Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
Mlinzi wa Kampuni ya Kachipa aitwaye James Mtongori (28) Mkazi wa Katoro anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Geita kwa kumpiga risasi pajani, Kijana Kulwa Sylvester (26) Mkazi wa Katoro Tarafa ya Buseresele Mkoani Geita.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema kabla ya kujeruhiwa Kulwa alitaka kumkata kwa shoka Mlinzi huyo ndipo Mtuhumiwa alijihami kwa kumfyatulia risasi na kumjeruhi kwenye paja.
"Kabla ya kujeruhiwa alitaka kumdhuru Mtuhumiwa kwa kumkata na shoka ndipo Mtuhumiwa alijihami kwa kumfyatulia risasi na kumjeruhi, Mtuhumiwa amekamatwa kwa mahojiano na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma”
Aidha Kamanda Mwaibambe ametoa wito kwa Wananchi pamoja na Walinzi wa Kampuni mbalimbali kutojichukulia sheria mkononi “Kulwa anapatiwa matibabu katika Kituo cha Afya Katoro na anaendelea vizuri”
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema kabla ya kujeruhiwa Kulwa alitaka kumkata kwa shoka Mlinzi huyo ndipo Mtuhumiwa alijihami kwa kumfyatulia risasi na kumjeruhi kwenye paja.
"Kabla ya kujeruhiwa alitaka kumdhuru Mtuhumiwa kwa kumkata na shoka ndipo Mtuhumiwa alijihami kwa kumfyatulia risasi na kumjeruhi, Mtuhumiwa amekamatwa kwa mahojiano na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma”
Aidha Kamanda Mwaibambe ametoa wito kwa Wananchi pamoja na Walinzi wa Kampuni mbalimbali kutojichukulia sheria mkononi “Kulwa anapatiwa matibabu katika Kituo cha Afya Katoro na anaendelea vizuri”