Mbunge Mkono kwa heri jimboni

Mbunge Mkono kwa heri jimboni

Pwaaaa

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2013
Posts
248
Reaction score
67
Kuna kila dalili zinazoonesha wazi kwamba wananchi wa Jimbo la Musoma vijijini (kwa sasa Jimbo la Butiama)hawatamchagua tena Mbunge wao, Nimrod Mkono. Kisa wananchi wanalalamika kawatelekeza kuboresha huduma muhimu za kijamii ikiwemo sekta ya maji na afya kwa akina mama.

Anayetajwa zaidi kwa sasa kumrithi Mkono ni Yusuph Kazi wa CHADEMA. Yetu macho na masikio, lakini waliopo huko Musoma wanaweza kutujuza kwa usahihi zaidi katika hili.
 
Kwani huyo Yusuph Kazi ana uwezo gani wa kushindana na Mkono?
 
Kazi atafanyiwa kazi asipokuwa makini. Azingatie masharti ya kisheria katika uchaguzi
 
Huyo yusufu kazi anafanya biashara isiyo halali kwanini awe kiongozi wa umma.
 
Pamoja na kutokuwa shabiki wa CCM - lakini Mkono hanyang'anyiki jimbo. Labda aamue kuachia.
 
huyu jamaa wa chadema atachukua maana mkono mwenyewe kachoka yule.
 
we hujui mbowe na mkono ni maswahiba, Uchaguzi uliopita Mbowe alihongwa milioni 20 na Mkono akapiga marufuku Chadema kusimamisha mgombea.
 
Jamaa wa escrow ndio wamesema katiba ni nzuri sana, walisema wakitokea kwao bukoba
 
Kati wabunge wa CCM ambao hawatasumbuka kupiga Kampeni ni Pamoja na mkono, CHADEMA mnapoteza muda bure
 
Mkuuu nahisi uko loliondo huijui vizuri hiyo sehemu yaani huyu jamaa ni mungu wao huko ukiacha mungu wa mbinguni...azawaisi unachosema ni sawa na

tff kuifuta timuya yanga kwenye ligi untarajia nini??
 
Mkono atakuwa kwenye wakati mgumu uchaguzi ujao kama atagombea tena. Itakuwa sio kati ya Mkono na wapinzani bali na Escrow pia. Mafisadi wenzake watamwaga pesa kuhakikisha anaumbuka kama alivyochangia kuwaumbua.

And too bad for him, ana mtu sasa hivi wakumsaidi kununua mgombea wa upinzani.
 
Butiama ni Mkono, na Mkono ni Butiama.

Kwa mwaka huu ambao huwa wanamsidia kushinda, waruri , wakwaya na Wajita wanamsubili kwa hamu wampige chini, wanadai anawabagua kimaendeleo kwa kupelekwa huko zanaki kila miradi na kuwaacha wao soremba. Kama atagombea malingo mengi Muhongo ,Mkono atapigwa chini asubuhi sana na kuku hatawika.
 
mkono ana pesaa atahonga wananchi!!!

kwanini asiwahonge huduma za maji na afya ? wakati mh selasini anamvaa Mramba ujinga kama huu ulitumika , mkono atang' olewa kiurahisi kuliko unavyodhani .
 
Kati wabunge wa CCM ambao hawatasumbuka kupiga Kampeni ni Pamoja na mkono, CHADEMA mnapoteza muda bure

yeyote atakayegombea ubunge nje ya UKAWA ataaibika vibaya sana ! wananchi wameamua kuikataa ccm na makandokando yake , hatutajali suti wala tarabushi ya mtu , huyu ni mmoja wa mafisadi walioiletea umasikini mkubwa nchi hii na nakuahidi kwamba mimi ni mmoja wa watakaojitolea hela za kuwezesha mchakato wa kumng'olea mbali ! nchi hii bila mafisadi inawezekana .
 
Mkono hang'oki ngo! Atahonga wanabutiama wote, na atashinda kwa kishindo, maana ni mafisadi walewale!
 
Back
Top Bottom