Mbunge kuwalipa mishahara waganga wa zahanati mbili

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
MBUNGE wa Ludewa mkoani Iringa, Deo Filikunjombe amejitolea kuwalipa mishahara waganga wa zahanati mbili za Kilondo na Lifuma jimboni humo ili kusogeza huduma ya afya kwa wananchi wa maeneo hayo. Ahadi hiyo imekuja siku chache baada ya Mbunge huyo kutumia Sh milioni 90 alizokopeshwa kwa ajili ya kununua gari la ubunge, kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake jimbo humo. Kwa kupitia fedha hizo, Filikunjombe aliyesema hahitaji gari jipya katika kipindi hiki ambacho wananchi wake wanasumbuliwa na kero nyingi; hivyo alinunua gari la wagonjwa lenye vifaa vya kisasa, trekta kubwa la kulimia, mabati, saruji na vifaa mbalimbali vya michezo na kuwakabidhi wananchi wake hivi karibuni.

“Juhudi zote za Halmashauri yetu ya Wilaya ya Ludewa za kumpata mganga kwa ajili ya Zahanati ya Kilondo zilishindikana. Safari hii nilipokwenda kuwatembelea nimewatafutia mganga,” alisema Filikunjombe. Alisema ametafuta mganga kwa ajili ya Zahanati ya Lifuma ambao kwa pamoja na yule wa Kilondo, atabeba mzigo wa kuwalipa mshahara mpaka pale Halmashauri itakapobeba jukumu hilo. Alisema watumishi wa afya wamekuwa wakikataa kwenda kufanya kazi katika maeneo hayo kwa kisingizio cha mazingira magumu na kwamba katika kipindi chake chote atakachokuwa mbunge wa jimbo hilo, hatakuwa tayari kuona watu wake wakifa kwa kisingizio hicho.

“Nipo tayari kuwalipa mishahara mizuri ili mradi watu wangu wafikiwe na huduma stahiki za afya kama ilivyo kwa watu katika maeneo mengine,” alisema. Alisema anayafanya hayo yote huku akiamini kwamba muda wa wanasiasa kuendelea kulumbana umekwisha, na wanachotakiwa kufanya ni kutekeleza ahadi walizowaahidi wananchi wao. Alivitaja vipaumbele vyake vikuu katika kipindi cha miaka mitano ya ubunge wake kuwa ni kuhakikisha barabara ya Ludewa - Njombe inajengwa kwa kiwango cha lami na miradi ya makaa ya mawe na chuma cha Liganga inaanza kufanya kazi.

Source" Habari Leo
 
Atawalipia mpaka lini?ni jukumu la serikali yake ya ccm kuajiri na kulipa madaktari.yeye akiwa bungeni kazi yake kushukuru tuu kumbe anatambua hakuna lolote serikali inalifanya ktk maendeleo
 
Zingekuwa zahanati saba ingekuwaje na kwa muda wa miaka mingapi then serikali ichukuwe jukumu lake?. Sidhani kama ni suluhisho. Hayo ndo madhara ya ndiyooooo! ipiteeeeeee!. na kupiga meza kama hamnazo kichwani!!
 
Atafanya hivyo kwa mangapi maana shida za watanzania sio hizo tu elimu affya maji na mengine atatoa pesa mfukaoni mwake? anazo za kutosha? Aaache huo unafiki aisukume serikali ifanye maana ni wajibu wake.
 
Halo hivyo vijiji havikaliki na serikali ameisahau wilaya ya Ludewa kabisa, Hongera Mbunge kwa kuanza ili serikali isome mfano wako
 
MBUNGE wa Ludewa mkoani Iringa, Deo Filikunjombe amejitolea kuwalipa mishahara waganga wa zahanati mbili za Kilondo na Lifuma jimboni humo ili kusogeza huduma ya afya kwa wananchi wa maeneo hayo. Ahadi hiyo imekuja siku chache baada ya Mbunge huyo kutumia Sh milioni 90 alizokopeshwa kwa ajili ya kununua gari la ubunge, kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake jimbo humo. Kwa kupitia fedha hizo, Filikunjombe aliyesema hahitaji gari jipya katika kipindi hiki ambacho wananchi wake wanasumbuliwa na kero nyingi; hivyo alinunua gari la wagonjwa lenye vifaa vya kisasa, trekta kubwa la kulimia, mabati, saruji na vifaa mbalimbali vya michezo na kuwakabidhi wananchi wake hivi karibuni.

