Mbowe wa CHADEMA ana upekee gani?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,188
25,493
Sina nia mbaya kukumbusha. Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda 'alianzisha' vita dhidi ya madawa ya kulevya mkoani Dar es Salaam na sasa vita hiyo imetapakaa Tanzania nzima. RC Makonda alikuwa akiongea kwa kujiamini, kutaja na kuagiza. Alikuwa akisubiriwa kwa hamu pale alipokuwa akitakiwa kutokeza na kuzungumza.

Siku alipotajwa Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa pamoja na Manji na Gwajima, mambo yakabadilika. Kwanza, kila aliyetajwa hapo akazungumza na waandishi wa habari. Mbowe akaenda mbali zaidi na kutamka kuwa hatakwenda kuripoti Central Police kwakuwa aliyemwita (Makonda) hana mamlaka ya kumwita.

Baada ya tamko hilo la Mbowe, mambo yakachachamaa. Wakajitokeza watanzania kwa maelfu wanaomuunga mkono Mbowe na wale wanaompinga. Kilichofuata ni kuteuliwa kwa Kamishna Mkuu wa Kamisheni ya Kudhibiti na Kuzuia Madawa ya Kulevya nchini ambaye kimsingi ndiye sasa ameyachukua majukumu yake ya mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.

Kuanzia siku alipotajwa Mbowe wa CHADEMA vita ya madawa ya Makonda ikapata dhoruba kali kwa kumbadili kiongozi wa vita hiyo. Kuanzia siku alipotajwa Mbowe, hakujawahi kuwepo na kutajwa washukiwa wengine wa matumizi au kuingiza madawa ya kulevya. Siku aliyotajwa Mbowe wa CHADEMA ikawa ndiyo turning point.

Yawezekana kutajwa kwa Mbowe kukasababisha hata mashauri ya madai dhidi ya RC Makonda kuhusu udhalilishaji kama ambavyo Mbowe anapanga kuanza kufanya hivyo. Kimsingi, najiuliza, Mbowe wa CHADEMA ana upekee gani hadi 'kubadili' upepo wa mambo yote hayo?
 
Mkuu nikusahihishe, aliyetajwa na makonda ni philemony mbowe, sijui kwanini freeman anahamaki?

Huyo mbunge wa hai anasakwa na kamanda sirro kwa sababu ambazo jeshi la polisi halijasema, inawezekana ni madawa au kuhusu kauli za tundu lissu au masuala yake ya kibiashara au ni sababu anazozijua yeye sirro.
 
Jibu ni moja tu, hii vita ya madawa aliyoianzisha Makonda ni feki, wameanzia kwa wasanii, wakaja sijui kwa akina nani, lakini lengo lao kuu ni Mh. Mbowe.

Na huu ni mkakati maalum, usidhani Makonda aliamka tu asubuhi akaanzisha haya maigizo. Ni mkakati ambao ulisukwa kwa lengo la kudhoofisha upinzani wakilenga kumchafua Freeman Aikael Mbowe maana ni moja ya watu ambao ni tishio kwa chama dola. Na mkakati huu una baraka zote kutoka juu.

Na ndio maana hutasikia Makonda akiendelea kutaja tena majina maana mlengwa mkuu tayari ameshatajwa. Bahati mbaya mikakati yao huwa haifanikiwi, maana ni ya kishetani.
 
Kwanza inatakiwa uelewe kitu, toka hii vita imeanzishwa na Makonda ilikuwa haina tofauti na ile vita ya kushika madangulo ya makahaba na wale mashoga, wakati hii ya madawa ya kulevya haikuhitaji mfumo wa mapigano hayo.

Na ndio maana toka imeanza baadhi ya watu walipongeza ila waliponda approach aliyotumia bwana mdogo.

Sasa alikuja kuharibu zaidi kuita watu wenye uelewa na wajuvi wa sheria katika suala la kumuita mtuhumiwa na kumfanyia investigation, kitu ambacho kinatakiwa kiwe kisheria zaidi kuliko ki propaganda, kama alivyokuwa akifanya mwanzo.

Kwahiyo upekee wa Mbowe una kuja kwamba alikuwa anaelewa taratibu na sheria za kuitwa kwake kama mtuhumiwa, kitu ambacho hakikufuatwa, na zaidi ni kama alitaka kuwaweka sawa katika suala zima la approach ambavyo ilitakiwa kuwa.

Kama unakumbuka vizuri siku anaongea na waandishi wa habari aliwaambia ni nini hasa hawezi kwenda kutokana na mbinu illegal waliyotumia kumuita, japo alisema pia yupo tayari kutoa ushirikiano wa kutosha katika vita hii ya madawa ya kulevya.

Na hili pia lilichangia, mpaka kumwamsha Rais kutoka usingizini, mpaka kuhoji sheria husika ya kudhibiti madawa ya kulevya ilipokuwa imefichwa, ili iweze kutolewa na kufanya kazi.
Kilicho shangazi zaidi ni kuwa wahusika walikuwepo pale pale ila hawajijui kama walikuwa sehemu ya usimamizi wa hiyo sheria yenyewe. Sasa sijui kule Bungeni walikuwa wamelala kipindi inapitishwa?
 
Jibu ni moja tu, hii vita ya madawa aliyoianzisha Makonda ni feki, wameanzia kwa wasanii, wakaja sijui kwa akina nani, lakini lengo lao kuu ni Mh. Mbowe.

