Mbunge Abood atunukiwa Shahada ya Udaktari (PhD)

Mbunge Abood atunukiwa Shahada ya Udaktari (PhD)

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,096
Mhe Abdulaziz M. Abood, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udakitari kwa kutambua mchango wake katika uongozi na kuisaidia jamii.

Kuanzia sasa atafahamika kwa jina la Dkt. Abdulaziz M. Abood.

Mchango wa Dkt. Abood kwa wananchi wa Morogoro hauna mashaka hata kidogo na amekuwa akijidhihirisha hivyo kupitia kazi zake kama Mbunge na misaada binafsi ambayo amekuwa akiitoa kwa wananchi wake.

Hongera sana Dkt. Abood. Unastahili!

------

TAARIFA ZAIDI

Ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini na mfanyabiashara maarufu wa usafirishaji nchini Abdulaziz Abood ambaye ametunukiwa Udaktari wa Heshima na taasisi ya Academy of University Global Peace ya nchini Marekani.

Kwahiyo rasmi ukitaka kumuita kuanzia leo usimwite Abood, ni sharti uanze na Mheshimiwa Dkt Abdulaziz Abood ukimaanisha kutambua heshima aliyotunukiwa kutokana na uongozi thabiti katika mambo mbalimbali ya kijamii.

Sherehe za kumtunuku Dkt Abood udaktari huo zimefanyika jijini Dar es Salaam ambapo watanzania wengine kadhaa wamepewa heshima hiyo.

Dkt Abood ni mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini kwa takribani vipindi vitatu na amekuwa na mafanikio mengi katika nyanja mbalimbali kwa wananchi wa jimbo lake.
IMG-20230128-WA0032.jpg
 
Sasa zinagawiwa kama njugu, tutegemee thamani yake (Doctorate) kushuku since..Since scarcity ya kitu ndio inakipa thamani.
Eg, huwezi kua pisikali wa thamani wakati hata kwa bia 2 wanakupata🙊🚶🚶

Zinatoka mara moja tu kwa mwaka baada ya tathmini kufanyika. Na ukifuatilia, wote wanaopewa wanastahili.

Mfano siku moja akipewa msanii Diamond Platnumz utaona hastahili?

Binafsi naona ni jambo jema kuwatambua watu wanaofanya mambo makubwa kwenye jamii na kuwapa heshima.
 
Zinatoka mara moja tu kwa mwaka baada ya tathmini kufanyika. Na ukifuatilia, wote wanaopewa wanastahili.

Mfano siku moja akipewa msanii Diamond Platnumz utaona hastahili?

Binafsi naona ni jambo jema kuwatambua watu wanaofanya mambo makubwa kwenye jamii na kuwapa heshima.
Abood kafanya jambo gani kubwa mkuu?
 
Wakazi wa Moro huwaambii kitu kwa Abood wao kisa anawapa bus wakiwa na misiba [emoji3]
Hili ni mojawapo. Yapo mengi.

Jamaa anasomesha, anasaidia matibabu, anashiriki kwenye miradi mingi hata kwa kutumia pesa zake mfano ujenzi wa soko kuu la wajasiriamali.

Ni vile sio mtu wa kujionesha sana ndio maana hamuyajui haya.

Sent from my SM-E135F using JamiiForums mobile app
 
Mhe Abdulaziz M. Abood, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udakitari (Ph.D) na Chuo Kikuu The American University USA cha nchini Marekani kwa kutambua mchango wake katika uongozi na kuisaidia jamii.

Kuanzia sasa atafahamika kwa jina la Dkt. Abdulaziz M. Abood.

Mchango wa Dkt. Abood kwa wananchi wa Morogoro hauna mashaka hata kidogo na amekuwa akijidhihirisha hivyo kupitia kazi zake kama Mbunge na misaada binafsi ambayo amekuwa akiitoa kwa wananchi wake.

Hongera sana Dkt. Abood. Unastahili! View attachment 2497939

Sent from my SM-E135F using JamiiForums mobile app
Kwanini wasifanye mpango wakawatunuku wabunge wote tu kwa ujumla, kwa kutambua mchango wao mkubwa katika kutuletea maendeleo? Ili pia badala tu ya kuitwa waheshimiwa, kila Mbunge sasa awe anaitwa "Mheshimiwa Dokta..."
Au nakosea ndugu zangu?
 
Mhe Abdulaziz M. Abood, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udakitari (Ph.D) na Chuo Kikuu The American University USA cha nchini Marekani kwa kutambua mchango wake katika uongozi na kuisaidia jamii.

Kuanzia sasa atafahamika kwa jina la Dkt. Abdulaziz M. Abood.

Mchango wa Dkt. Abood kwa wananchi wa Morogoro hauna mashaka hata kidogo na amekuwa akijidhihirisha hivyo kupitia kazi zake kama Mbunge na misaada binafsi ambayo amekuwa akiitoa kwa wananchi wake.

Hongera sana Dkt. Abood. Unastahili! View attachment 2497939

Sent from my SM-E135F using JamiiForums mobile app
Kwa mtindo huu Bunge letu litajazwa na ma Dtk
 
Back
Top Bottom