Mbunge adai watoto 15 kati ya 45 darasani hawafundishiki

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mbunge Neema Lugangira amesema suala la Lishe Shuleni linapaswa kupewa uzito na kwamba hali ya Udumavu inachangia watoto kutofaulu na kufundishika kwa kiasi kikubwa watoto.

Akiwa Bungeni amesema, "Wataalamu wa Lishe kutoka TAMISEMI wanatuambia kwamba katika kila Darasa la Watoto 45, Kumi na Tano hawafundishiki".

Ameongeza kuwa pamoja na jitihada zote, ikiwa bado suala la lishe Shuleni litawekwa pembeni malengo ya Serikali kuhakikisha Elimu inanufaisha Watoto yatafifishwa.

1620131901379.png

 
Back
Top Bottom