Mbunge wa Tunduma (CHADEMA), Frank Mwakajoka amekamatwa na polisi ikielezwa kuwa atafikishwa mahakamani muda wowote kujibu tuhuma za kumpiga mtu mwaka 2018.
Akizungumza leo Alhamisi Julai 11, 2019 kamanda wa polisi Mkoa wa Songwe, George Kyando amesema mbunge huyo amekamatwa leo na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.
Amebainisha kuwa Mwakajoka anadaiwa kumpiga mwananchi ambaye hajamtaja jina, kwamba kesi hiyo ni ya muda mrefu
"Kuhusu jina la mtu aliyepigwa hapa sina labda unipe muda ili nilitafute,” amesema kamanda huyo.
Katibu wa Baraza la Vijana la CHADEMA(BAVICHA) Mkoa wa Songwe, Ayub Sikagonamo amedai Mwakajoka amekamatwa kwa madai ya kumpiga ofisa mtendaji wa mtaa, Deus Mwampashe.
Mbunge huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
Hahaha labda na Spika Ndugai atakamatwa siku moja kwa makosa kama haya, ngoja waweke precedent.
Rudisheni kumbukumbu zenu, hata kama uluwahi kupigwa ukiwa primary, unaweza shitaki sasa.
Lini Spika Ndungai atapandishwa kizimbani kwa kosa lake la kumpiga mwanaCCM mwenzake kwa rungu mnamo mwaka 2015???
Hahaha anasema siku hizi ni rafiki yake, wanapigiana simu na kutaniana. Bila shaka jamaa aliogopa kabisa siasa.Hivi yule jamaa aliyepigwa na spika alipona kweli maana alitandikwa bonge la fito
Jeshi la police linafutwaje?Baada ya Chadema kutwaa nchi 2020 kama wananchi wengi wanavyotarajia Jeshi la polisi litafutwa na baadhi ya viongozi wake watakamatwa .
Kuanza upya si ujinga
Kwa kutumia njia ile ile aliyoitumia nyerere kufuta jeshi la kikoloniJeshi la police linafutwaje?
Acha kuhamisha magoliLini Spika Ndungai atapandishwa kizimbani kwa kosa lake la kumpiga mwanaCCM mwenzake kwa rungu mnamo mwaka 2015???
Kweli aisee limepoteza misingi yake!.Jeshi la police linafutwaje?
hivi unajua maana ya jinai???Acha kuhamisha magoli
Huyo spika atakamatwa hata hakuna aluefungua kesi?