Na huu ni mkakati maalum, usidhani Makonda aliamka tu asubuhi akaanzisha haya maigizo. Ni mkakati ambao ulisukwa kwa lengo la kudhoofisha upinzani wakilenga kumchafua Freeman Aikael Mbowe maana ni moja ya watu ambao ni tishio kwa chama dola. Na mkakati huu una baraka zote kutoka juu.

Na ndio maana hutasikia Makonda akiendelea kutaja tena majina maana mlengwa mkuu tayari ameshatajwa. Bahati mbaya mikakati yao huwa haifanikiwi, maana ni ya kishetani.
Tishio kwa dola kivip? Ina maana mbowe asipokuwepo na upinzani unakufa?kwa hyo mbowe ndio upinzani?
 
Mkuu nikusahihishe, aliyetajwa na makonda ni philemony mbowe, sijui kwanini freeman anahamaki?

Huyo mbunge wa hai anasakwa na kamanda sirro kwa sababu ambazo jeshi la polisi halijasema, inawezekana ni madawa au kuhusu kauli za tundu lissu au masuala yake ya kibiashara au ni sababu anazozijua yeye sirro.
Na wewe umesahau. List ile ilitaja Philemon Mbowe, mwenyekiti wa CHADEMA na mbunge wa Hai. Polisi wakasema regardles of the name, mbunge wa Hai na mwenyekiti wa chadema anafahamika, kwa hiyo anatakiwa kuripoti kituo cha Polisi. Hapo Freeman (sio Filemon) Mbowe kama mbunge wa Hai ndipo alipojitokeza kwenye media na kukataa kuripoti polisi.
 
Mbowe ni mwenyekiti chama cha upinzani na JPM ni mwenyekit wa CCM hiv makonda anaweza kumuita JPM hiv hiv?
Mkuu, Mbowe anaishi Mikocheni Dar. Makonda ni mkuu wa mkoa wa Dar, kwanini asiwe na mamlaka ya kumuita mkazi wake aende central police. Kina Iddi Azzan na wengine mbona walikwenda central na mambo yakaisha?.

Mzee Mtei ambaye ndiye mwanzilishi wa CDM kasema Mbowe ajitafakari hapa alipofikia, kwani kutajwa jina lake ni doa kwa chama ambacho yeye Mzee Mtei alikianzisha.


Tatizo ambalo ni la msingi ni baadhi ya wanasiasa kushindwa kubadilika kadri ya muda unavyokwenda. Siasa za kuvimbiana zilifanyika enzi zile za JK aliyeweza kumchekea yoyote yule aliye mbele ya macho yake. Awamu ya tano haivimbiwi kipuuzi tu.
 
Jibu ni moja tu, hii vita ya madawa aliyoianzisha Makonda ni feki, wameanzia kwa wasanii, wakaja sijui kwa akina nani, lakini lengo lao kuu ni Mh. Mbowe.

Na huu ni mkakati maalum, usidhani Makonda aliamka tu asubuhi akaanzisha haya maigizo. Ni mkakati ambao ulisukwa kwa lengo la kudhoofisha upinzani wakilenga kumchafua Freeman Aikael Mbowe maana ni moja ya watu ambao ni tishio kwa chama dola. Na mkakati huu una baraka zote kutoka juu.

Na ndio maana hutasikia Makonda akiendelea kutaja tena majina maana mlengwa mkuu tayari ameshatajwa. Bahati mbaya mikakati yao huwa haifanikiwi, maana ni ya kishetani.

Majibu yenyewe kama ndiyo haya, basi mkoloni akiamua kurudi Barani Afrika ni rahisi sana kututawala tena!! Oh yes - we're disorganised lot mpaka tunasahau kabisa kuwa wamoja katika vita ya ku-save nguvu kazi ya Taifa letu dhidi ya madawa ya kulevya, badala yake mnakimbilia kumtetea MBOWE wakati hamjui alikuwa anaitwa Kituo cha Polisi kwa kosa gani? - masaa yote kutumbukiza siasa kwa kusingizia Serikali kwamba inakadamiza demokrasia na kudhoofisha upinzani Nchini, actually yeye kama Kiongozi wa upinzani alipashwa kuonyesha mfano bora kwa kuiitikia wito wa Polisi kuliko kubishana bishana nao, kwani walio itikia mwito wa Polisi kawazidi nini?
 
Mbowe ni kiongozi wa waj...a,mwalimu wa vip..u. injili yake haipingiki hatuna uwezo wa kuipinga. Hata akituuza tutakwenda tulikouzwa bila makwesheni.
 
Majibu yenyewe kama ndiyo haya, basi mkoloni akiamua kurudi Barani Afrika ni rahisi sana kututawala tena!! Oh yes - we're disorganised lot mpaka tunasahau kabisa kuwa wamoja katika vita ya ku-save nguvu kazi ya Taifa letu dhidi ya madawa ya kulevya, badala yake mnakimbilia kumtetea MBOWE wakati hamjui alikuwa anaitwa Kituo cha Polisi kwa kosa gani? - masaa yote kutumbukiza siasa kwa kusingizia Serikali kwamba inakadamiza demokrasia na kudhoofisha upinzani Nchini, actually yeye kama Kiongozi wa upinzani alipashwa kuonyesha mfano bora kwa kuiitikia wito wa Polisi kuliko kubishana bishana nao, kwani walio itikia mwito wa Polisi kawazidi nini?
Huyo rais wako mwenyewe anaendesha nchi kisiasa, unajifanya kipofu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom