Mch. Lusekelo na siasa

Mch. Lusekelo na siasa

Asilimia kubwa ya watu wana comment huu uzi inaonekana hata kipindi chenyewe hawajakiangalia, kwanza aliponda sana nguvu inazotumia polisi dhidi ya waandamanaji, alihoji pia, ilikuaje waislam waende waandamane hadi makao makuu ya polisi, yaani wizara ya mambo ya ndani?

Kwasababu watu wameisha kuwa sugu, akasema, sifa moja wapo ya kumchagua kiongozi (alitolea mfano, kama unataka kumchagua mzee wa kanisa) angalia, je anapendwa na watu? kila ukimtazama, unaona kuna watu wengi wanamzunguka, hivi hapa kwanini tusiseme alikuwa anawafagilia indirect akina Dr. Slaa, kwani pamoja na kwamba wanapokuwepo kunakuaga na tension kubwa sana ya polisi, still watu wanaenda wengi tena kwa nauli zao.

Tujifunze kuchangia kitu kama kweli tunakijua vizuri badala ya kuponda kila kitu au kupongeza kila kitu while hatuna details za hicho tunacho kisema.
 
Sijamsikia Mchungaji Lusekelo jana ila nimekuwa nikimfuatilia kwa mda kidogo juu ya kile anachokihubiri na kile biblia inachomaanisha ni vitu viwili tofauti. Wachungaji walio na busara bila hata kulazimika kujificha katika lugha ya kilaghai iliyozoeleka kwa sasa kama ''Mungu ameniambia,Mungu amenionyesha'' hawezi kuonyesha hisia zao za upenzi kwa chama cha siasa. Maana wanajua wazi kuwa kondoo zao wana vyama na wanayo haki ya kuamini katika mojawapo ya vyama. Sasa mtumishi wa Mungu hapaswi kuwa mshabiki bali mzungumza ukweli akikemea, kuonya na kuifundisha njia ya haki kwa gharama yoyote hata kama itakulazimu kufa. Kifupi ni kwamba watumishi wengi wa kipentekoste siku hizi wamezigeuza madhabahu kuwa kijiwe cha porojo na fitna za kujitafutia mkate wa siku. Wamesababisha ahadi za Bwana Yesu kwa kanisa lake ziwe changa la macho. Hata hivyo kuna baadhi na wachache sana waliosimamia ukweli na hawa ndio nguzo la tumaini ya imani kwa Bwana Yesu. Mungu awabariki watumishi waaminifu waliojiweka mbali na propaganda za kisiasa.
.
 
Mchungaji Lusekelo, nakushauri uchague kuwa mwanasiasa ili upate muda wa kutetea sera za CCM au Ubaki kuwa Mchungaji ili utetee sera za Ufalme wa Mungu. Vinginevyo ni lazima utawachanganya washirika wa kanisa unaloliongoza pia utaharibu taswira nzuri ya Kanisa la Mungu. Pia usifikiri kuwa wanaoabudu hapo kanisani kuwa wote ni CCM kwa sababu ww ni CCM hapana. Please!!!
 
Mch. Lusekelo anajisahau na kujiona kwamba kesha fika na yeye ni SUPER katika kila jambo kuliko watumishi wengine wote Tanzania na pengine Afrika Mashariki na ya kati, akiwa ni mtumishi wa Mungu kweli aikemee roho ya kujisikia na kujiona na kujikweza! anao wafuasi wengi lakini jinsi anavyoenenda na kauli TATA za kupinga watumishi wengine wa MUNGU afahamu kuwa watu wanachuja na kuangalia mbivu na mbichi. Katika dunia hii sijawahi kuona Mchungaji anafupwa (kutuzwa) manoti akiwa madhabahuni, yeye anaiona hali hiyo ni kukubalika lakini aangalie MUNGU wake analifurahia jambo hilo au
 
mnafiki mkubwa,hajitambua nafasi yake ktk jamii laa sivyo asingekuwa anaongea huo ujinga
 
Anthony Isyu lya kyala likutobile, wandile kangi ni syasya sya sisiemu kangi! Po sikukutoba wakukaya. Bhangogile UNDAVITI UWAMWANGOSI ukapilika? Sili bule bule kangi?
 
