Wakuu! Je mwajua kuwa majengo haya ya TPDC ndiko pia alikokuwa akiishi mtoto wa mkuu wa kaya (JK) anayeitwa Miraji? Je mwajua pia kwamba hapo ndipo alipokuwa akiishi mke wa Director General wa TPDC?
Ninaoamba kumuuliza ndugu yetu Makupa; Je ni kwa nini hajasema lolote kwa hawa wapangaji wengine ambao nao wametimuliwa eneo hilo? Je ule utamaduni wa kupendeleana, kulindana na kuchimba wapinzani ndio uliosababisha hao wakubwa wengine wasijadiliwe na kuishia tu kumjadili Owenya? Je katika habari nzima na mjadala uliofuatia mbona hakuna habari kwamba kuna walionusurika kwa kulipa kodi mpya? Je ni nani na nani walioachwa kwa kupendelewa kwao?
Hili ni jukwaa la Great thinkers! Ni vizuri mtu anapoleta hoja humu ndani asiache nafasi yoyote ya kuonyesha ubaguzi, kuchimbana, kulindana, kupendeleana na kuogopana.
Hata hivyo tuwatetee wapangaji kutokana na ukweli kwamba walipandishiwa kodi ya pango kutoka TSH400,000 hadi 1,600,000 bila kufanyika kwa mazungumzo yoyote na wapangaji na baada ya wapangaji kugoma kulipa kodi mpya ndipo ikaamuliwa watimuliwe kibabe siku ya jumapili ambapo haiwezekani hata kwenda mahakamani kuweka pinjgamizi.
"mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni"