Otorong'ong'o
JF-Expert Member
- Aug 17, 2011
- 37,448
- 25,591
Msitakae nchanganyikiwe.NAPE TOA TAMKO.pipoooooooooz...
Watasema ccm imekomaa kisiasa. Wako tayari kukubali majibu.
Msitakae nchanganyikiwe.NAPE TOA TAMKO.pipoooooooooz...
Sasa CDM tuanze kunyemelea jimbo la Pinda Mtoto aw mkulima. tumweke mgombea wa CDM ktk uchaguzi ujao. Pinda hana mshiko huko
Tulianza na Mungu, tunamaliza na Mungu.
Vigezo vya kupiga ban ni vipi?
Wakuu watueleze makosa ya mkuu wetu MOLEMO.
Wakuu leo ndiyo kunatolew hukumu ya kupinga matokeo ya ubunge wa sumbawanga mjini wa Aeshy Hilaly Halphany CCM dhidi ya mwalimu Norbet Joseph Yamsebo wa Chadema ambaye anadai kuchakachuliwa katika uchaguzi huo.
Madai miongoni ni pamoja na kutoa rushwa kwa makundi mbalimbali na watu wengi walijitokeza kutoa ushahidi huo na kukiri kuwa ni kweli walipokea vitu mbalimbali ikiwemo fedha, baskeli, pikipiki, vinywaji, kinanda kwa kanisa katoliki, nk kwa sharti la kumpigia kura mbaya zaidi ni kwa mkurugenzi mwanamama kutoa ushahidi wa kupinga ushindi wa mbunge huyo, mkurugenzi huyo alihamishwa muda mfupi mara baada ya matokeo ya uchaguzi kutolewa na kupelekwa wilaya ya Ileje.
Moja ya kituko katika kesi hii mara baada ya mbunge huyo kuulizwa kama anaamini na kusema hajui kama alishinda ila mkurugenzi ndiye anayejua ushindi huo, kimsingi ulinzi umeimalishwa kwani yaweza kuwa mbaya endapo Aeshy atatangazwa mshindi, askali wapo wa kutosha, washawasha na mabomu, lakini kesi hii ilikosa umaarufu kwa kuwa waandishi njaa wote walikuwa upande wa Aeshy mpaka ripota wa ITV Joshua joel update tutawaletea mara kesi itakapoanza....
Kamanda Doma.
UPDATES:
Umati umejitokeza kwa wingi sana na watu wamejaa ndani hivyo imebidi spika zifungwe nje lakini gari la polisi limekuwa likizunguka kuonya juu ya uvunjifu wowote wa amani.
Muda mfupi ujao jaji ataingia ila naona makamanda wengi sana kutoka sehemu mbalimbali wakiwa ndani ya magwanda
Jaji ameingia na kuanza kusoma kesi kwa lugha ya kiingereza na kesi nzima ina takribani kurasa 68
Mawakili wanaendelea kutoa utetezi wao wa mwisho lakini umati uliopo unatisha na Licha yakuonekana wafuasi wengi ni wa Chadema lakini Askari wameondolewa na kuashiria uwezekano wa chadema kushinda kesi.
Hoja za mwisho zinaweza kuwabana Magamba lakini naona Polisi wameanza kumwagika
UPDATES
mashabikina wafuasi wa Chadema wanashangilia nje ya mahakama kwa mbwembwe japo jaji bado hajatoa tamko
UPDATES
HATIMAYE CHADEMA WAIBUKA NA USHINDI NA UCHAGUZI KUTANGAZWA KURUDIWA UPYA BAADA YA BWANA AESHY KUKUTA NA KOSA LA KUTOA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI HUO. Chademaaaaaaaaaaaaaaaaa vemaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Hatimaye kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo la sumbawanga mjini imetolewa na kuonekana kuwa ushindi wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia ccm haukuwa huru na haki.Hii ni kutokana na ushahidi kuthibitisha pasi na shaka kuwa mgombea wa chama cha mapinduzi alitumia rushwa katika kushawishi wananchi kumpigia kura.Lakini pia kulikuwa na tetesi kuwa hata utangazaji wa matokeo uligubikwa na utata mkubwa na unaonekana uliingiliwa na watu wenye mamlaka za juu kitaifa. Mahakama ya hapa mjini imetoa maamuzi kuwa aeshy Hilary siyo mbuge halali na hivyo uchaguzi urudiwe upya. Je maamuzi haya yaweza kuwa ndio usahihi wa maamuzi ya mahakma zetu nchi tanzania?
kama mahakama imedhibitisha kuwa amepokea rushwa nitashangaa tena kama hatafunguliwa kesi nyingine ya kosa la kutoa rushwa. Pccb haihitaji kuumiza kichwa tena hapo, kwani ushahidi upo. Kazi ni kufungua tu file la kosa la rushwa.
kama mahakama imedhibitisha kuwa amepokea rushwa nitashangaa tena kama hatafunguliwa kesi nyingine ya kosa la kutoa rushwa. Pccb haihitaji kuumiza kichwa tena hapo, kwani ushahidi upo. Kazi ni kufungua tu file la kosa la rushwa.
binafsi ritz keshanisababishia ban tatu, ya mwisho ya miezi mitatu ndiyo imeisha juzi juzi...ritz and co wanafanya kamchezo ka ku provoke watu na uki retaliate kwa lugha kali kidogo ujue unapigwa dude.. nadhani wana mod/s wao ambaye yuko standby kwa shughuli hiyo...wacha watupige ban kwa sasa lakini ipo siku tutapata vyanzo vingine vya habari za kuaminika zaidi ya jf...!Sijajua vigezo lakini nasikia ni pale Ribosome alipolalamika eti Molemo kamuita FF