kweli nimeamini sasa kua JF ni jukwaa la umbea,kwa yeyote aliangalia kipindi ataungana na mimi kua muanzisha mada hakuelewa hata kilichosemwa na sijui kaja na mtazamo huu kutoka wapi,inakera inaudhi sana kuwadanganya watu na watu hao pasipo kuutafuta ukweli kuchangia kitu wasichokijua wala haki exist na kujisifu kua ni great thinkers,nathubutu kuwaita wajinga,Yes waliochangia kusuport hii mada ni wajinga
 
Huyu Arnold simwelewi vizuri hivi yupo sawa kweli.Hivi anafikili chama ni bendera na jina.Chama ni Viongozi na kama viongozi wamekuwa mafisadi chama hicho hakifai.Na kama yeye ni mwanachama anaweza kujua kwamba mfumo wa CCM mzima umeoza.Ina maana hafahamu kwamba hii ni nchi ya Tatu kwa kutoa zahabu nyingi Afrika, uliza sasa pesa kiasi gani zinatoka kwenye zahabu,na kwa taarifa yako kwa sababu ya mikataba mobovu iliyoiingiwa na serikali ya CCM, Migodi hailipi kodi kiasi hicho, je unajua kwamba Viwanda vya Pombe vinatoa /kulipa kodi nyingi kuliko Migodi ambayo mikataba yake mibovu imeingiwa na CCM.Na kwa sasa nchi hii inatarajia kuwa ya pili au ya tatu kwa gesi nyingi duniani lakini kwa hakika wananchi hawatafaidi matunda ya Gesi bali watakaofaidi ni Mafisadi walewale wa CCM. Tunahitaji Serikali mpya watu wapya.CCM ni mbaya na haifai. Labda kwa Arnord inamfaa. Na kuna baadhi ya shule zina walimu watatu kwa Arnold hii ni sawa.
 
Asilimia kubwa ya watu wana comment huu uzi inaonekana hata kipindi chenyewe hawajakiangalia, kwanza aliponda sana nguvu inazotumia polisi dhidi ya waandamanaji, alihoji pia, ilikuaje waislam waende waandamane hadi makao makuu ya polisi, yaani wizara ya mambo ya ndani?

Kwasababu watu wameisha kuwa sugu, akasema, sifa moja wapo ya kumchagua kiongozi (alitolea mfano, kama unataka kumchagua mzee wa kanisa) angalia, je anapendwa na watu? kila ukimtazama, unaona kuna watu wengi wanamzunguka, hivi hapa kwanini tusiseme alikuwa anawafagilia indirect akina Dr. Slaa, kwani pamoja na kwamba wanapokuwepo kunakuaga na tension kubwa sana ya polisi, still watu wanaenda wengi tena kwa nauli zao.

Tujifunze kuchangia kitu kama kweli tunakijua vizuri badala ya kuponda kila kitu au kupongeza kila kitu while hatuna details za hicho tunacho kisema.
Nimekugongea LIKE na nimekuongezea Reputation power zako kwa bandiko lako hili na nisign kama Guest kwenye wall yako yako ya Guests. Tumepungukiwa na Great Thinker humu sasa watu wanapayuka payuka tu.
 
Mchungaji Antony Lusekelo kwenye kipindi chake cha chanel ten usiku huu, kasema CCM ni chama cha ukombozi. Ameonesha kujipendekeza sana kwenye chama hiki. Aidha amedai mvua za el nino zilizotabiriwa na mamlaka ya hali ya hewa hazitakuwepo, kwa mujibu wa maono yake.

Hee anapingana na wataalam watabiri wa mvua?
 
He is an opportunistic, sitashangaa nikisikia kesho kasema CHADEMA ni chama kilichoshushwa toka peponi! Halafu pia check na oudience inayomsikiliza utagundua kuwa anasema hivyo kwakuwa anajua anahubiria watu wa aina gani. Ndio hawa hawa wanaopendekeza uchumi wa nchi uombewe ili ukue
 
Kama karibu watumishi wote wa Mungu wanaikemea serikali iliyoko madarakani kwa maana ya chama tawala -CCM,yeye anaongea mambo ya hovyo kuisifia CCM eti imetoa mchango wa ukombozi wa Afrika. CCM ya wakati ule kwa maana ya TANU si ya leo. Sasa hivi CCM ni ya kifalme,kifisadi,kibinafsi,kikandamizaji na uchafu wote unao endana na huo. Halafu namshangaa kuhusu maono yake eti hakuna mvua za el nino. Mbona hakutoa maono yake mwanzoni wakati wana hali ya hewa walipotabiri. Nabii wa kweli anatoa utabiri kabla mtu wa kwaida hajajua. Kapima upepo kaona Septemtember inayoyoma bila kuwapo kwa dalili za el nino. Unabii wake bado nautilia mashaka kwa mengi.
 
