Mbwana Samatta arudi tena Ubelgiji, aenda Royal Antwerp

Bon-CN

JF-Expert Member
Oct 14, 2020
1,338
2,753
Samatta.png


Kama ambavyo tweet inavyoonesha hapo juu, Mbwana Ali Samatta amerudi nchini Ubeligiji, na safari hii akijiunga na klabu kongwe nchini humo, yaani Royal Antwerp! Kwa wafuatiliaji, bila shaka wanafahamu Samatta hakuwa akipata nafasi ya kutosha pale Fenerbahce. Jambo lililonishangaza, inaonekana mashabiki wa Fenerbahce bado walikuwa na imani zaidi na Samatta, lakini Benchi laUfundi likamuona hatoshi!

Kwa mujibu wa Gazeti la Hurriyet la nchini Uturuki, Samatta ameenda Royal Antwerp kwa mkopo wa mwaka mmoja, huku kukiwa na kipengele cha kukiwa na option ya kumnunua kwa $4.72 Million, takribani Sh 11 Bilion za Tanzania.

Ukiangalia kwenye msimamo wa ligi ya Ubelgiji, Royal Antwerp haijafanya vizuri kwenye mechi zake 5 ilizocheza, na matokeo yake timu hiyo ipo nafasi ya 3 kutoka chini. Sio hivyo tu, ingawaje timu hii ina support kubwa sana kutokana na ukongwe wake, lakini mara ya mwisho timu hii kuchukua kombe "kuu" ni wakati mama yangu mzazi akiwa na umri wa mwaka mmoja, na sia ajabu wakati Mzee Samatta enzi hizo akiwa Shule ya Vidudu.

Pamoja na hayo, kwangu naona hii ni fursa kwa Samatta kuonesha uwezo wake. Akifanya yale aliyokuwa amefanya Genk, na Royal Antwerp kufanikiwa kuchukua ubingwa, basi mademu wote wa Antwerp watakuwa wake. Mwamba ataimbwa kila kona, hadi ManU ambao ni marafiki wakubwa wa Royal Antwerp watafahamu uwepo wa Mbongo huyo!!

Mafanikio makubwa ya Royal Antwerp ni wakati Mbwana Samatta akiwa na umri wa mwaka 1, ambapo mwaka huo, yaani 1993 Royal Antwerp walifanikiwa kufika Fainali ya UEFA Cup Winners' Cup, ambapo timu ya Parma kutoka Italia ndie alichukua ubingwa mbele ya Royal Antwerp.

Je, safari ya Samatta kurudi Bongo inakaribia?
 
Ningemshauri baada ya kumaliza kukipiga ajikite kwenye uwakala wa wachezaji,Kwa sababu ana connection na exposure ya kuishi ulaya na kulijuw soka la ulaya
Sure, na wala asitake mambo ya ukocha kama ilivyo kwa wengi manake ukocha ni full stress!! Na pamoja na kuwa na connection, pia pesa atakuwa nayo kwahiyo hatafanya uwakala wa njaa! Kama huna njaa unaweza kusimamia hata vijana wadogo kabisa from the grass-root.
 
Ugonjwa huja kwa kasi ila huondoka polepole, kwisha kunakaribia
 
Umri ushasogea, ila alichokifanya ni kikubwa kwa maisha yake na kwa soka la Tanzania, kila zama zina mwisho, akiwa na zali zuri anaweza kurudi tena au lah, anakusanya fedha za mwisho mwisho, uamuzi wa kukimbilia uingereza haukuwa mzuri saana kwake.
 
Sijui nani kamroga huyu dogo!!!?
ilipaswa a stick kwenye ligi ya Uingereza kama miaka 3 hv
Hakuna hata aliye mroga! Sema tu dogo tangu afunge ndoa na kwenda kuishi na mke wake majuu, amekua ni mchezaji wa kawaida sana!!

Inawezekana amewekeza zaidi kwenye familia, kuliko kujitengeneza yeye mwenyewe, ili awe fit na hatari zaidi kwa timu anazo kutana nazo uwanjani.

Yaani amekosa kabisa stamina ya kupangua mabeki kama zamani. Ukimkuta uwanjani, ni mtu kudokoa dokoa tu mpira na kutoa pasi fupi fupi na zisizo na faida yoyote ile kwa timu!
 
Hakuna hata aliye mroga! Sema tu dogo tangu afunge ndoa na kwenda kuishi na mke wake majuu, amekua ni mchezaji wa kawaida sana!!

Inawezekana amewekeza zaidi kwenye familia, kuliko kujitengeneza yeye mwenyewe, ili awe fit na hatari zaidi kwa timu anazo kutana nazo uwanjani.

Yaani amekosa kabisa stamina ya kupangua mabeki kama zamani. Ukimkuta uwanjani, ni mtu kudokoa dokoa tu mpira na kutoa pasi fupi fupi na zisizo na faida yoyote ile kwa timu!
Madhara ya kupiga bao 3 kila siku afu mtu anaenda zoezi.Wazungu wanaishi na wake zao lkn wao story za kupiga bao 3 hawanaga.1 la afya afu imeisha hio.
 
Samatta kinaweza kikamkuta kilichomkuta aliposajiliwa Aston Villa,


Samatta aliikuta Villa ikiwa kwenye matatizo hivyo asingeweza kubadili kitu chochote wakati timu yote ilikua imesha jichokea na iliponea kwenye tundu la Sindano tu kushuka daraja,

The same na huko anapokwenda sasa,

Antwerp ipo kwenye Down fall,Samatta atacheza under pressure na sio rahisi yeye kama yeye kuibeba team peke yake,

Good luck SAMATTA.
 
Sijui nani kamroga huyu dogo!!!?
ilipaswa a stick kwenye ligi ya Uingereza kama miaka 3 hv
EPL ngumu na uchezaji tofauti speed sana na sio kila mtu anaweza kucheza EPL kuna wengi tu wameshindwa pale na haiukufanyi kuwa mchezaji mbaya ila ukiona mchezaji wa nje hasa Africa kama kina Sadio, Mo au Toure ni lazima uwe na kitu cha ziada sana kukubaliwa hawa wanavipaji next level. Nadhani league ya Belgium itamfaa kwa style yake ya mpira ila kajitahidi sana kufanya aliyoyafanya hatuwezi kumbeza.
 
Kocha wa Fenerbahce alisema Samatta alikosa confidence, ila kama angejiamini ni mchezaji mzuri.
 
Zama zake naona ndio zinaishia, hv hata team ya taifa kaitwa kweli?
Ila bado anaweza kwenda nchi za kiarabu na akakiwasha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom