au such mitigating tacts za aina hii hata siku moja. Haki ni haki yake !


The King.
 
Hiv vitu vickie tu,halaf pita kimya mtu akuvunjie mjengo kama hizo picha,unaweza ukapiga mtu risasi au ukamroga kabisa,au ikishindikana ukatafuta wauaji wa kukodi,watu wanashabikia kama vile sheria iliyovunjwa ni hiyo tu mbona ziko nyingi imagine ni ww halaf ukoment,mtu hata kibanda cha njiwa hujawah kujenga unajifanya bush lawyer,hiv sehem kiasi gan ya tz imepimwa ili tusijenge ovyo ovyo,cku zote akili ya watu weusi ni kurudishana nyuma ili wote tukose,mtu anayebomoa anajua cost ya hiyo decra.
 
[h=2]Mch. Rwakatare avunjiwa nyumba[/h]
Rungu la Sheria limetua kwa Mch.Gertrude Rwakatare,Mchungaji Kiongozi wa 'Mlima wa Moto'.Ni nyumba yake iliyokuwa Mbezi Beach. Alijenga katika eneo la mjane alilolivamia. Hatimaye sheria imechukua mkondo wake. Mjane alilia kwa furaha. Nyumba hiyo ilisajiliwa kwa jina la mtoto wa Mch.Rwakatare. Uboboaji huo ulifanywa chini ya ulinzi mkali wa askari waliokuwa wamesheheni silaha za moto.

Wakati wa ubomoaji,alijitokeza mtu mmoja aliyedai kuwa ni Wakili wa mwenye nyumba akiwa na nyaraka za kimahakama zinazodaiwa kuweka zuio la kubobolewa kwa nyumba hiyo.Hatahivyo,alipuuzwa na ubomoaji kuendelea kama ulivyopangwa. Kweli sheria ni msumeno!

Chanzo: ITV


Serikali yabomoa nyumba za mamilioni Mbezi Beach


mbezi.jpg


Katapila likibomoa moja ya nyumba nne za Tibe John katika eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam jana.
Picha na Beatrice Moses.

Na Beatrice Moses na Ally Nguba, Mwananchi


Kwa ufupi

Nyumba hizo zilizokuwa katika Kitalu namba 314 chenye mgogoro wa umiliki, zilikuwa zinajengwa na John kwa kasi bila kujali kuwa kulikuwa na amri ya Baraza la Ardhi ya kuzuia ujenzi huo hadi mgogoro uliohusu eneo hilo utakapotatuliwa.


Dar es Salaam.

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imebomoa nyumba nne zenye thamani ya Sh800 milioni mali ya Tibe K. John zilizojengwa katika eneo la Mbezi Beach bila kibali na kinyume na sheria za mipango miji.


Nyumba hizo zilizokuwa katika Kitalu namba 314 chenye mgogoro wa umiliki, zilikuwa zinajengwa na John kwa kasi bila kujali kuwa kulikuwa na amri ya Baraza la Ardhi ya kuzuia ujenzi huo hadi mgogoro uliohusu eneo hilo utakapotatuliwa.

Wakati wa ubomoaji huo uliosimamiwa na Manispaa ya Kinondoni chini ya Mhandisi Baraka Mkuya, kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi wenye bunduki na mabomu ya machozi, wakiongozwa na Ofisa wa Operesheni, Emmanuel Tille.

Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Alphayo Kidata alisema kuwa ametoa agizo hilo kwa sababu sheria zinapaswa kuzingatiwa na kwamba nyumba hizo zilijengwa bila kuwa na kibali chochote cha manispaa kama inavyotakiwa.

“Kuwapo kwa kesi mahakamani hakuzuii sheria nyingine kutekelezwa, wamejenga hawana kibali,” alisema Kidata.

Wakili wa John, Emmanuel Augustino alidai kwamba hatua hiyo imetekelezwa kibabe na katibu mkuu, kwa kuwa kuna kesi wamefungua katika Baraza la Ardhi Kinondoni ambayo inaendelea kusikilizwa.

“Anajua wazi kuwa alichokifanya ni kinyume cha sheria, ameingilia uhuru wa mahakama,” alisema.

Augustino alisema hawajui watamshtaki nani ili kudai fidia, hasa kwa kuwa katibu mkuu alitoa agizo la mdomo na hakuna barua yoyote aliyoandika ambayo ingeweza kutumika kama ushahidi.

Wakili wa anayedaiwa kuwa mmiliki wa kiwanja hicho cha Janet Kiwia, ambaye ni Howard Msechu kutoka katika Kampuni ya Uwakili ya Homac, alisema wamefurahishwa na hatua hiyo kwa sababu walikiuka amri ya Baraza la Ardhi ya kupiga marufuku shughuli za ujenzi kuendelea.