Huna tofauti na wale wanaopinga filamu na cartoon ya kumdhalilisha mtume wakati hata hawajaiona. hear saying ni mbaya sana, unaweza kulishwa sumu kwa mtazamo wa mtu mmoja binafsi.

Chadema kama ndio ina watu wenye mtazamo huu tukiwapa nchi mtageuka madikteta kama hamtaki kusikia habari kinyume na matakwa yenu. Lusekelo hana tatizo lolote kwa kipindi chake cha jana licha ya kwamba hata mimi najuwa fika yeye ni mganga njaa tu.

Nakumbuka ulianzisha thread ku complain kwamba kuna watu wanaingiza mambo ya dini na kukashifu ili kuvuruga thread,kuna mod alikujibu hata wewe uwe makini!ndugu yangu una tatizo gan na waislamu?una uhakika hawajaiona wakat ipo u tube?you should walk on your talk bro.
 
kitu kinachonikera jf ni baadhi ya watu kudhani ni lazima kuanzisha uzi kana kwamba usipoanzisha utapigwa ban..acheni kuanzisha nyuzi zisizokuwa na utafiti,mnaipunguzia heshima jf..kuweni wasomaji wa threads za watu kama sisi kwa sababu hatuna habari ya kuandika zaidi ya kuchangia..ebo!!!!
 
Naomba tumtendee haki Mchungaji Lusekelo, nimeangalia kile kipindi tangu mwanzo mpaka mwisho. Mbali na kuongelea mvua za elnino ambazo ameziongelea mwisho wa kipindi, yeye alitumia muda wake mwingi kuwaasa watawala wanaotumia vyombo vya dola kuua raia wasio na hatia. Pia amesema jambo hilo la mauaji kwenye mikutano ya siasa kama watawala wanalitumia ili kuwatisha wananchi basi mbinu hiyo haijafanikiwa na badala yake wanawajengea usugu watanzania. Ametolea mfano wa Maandamano ya wana habari na kufukuzwa kwa waziri mwenye dhamana na jeshi la polisi, pia ameongelea umati wa watu uliohudhuria mapokezi ya viongozi wa BAVICHA Morogoro kwamba pamoja na mauaji haya yanayofanywa na vyombo vya dola bado wananchi hawaogopi kukusanyika na wanakuwa sugu zaidi.

Akasema viongozi wa sasa wanakidhalilisha CCM na kusahau kuwa ni CHAMA kilichoasisi UKOMBOZI wa bara la Afrika na kuwataka viongozi hao waende na wakati kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yanayoendelea duniani na wasiwe na FIKRA mgando za kukandamiza mabadiliko haya na wakubali ukweli juu ya uwepo wa DEMOKRASIA nchini na duniani. Aliwataka pia watawala kuwa wabunifu ili kuendeleza mipango ya maendeleo ya nchi na wananchi wake badala ya kuwa wauaji.
kwaio chanel 10 amelipia siasa au injili?? we mchungaji gani na balzamen tu wa mbagala uyu hana lolote bendela fata upepo
 
kweli nimeamini sasa kua JF ni jukwaa la umbea,kwa yeyote aliangalia kipindi ataungana na mimi kua muanzisha mada hakuelewa hata kilichosemwa na sijui kaja na mtazamo huu kutoka wapi,inakera inaudhi sana kuwadanganya watu na watu hao pasipo kuutafuta ukweli kuchangia kitu wasichokijua wala haki exist na kujisifu kua ni great thinkers,nathubutu kuwaita wajinga,Yes waliochangia kusuport hii mada ni wajinga

