Mbunge yule Kijana aliyeniomba Ushauri...!

Mbunge yule Kijana aliyeniomba Ushauri...!

Thanks mkuu nimelipenda sana neno la leo, japo ni chungu lkn ntalimeza.
 
Sasa we ulitaka asiposhughulikia gari lake apande gari la mkwe wako? We Majid acha habar zako kwani nishakushusha hadhi tangu siku ile umewasaliti waandishi wenzako wa habar kwenye msiba wa mwangosi, We ni hatari na wa kuogopwa kama ukoma na 2015 ukishinda ubunge huko iringa kijijin mi ntatembea utupu nchi nzima.
 
maggid ni mtu wa hovyo sana. Yeye huwa hana mchango kwenye thread za wenzake. Akitoa thread huwa pumba mwanzo mwisho na huingia mitini moja kwa moja, njoo sasa maggid ujibu hoja
 
Last edited by a moderator:
Alichosema Maggid ni ukweli mtupu. Si mnamkumbuka yule mbunge ambaye kwenye ukurasa wake wa facebook kila wakati anaweka status ya jinsi anavyokula raha kwenye Landcruiser Amazon yake. Aliposhinda uchaguzi tu kitu cha kwanza kikawa kutafuta X5.

Sasa hivi wale vijana wa bodaboda waliompigia kampeni hataki tena kukaa nao. Amesahau kuwa hawa walimpigia kampeni kutokana na matumaini aliyowapa.

Mpaka sasa hajatekeleza ahadi hata moja anayoweza kujivunia...
 
Wacha woga kama kweli ulikerwa na huyo Mbunge wa upinzani kijana weka jina lake hapa na u-mention kwenye hii topic ili aje akubali ama akatae.
Unless other wise imekaa kiudaku sana hii coz wabunge vijana wa upinzani wanaongezeka kila kukicha so hatuwezi ishi kwa kuhisi ni nani....
Wacha kudhalilisha tasnia yenu bana.....too much blah blah.
 
Sasa we ulitaka asiposhughulikia gari lake apande gari la mkwe wako? We Majid acha habar zako kwani nishakushusha hadhi tangu siku ile umewasaliti waandishi wenzako wa habar kwenye msiba wa mwangosi, We ni hatari na wa kuogopwa kama ukoma na 2015 ukishinda ubunge huko iringa kijijin mi ntatembea utupu nchi nzima.

Mkuu Sharcode, hii mpya. Kumbe mdau anataka kuchukua jimbo mitaa ya kati???
 
Sasa tujifunze nini hapa?


Soma upya utajifunza kitu hapa. Ukiona hujajifunza baada ya kusoma mara ya pili, achana na huu uzi manake utakupoteza mazima!!!! Some issues are beyond your mental understanding, it take years to reach through experience and education.
 
siamini ninachokisoma, ni ww maggid ama kweli ukiyastaajabu ya mussa ya firauni utayashangaa
 
Wacha woga kama kweli ulikerwa na huyo Mbunge wa upinzani kijana weka jina lake hapa na u-mention kwenye hii topic ili aje akubali ama akatae.
Unless other wise imekaa kiudaku sana hii coz wabunge vijana wa upinzani wanaongezeka kila kukicha so hatuwezi ishi kwa kuhisi ni nani....
Wacha kudhalilisha tasnia yenu bana.....too much blah blah.
Mmchungaji Peter Msigwa wa Iringa mjini
 
hahahahaa PR manager wa kapteni Komba..hadithi yake inatufundisha Kepteeeeni aendeleee kulala...yeera, sponsored by magodoro dodoma:A S shade:

wala sio kamusi huyu no m...k ...kabisa silly
 
NENO LA LEO: MBUNGE YULE KIJANA ALIYENIOMBA USHAURI..!


a1_be7bd.jpg

Ndugu zangu,
Kuna simulizi ya kwenye Biblia. Enzi za Mfalme Suleiman kuna watu waliolalamika sana, kuwa wanaishi kwenye manyanyasiko mno.
Kukawa na vijana waliokuwa na kiu ya kutaka mabadiliko ya uongozi wa mfalme. Walitaka watawaliwe na mfalme kijana.

Wazee walipoombwa ushauri wakatamka; kuwa vijana mara nyingi hupungukiwa na busara. Hivyo, si lazima mfalme awe kijana.
Vijana wale wakakaidi ushauri wa wazee. Wakampata Mfalme kijana. Naye alipokuwa madarakani, alitenda mara mbili ya dhambi alizotenda mtawala aliyetangulia.