CHANZO: Mwananchi​
 
Hawa Manabii wa CCM wanakera sana... hata Wajane wanawavamia na kuwadhulumu?... Kwani biashara zake za Sembe hazimtoshi?...
 
Hawa Manabii wa CCM wanakera sana... hata Wajane wanawavamia na kuwadhulumu?... Kwani biashara zake za Sembe hazimtoshi?...
mkuu nadhani pia ni muda muafaka kubomoa Mbowe club aka billcanas. iludishwe NHC. Ruzuku anazojilipa zinamtosha Dj Zero.
 
Ukishaamua kuuza sembe mjane ni kutu gani......huku ukuhubiri neno kwa mapovu mengi.
 
Sheria ina kanuni zake na wala haihitaji jazba. Sijabariki dhuruma na wala hilo halina dispute lakini Janeth Kiwia si mjane. Marehemu aliyekuwa mmiliki wa eneo lile hakuwa mme wake bali ni shemeji yake. Ujane hapa haupo ila ni gear ya kutafuta sympathy and mob support.

Ninachokiongea ni kufuata sheria. Kwa nini waliendelea kuvunja wakati kuna Court Stop Order? Wanajua mahakama ilitaka kufanya nini juu ya hil shauri? Wizara ya ardhi na halmashauri si mahakama watoe court orders. Ndiyo maana kuna mahakama ambapo jambo lolote lisiloafikiwa linastahili kusikilizwa na kuamuliwa. Badala ya kuamua nyumba zivunjwe, Manispaa ya kinondoni na wizara ya ardhi, walipaswa kum support yule mama Mahakamani, hasa baada ya kufahamu kwamba shauri hili tayari lipo mahakamani na kuna stop Order.

Vinginevyo, ukiukwaji wa sheria kwa vyombo vya serikali ni chanzo kikubwa cha kukosekana kwa heshima kwa sheria na ni mlango wa watu kuchukua sheria mkononi na machafuko.

Sasa mama Rwakatare amefile Civil Case, anadani million 800 kupitia mahakamani. Sijui defendants watatoa utetezi gani wa kuvunja nyumba wakati shauri liko mahakamani na kudharau amri halali ya mahakama iliyozuia nyumba isivunjwa.

Naomba tuache mob psychology, kuchangaanya hoja, na kushabikia kwa lengo la utashi wa kumkomesha mtu kinyume cha sheria.
Yap, nimeipenda analysis yako, definitely utakuwa lawyer by profession?
 
Hii ndio hasira ya kiyahudi akimwaga mboga mwaga ugali toboa na sufuria asirudi jikoni kupika tena
 
Kwahiyo unatuambia tufanyeje!

Kwani kila siku habari zikiletwa humu zinakuwa zinataka watu wafanyeje? Hahahaha wewe utakuwa unasali Milima ya Moto wewe pole sana.Maana ya habari kuletwa humu ni kupashana matukio yanayotokea kila pande nne za dunia.By the way wewe kwa nini unaangali taarifa ya habari ama unasoma magazeti?
 
Hivi kuliko hii sheria ya kuvunja nyumba kwa nini isingekuwepo nyingine ambayo kama wewe umedhulumu kiwanja cha mwenzako na mahakama imetoa hukumu, sasa hukumu ingekuwa badala ya kuvunja nyumba iliyopo ni bora mlalamikaji apewe hiyo nyumba sababu ilijengwa kwenye kiwanja chake, akishapewa hapo sasa ni maamuzi yake, aishi ama avunje, kuliko kupoteza nguvu na mali bure na kutiana umaskini wa buure, Mfano huyo mama mjane tayari angeshajipatia mtaji wa kutosha, angemalizia tu kisha angepangisha nyingine na pia angetoa ajira na kodi pia angelipa sirikalini, sasa wamevunja hapo huenda huyo mama hana hata uwezo wa kusimamisha hata nyumba ya vyumba viwili vya haraka, hebu tubadilike jamani, lile lilikua booonge la mtaji kwa mama.
Mbona polisi wakikamata magari ya ujambazi na yakikaa muda mrefu bila kuja kutambuliwa na wenyewe hatusikii kama yalichomwa moto ama kuvunjwa vipande?
Huko ni kuirudisha nchi yetu nzuri nyuma.
 
Mbona picha inaonyesha vinavyovunjwa ni vibanda tu, hekalu (pichani) mbona halionekani likivunjwa??
Hapa nami machale yananicheza pia, mwenye picha kamaili atueleze vizuri tafadhali.
 
safi sna hii ni kuonyesha uwajibikaji wa viongozi :::::::tunahitaji nchi hii iendeshwe kwa mifano hii kila idara tutafika
 
Mahakama zisigeuzwe kichaka cha waharifu kubuy time, hili ni fundisho kwa wote

Copy: Zitto
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom