Mbunge ashauri bei ya VIP SGR ipunguzwe

Mbunge ashauri bei ya VIP SGR ipunguzwe

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,408
Reaction score
14,554
Mbunge wa Kyerwa, Innocent Bilakwate ameiomba Serikali ipunguze nauli ya daraja la VIP katika treni ya kisasa (SGR) kutoka TSh 150,000 hadi TSh 70,000 ili kuongeza mapato.

Amesema bei ya juu inachangia idadi ndogo ya abiria, akitoa mfano wa behewa linalobeba abiria 40 wakati mwingine husafiri likiwa na abiria 10 hadi 20.

Ametoa ushauri huo leo, Jumatatu Aprili 14, 2025, wakati akichangia hoja bungeni jijini Dodoma.

 
70000 × 40 = 2,800,000/=
150000 × 20 = 3,000,000/=

Mbunge ana hoja ya kipumbavu. Pia kulingana na muda watu wataendelea kuongezeka huko V.I.P. Mtu anayeweza kulipa 150k lazima atakuwa na ustaarabu hivyo kuzuia uharibifu wowote.
 
70000 × 40 = 2,800,000/=
150000 × 20 = 3,000,000/=

Mbunge ana hoja ya kipumbavu. Pia kulingana na muda watu wataendelea kuongezeka huko V.I.P. Mtu anayeweza kulipa 150k lazima atakuwa na ustaarabu hivyo kuzuia uharibifu wowote.
matusi ya nini sasa? Fanya VIP Tsh 80,000 basi!
 
matusi ya nini sasa? Fanya VIP Tsh 80,000 basi!
anatumia mihemuko kujibu hajui biashara yenye mzunguko mkubwa wa pesa ndiyo ina faida unaweza kuweka nauli kubwa na ukapata abiria wachache ni bora upate abiria 100 wenye value ya 1M kuliko abilia watano 5 wenye value ya 1M kiuchumi hiyo ni hasara maana kutembeza train yenye abiria 200 badala ya 2000 ni uzwazwa
 
Back
Top Bottom