Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Mkuu tatizo hapa ni kuomba apewe hicho kibali hapo wakati anachangia. Wabunge wanawawakilisha wananchi sasa akiensa kujiombea tena inakuwaje? Wenzake ambao wako katika biashara hiyo lakini si wabunge wana fursa ya kufika hapo na kumkomalia ama kumkumbusha juu ya maombi yao? Angeishia tu ku declare kwamba naye ni mdau katika hiyo biashara basi.Lakini Pindi Chana hawajavunja sheria yoyote wala kukiuka maadili ya kazi yake kama mbunge. Zamani sana tulikuwa na maadili ya viongozi, wenzetu wanaita "leadership code of conduct" au "leadership ethics." leo hii hakuna kitu cha namna hiyo, kwa hivyo Pindi ana haki ya kuuliza swali hilo bila wasiwasi wowote.