“Juhudi zote za Halmashauri yetu ya Wilaya ya Ludewa za kumpata mganga kwa ajili ya Zahanati ya Kilondo zilishindikana. Safari hii nilipokwenda kuwatembelea nimewatafutia mganga,” alisema Filikunjombe. Alisema ametafuta mganga kwa ajili ya Zahanati ya Lifuma ambao kwa pamoja na yule wa Kilondo, atabeba mzigo wa kuwalipa mshahara mpaka pale Halmashauri itakapobeba jukumu hilo. Alisema watumishi wa afya wamekuwa wakikataa kwenda kufanya kazi katika maeneo hayo kwa kisingizio cha mazingira magumu na kwamba katika kipindi chake chote atakachokuwa mbunge wa jimbo hilo, hatakuwa tayari kuona watu wake wakifa kwa kisingizio hicho.

“Nipo tayari kuwalipa mishahara mizuri ili mradi watu wangu wafikiwe na huduma stahiki za afya kama ilivyo kwa watu katika maeneo mengine,” alisema. Alisema anayafanya hayo yote huku akiamini kwamba muda wa wanasiasa kuendelea kulumbana umekwisha, na wanachotakiwa kufanya ni kutekeleza ahadi walizowaahidi wananchi wao. Alivitaja vipaumbele vyake vikuu katika kipindi cha miaka mitano ya ubunge wake kuwa ni kuhakikisha barabara ya Ludewa - Njombe inajengwa kwa kiwango cha lami na miradi ya makaa ya mawe na chuma cha Liganga inaanza kufanya kazi.

Source" Habari Leo
Laaa hii ndio Tanzania tunayoijenga. hakika nchi ipo ktk autopilot, inajiendesha yenyewe! Yaani haya niloyasoma kama ni kweli basi tumefikia hali mbaya kupita kiasi na pengine hatuna haja ya kuwa na serikali...
 
Halo hivyo vijiji havikaliki na serikali ameisahau wilaya ya Ludewa kabisa, Hongera Mbunge kwa kuanza ili serikali isome mfano wako
mie nimebahatika kufika kwenye hivi vijiji vinavyotajwa hapo juu, kilondo na lifuma, kilichopo ni kwamba vile vijiji vipo pembezoni mno mwa wilaya na mazingira yake ni magumu sana. Hivyo, kila mtumishi wa serikali anayepangwa huko amekuwa akikataa kwenda. Watu wa Kilondo wamekuwa wanakufa hata kwa mafua tu. Zahanati ipo. Dawa zipo waganga hakuna. Hili alilolifanya Filikunjombe ni jambo jema kwani hapa ni swala la kuokoa maisha na uhai wa wananchi wake. Ushauri wangu kwa mhe. Filikunjombe, asiishie kuwatafuta hao waganga na kuwalipa mishahara, la hasha, Mhe. Filikunjombe, atengeneze mfumo mzuri utakaotatua tatizo hilo moja kwa moja. Leo, mhe. Filikunjombe akifa itakuwaje? It's a good start, but we need a permanent solution for that.
 
Laaa hii ndio Tanzania tunayoijenga. hakika nchi ipo ktk autopilot, inajiendesha yenyewe! Yaani haya niloyasoma kama ni kweli basi tumefikia hali mbaya kupita kiasi na pengine hatuna haja ya kuwa na serikali...
kwani kuna serikali tanzania?
 
Hongera Deo, ni viongozi wachache wenye moyo wa kukumbuka wapiga kura wao, usiishie hapo anza kutafuta wafadhali kwani najua Deo unafahamiana na watu mbalimbali pia una marafiki ambao wanaweza kukusuport kuifikisha Njombe katika maendeleo ya kweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom