Mbwembwe za mikutano ACT zimeishia wapi?

Mbwembwe za mikutano ACT zimeishia wapi?

copper wire

Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
12
Reaction score
4
kulikuwa matangazo mengi ya kuhusiana mikutano mikubwa (kutikisa) ya ACT kuanza tarehe 22 mwezi nane, sasa hautuon mrejesho au tarehe wamebadilisha? au kelele za chura mwalimu kaijage njoo utujulishe.
 
Kuna watu wapo nyuma ya pazia wanangojwa wajitokeze , hapo ndipo chama kitapata nguvu.
 
mpiga ngoma anahitaji wachezaji, huwezi kuendelea kupiga ngoma kama watu hawaichezi kabisa hiyo ngoma yako.

labda wamekosa wachezaji, tusubiri tuone.
 
Subirini Zitto apate fedha za mikutano toka kwa swahiba wetu CCM ndio mtaona moto wetu
 
Chama ambacho hata viongozi hakina kamwe hakiwezi kuwa na mafanikio yoyote yale na pia chama ambacho kimekubali kutumika na chama kilichopo madarakani ili kukisaliti chama kikubwa cha upinzani nchini pia kitakuwa kinasuasua tu na hatimaye kujifia tu. Tangu tuanze kuisikia ACT ni zaidi ya mwezi wa tatu sasa, lakini hadi hii leo chama hiki kimeshindwa kutangaza safu yake ya Viongozi wa juu wa chama hicho huku wakishindwa kutoa hata sababu ya hali hii imesababishwa na nini. Kuanzisha chama si lelemama.
 
Mkutano wao mkubwa saaana ulifanyika pale Singida.
 
Sasa ATC sijui wapo wangapi hapa JF nawaona ona utadhani wapo wengi kumbe kelele tuu.Yaani wao sera ni kuiponda Chadema badala ya kutafuta njia ya kuing'oa CCM washike dola.
 
Na maandamano ya UKAWA nchi nzima yameishia wapi? Make nasikia eti wanahaha kuonana na Rais ili wakanye Juis ya ikulu.

Hivi ile juisi huwa inachanganywa na matunda gani kiasi kwamba iwakoseshe usingizi wapinzani?? Tafadhali mwenye kujua na atujuze.
 
Chama ambacho hata viongozi hakina kamwe hakiwezi kuwa na mafanikio yoyote yale na pia chama ambacho kimekubali kutumika na chama kilichopo madarakani ili kukisaliti chama kikubwa cha upinzani nchini pia kitakuwa kinasuasua tu na hatimaye kujifia tu. Tangu tuanze kuisikia ACT ni zaidi ya mwezi wa tatu sasa, lakini hadi hii leo chama hiki kimeshindwa kutangaza safu yake ya Viongozi wa juu wa chama hicho huku wakishindwa kutoa hata sababu ya hali hii imesababishwa na nini. Kuanzisha chama si lelemama.

Unataka uongozi ACT?g
 
You are commenting in a wrong thread sir!
Tunaongelea ACT, sio UKAWA.

Si vibaya swali likaulizwa kwa swali. Huenda jibu la swali A laweza kuwa jibu la swali B vilevile.
 
Back
Top Bottom