Mfano, kama mtawala aliyepita alitoa adhabu ya kuchapa kwa mjeledi, basi, mfalme kijana yeye alitaka atumie rungu. Hakukuwa na nafuu walioitarajia.
Ndugu zangu,

Juma la kwanza tu baada ya Bunge kuanza mwaka 2010, nikiwa njiani kutoka Singida nilisimama Dodoma. Hapo nilipata bahati ya kukutana na mmoja wa Wabunge vijana kutoka kambi ya upinzani.

Tulikaa na kunywa chai pamoja. Alinitaka pia ushauri katika kazi yake. Hakika,niliingiwa na matumaini makubwa juu ya fikra zake za kimaendeleo pale alipoanza mazungumzo. Mathalan, kati ya dhambi kadhaa zinazofanywa na wabunge alizoziona, akaniambia juu ya kustaajabishwa kwake na tabia ya Wabunge kufoji risiti za safari zao ili wapate fedha zaidi.

" Yaani kaka Maggid, sikujua kuwa Wabunge hawa wanafanya mambo kama watoto wa shule. Yaani Mbunge anahangaika kufoji risiti za mafuta na kudai kuwa ametokea mahali fulani kuja hapa Dodoma wakati sio!" Aliniambia kwa uchungu mbunge yule kijana.

Lakini, mashaka yakanijia pale nilipomwuliza;
" Sasa ukitoka hapa Dodoma umejiandaa na kipi cha kwenda kuwaambia wapiga kura wako kwenye mkutano wako wa kwanza wa hadhara baada ya kikao chako cha kwanza Bungeni?"

Mbunge yule kijana aliniangalia na kuniambia; " Naenda kwanza Dar kuhangaikia gari yangu mpya!"
Nikawa nimekatishwa tamaa na Mbunge yule kijana. Kwamba katika juma la kwanza tu la kukaa Bungeni, tayari ameanza kufikiria kuhangaikia masuala yake binafsi, na si masuala ya wananchi waliompigia kura!

Naambiwa, naye siku hizi anapomaliza vikao vya kuongea hata na jamaa zake tu, haraka sana hukimbilia kutoa ' bahasha za nauli'.
Siku hizi mbunge yule kijana ana gari zaidi ya ile aliyokwenda kuichukua Dar. Amekuwa mbunge-mfanyabiashara.

Sifikirii tena kwenda kumpa ushauri mbunge yule kijana, maana, naweza kuambulia kudhalilishwa kwa kupewa ‘bahasha ya nauli' ya kurudia nyumbani kwangu.

Naam, ni heri ya ndugu yangu John Komba, hata akisemwa kuwa anasinzia Bungeni, bado ana mchango kwa jamii; kwa nyimbo zake zenye kuburudisha na kuelimisha.

Ndio, nchi hii inahitaji mabadiliko ya kimsingi, lakini, ni vizuri kutambua, kuwa wengine tunaofikiri kuwa wanaweza kutusaidia katika kuyafikia mabadiliko hayo, hawana tofauti kabisa na baadhi ya tunaofikiria hawatufai.

Na hutokea, kuwa dhambi wafanyayo, na watakayoifanya, yumkini yaweza kuwa ni mara mbili ya inayofanywa na baadhi ya waliopo sasa.

Ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765

 
Mmchungaji Peter Msigwa wa Iringa mjini

Hakuna muhehe mnafiki....we ni mnafiki sana!!umejuaje kama ni Msigwa?tumeona kampuni yako ipo kwenye list ya yale yatakayokagua magari kwa niaba ya TBS....Jambo jema!ila wahehe hawawezi kukupa jimbo bwabwa kama wewe
 
Jimbo la msigwa linakuumiza kichwa sana kaka? rudi nyumbani uanze mipango mapema otherwise utaishia kupiga deal za hapa na pale tu nchi za watu


"fimbo ya mbali haiui nyoka"
 
Jamaa kwa kuandika pumba na unafiki ndio mwenyewe, eti naye ni mwandishi wa habari!!!


Mnafiki angekuwa nguo tungemtambua kwa rangi!

Kama kweli wewe una uchungu na nchi , acha unafiki na umtaje kabisa jina huyo Mbunge na chama chake ili wananchi tumtambue.
Wacha kumficha muovu.
 
Jimbo la msigwa linakuumiza kichwa sana kaka? rudi nyumbani uanze mipango mapema otherwise utaishia kupiga deal za hapa na pale tu nchi za watu


"fimbo ya mbali haiui nyoka"
Dalili ya mvua ni mawingu
 
badala ya wavuvi wa watu kama yesu alivyo mwambia petro wameamua kuasi na kuwa wavuvi wa vitu
 
Back
Top Bottom