Mbunge Lijualikali bado ni muhalifu

Mbunge Lijualikali bado ni muhalifu

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,931
Reaction score
7,829
Kwa wapenda haki kuachiwa mbunge lijuakali na jaji munisi kwa msingi eti hati ya mashitaka ilikosewa kujazwa ni kutoitendea fani ya sheria haki.

Lijuakali alikutwa na makosa (was found guilty) kwa makosa aliyoshitakiwa nayo kwa hivyo mahakama ya juu kumuachia kwa kasoro ya kujazwa fomu ya mashitaka inaonyesha uzembe au kukosa uwajibikaji kwa jaji. ingekua sahihi jaji kuelekeza mashtaka yafunguliwe upya kuliko kumuachia mhalifu.

Wapo wanasheria kama lisu nihodari wa kuwatoa wahalifu lupango kwa makosa ya kiufundi (technical faults). wanaweza kumtoa mhalifu gerezani kwa kosa la kiufundi lisilo na uzito ukichukulia wanasheria wengi kua na kawaida ya kuuza haki. ukizingatia hayo utaona idadi ya wahalifu kuachiwa kwa sababu za kiufundi huku tayari wakiwa wameonekana na makosa yaweza kuongeza huko tunakoelekea.

Kwa wapenda haki mbunge Lijuakali bado ni muhalifu kwa sababu rufani yake haikumuona hana kosa alilokua amekatiwa hukumu ya kifungo na mahakama ya chini.
 
Una haki ya kwenda kumfungulia kesi ,nakushauri fanya hivyo ili sheria ifuate mkondo wake. Huku ukiandika sisi hatuna msaada wowote kwako kwa sababu naamini hata huyo jaji hayupo hapa kuweza kusoma hizo habari zako.
 
Kwa wapenda haki kuachiwa mbunge Lijuakali na jaji Munisi kwa msingi eti hati ya mashitaka ilikosewa kujazwa ni kutoitendea fani ya sheria haki. Lijuakali alikutwa na makosa (was found guilty) kwa makosa aliyoshitakiwa nayo kwa hivyo mahakama ya juu kumuachia kwa kasoro ya kujazwa fomu ya mashitaka inaonesha uzembe au kukosa uwajibikaji kwa jaji.

Ingekuwa sahihi jaji kuelekeza mashtaka yafunguliwe upya kuliko kumuachia mhalifu. wapo wanasheria kama Lissu ni hodari wa kuwatoa wahalifu lupango kwa makosa ya kiufundi.

Ukichukulia wanasheria wengi kuwa na kawaida ya kuuza haki idadi ya wahalifu kuachiwa kwa sababu za kiufundi huku tayari wakiwa wameonekana na makosa yaweza kuongeza huko tunakoelekea.

Kwa wapenda haki mbunge Lijuakali bado ni muhalifu kwa sababu rufani yaka haikumuona hana kosa aliloshitakiwa nalo.
Wewe hujapendezewa lijuakali kutoka na ndio tatizo lako lakin hujui sheri hata kidogo ila amin kuwa kosa dogo la kisheria laweza kuachia huru hata mtihumiwa wa mauaji ,sheria haifanyi kazi kwa hisia kama unavyo dhani
 
Ujinga sio sifa ulichoandika ni upumbavu hoja za Kukata Rufaa zilikuwa zaidi ya moja sababu za kiufundi ziliwalazimisha Majaji kutojadili hoja zingine
 
" ...Tatizo la Watanzania wengi ni ule ushupavu wa kuona wanajua na wanaweza kujadili kila kitu..."

IGP Omari Mahita
 
Mleta mada unajuwa vizuri kesi ya kutengenezwa iliyompereka Lijualikali gerezani, na pengine ungefurahi aendelee kusota jela!! Lakini nikuhakikishie maendeleo ya Tz hayataletwa na chuki dhidi ya wapinzani wa CCM, wala kuwalazimisha majaji kuipendelea CCM hakutaleta maendeleo tunayoyataka.

Pia ujue mambo ya kisheria ni very technical kosa lako anguko lako. Mwache Lijualikali awatumikie watu wake kama hujaridhika kata rufaa
 
Mtoa post akili zake zipo sawa na Mwenyekiti Sizonje ambae kiingereza kilimshinda alipokutana na waziri wa Ethiopia ilibidi atumie Kiswahili baada ya kuelemewa na msamiati wa malkia
 
Ni bora kumuacha mhalifu akiwa huru kuliko kumfunga mtu asiye na kosa....
 
Fake news. Wajinga day.
Lijuakali anapeta tuu
 
Kaa ukijua kuwa huyu ni mwansiasa na mmbunge, sababu ya kutoka lema ndo hiyo hiyo iliyotumika hapo, huyo munis ametumika kama daraja tu, na hiyo sababu aliyoitoa ni technical lakini haihusiki kabisa, kuna sababu kubwa ambayo hamuwezi ambiwa.
 
Hapo tuwe makini....maana nimesikia toka kwa mwanasheria mmoja kuwa inawezekana kushitakiwa tena! Sijaelewa itakuwaje
 
Back
Top Bottom