Mtoa mada alikuja akiwa amelewa kwahiyo hakuangalia kipindi chote. ni mvurugaji wa mijadala hapa jukwaani, kwani alichosema sicho alichosema Lusekelo. Lusekelo ameiponda sana serikali juu ya mauaji ya Mwangosi na wengine na kuiasa kuwa mauaji hayo yanawapa usugu watanzania hivyo kuzidi kuwafanya wasiogope mikusanyiko. Pia amewaponda watawala kwa kukidhalilisha chama cha mapinduzi ambacho kimepata sifa ya kusimamia ukombozi wa Africa. Na hii ni kweli tupu, kwamba Tanzania imesimamia ukombozi wa nchi nyingi za africa chini ya ccm/tanu, ukweli huu haupingiki. Mimi sina chama chochote cha siasa lakini napenda sana kuwe na mabadiliko nchini kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa.
 
word!!!
Naomba tumtendee haki Mchungaji Lusekelo, nimeangalia kile kipindi tangu mwanzo mpaka mwisho. Mbali na kuongelea mvua za elnino ambazo ameziongelea mwisho wa kipindi, yeye alitumia muda wake mwingi kuwaasa watawala wanaotumia vyombo vya dola kuua raia wasio na hatia. Pia amesema jambo hilo la mauaji kwenye mikutano ya siasa kama watawala wanalitumia ili kuwatisha wananchi basi mbinu hiyo haijafanikiwa na badala yake wanawajengea usugu watanzania. Ametolea mfano wa Maandamano ya wana habari na kufukuzwa kwa waziri mwenye dhamana na jeshi la polisi, pia ameongelea umati wa watu uliohudhuria mapokezi ya viongozi wa BAVICHA Morogoro kwamba pamoja na mauaji haya yanayofanywa na vyombo vya dola bado wananchi hawaogopi kukusanyika na wanakuwa sugu zaidi.

Akasema viongozi wa sasa wanakidhalilisha CCM na kusahau kuwa ni CHAMA kilichoasisi UKOMBOZI wa bara la Afrika na kuwataka viongozi hao waende na wakati kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yanayoendelea duniani na wasiwe na FIKRA mgando za kukandamiza mabadiliko haya na wakubali ukweli juu ya uwepo wa DEMOKRASIA nchini na duniani. Aliwataka pia watawala kuwa wabunifu ili kuendeleza mipango ya maendeleo ya nchi na wananchi wake badala ya kuwa wauaji.
 
Anthony Isyu lya kyala likutobile, wandile kangi ni syasya sya sisiemu kangi! Po sikukutoba wakukaya. Bhangogile UNDAVITI UWAMWANGOSI ukapilika? Sili bule bule kangi?

Nkamu gwangu Havizya LE GAGNANT ntungulu fijo, Umwanitu uju Athony Lusekelo ajovile fijo, asulumenye fijo ifwa ja Ndaviti Umwangosi, atile aligwa kukaja fijoooooooooooooo
 
Naomba tumtendee haki Mchungaji Lusekelo, nimeangalia kile kipindi tangu mwanzo mpaka mwisho. Mbali na kuongelea mvua za elnino ambazo ameziongelea mwisho wa kipindi, yeye alitumia muda wake mwingi kuwaasa watawala wanaotumia vyombo vya dola kuua raia wasio na hatia. Pia amesema jambo hilo la mauaji kwenye mikutano ya siasa kama watawala wanalitumia ili kuwatisha wananchi basi mbinu hiyo haijafanikiwa na badala yake wanawajengea usugu watanzania. Ametolea mfano wa Maandamano ya wana habari na kufukuzwa kwa waziri mwenye dhamana na jeshi la polisi, pia ameongelea umati wa watu uliohudhuria mapokezi ya viongozi wa BAVICHA Morogoro kwamba pamoja na mauaji haya yanayofanywa na vyombo vya dola bado wananchi hawaogopi kukusanyika na wanakuwa sugu zaidi.

Akasema viongozi wa sasa wanakidhalilisha CCM na kusahau kuwa ni CHAMA kilichoasisi UKOMBOZI wa bara la Afrika na kuwataka viongozi hao waende na wakati kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yanayoendelea duniani na wasiwe na FIKRA mgando za kukandamiza mabadiliko haya na wakubali ukweli juu ya uwepo wa DEMOKRASIA nchini na duniani. Aliwataka pia watawala kuwa wabunifu ili kuendeleza mipango ya maendeleo ya nchi na wananchi wake badala ya kuwa wauaji.

Eliah G Kamwela says thanks for this very useful post.
 
Lusekelo mi napenda sana kuisikiliza mipasho yake.jamaa yuko juu na harembi wala nini.
 
Back
Top Bottom