Mbowe: Tumechoka!

Mbowe: Tumechoka!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
 
Hivi Mh maguli yupo? Au kasafiri nje ya nchi, amesikia au hajasikia?
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwakwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.



Kwa hiyo kama amechoka sisi tufanye nini sasa? Mwambie aende Dubai likizo kupumzika! Halafu pia mwambie awaache Askari wetu wafanye kazi yao, Askari wetu wana uwezo wa kuingia popote pale ndani ya ardhi ya TanZania hivyo hata yeye Mbowe pia ajitayarishe tu siku wakimpigia hodi atoe ushirikiano!
 
Kwa hiyo kama amechoka sisi tufanye nini sasa? Mwambie aende Dubai likizo kupumzika! Halafu pia mwambie awaache Askari wetu wafanye kazi yao, Askari wetu wana uwezo wa kuingia popote pale ndani ya ardhi ya TanZania hivyo hata yeye Mbowe pia ajitayarishe tu siku wakimpigia hodi atoe ushirikiano!
Unaweza ukadhani ni sifa lakini kinachojengwa ni kiovu kupitiliza.Hujui kesho yako.Siasa siyo mwisho wa kila kitu.Kuna maisha nje ya siasa.
 

Kwa hiyo kama amechoka sisi tufanye nini sasa? Mwambie aende Dubai likizo kupumzika! Halafu pia mwambie awaache Askari wetu wafanye kazi yao, Askari wetu wana uwezo wa kuingia


popote pale ndani ya ardhi ya TanZania hi yeye Mbowe pia ajitayarishe tu siku wakimpigia hodi atoe ushirikiano!
Kweli askari wenu...
 
Yupo Arusha,hawezi kusema maana ndiye aliyetoa order.Na pia watasema haimuhusu inamuhusu Mkuu wa Mkoa na Mkurugenzi
Makada tuwe waungwana japo kwa muda mfupi. Kikwete alikuwa mwepesi sana wa kuzungumza pindi ishu kama hizi zinapojitokeza. Tukamuona punguwani na dhaifu. Sasa tunaanza kulia ia ili rais aingilie. Sasa ujinga tufanye sisi tumlaumu Rais wetu? Kwa lipi?
 
Sasa kama Mwenyekiti wetu anaishia kulalamika, sisi mashabiki tutafanyaje? Haya ndo madhara ya chama chetu kuongozwa na mtu ambaye hajapevuka kisiasa. Bora Mwenyekiti awe Lowasa, mzee wa maamuzi mahumu
Wahi dirisha la ulua lumumba.
 
Mbowe amekuwa dhaifu mno, kama uongozi wa chama umemshinda aachie damu changa akina Mnyika. Kiongozi wa chama cha upinzani hatakiwi kuwa anakubali kila dhuluma anayofanyiwa na chama tawala na polisisiemu na kuishia kutoa matamko yasiyo na tija.

Itisha maandamano Mbowe, Lijualikali amekataliwa kupiga kura, huku Dar wabunge wanadhalilishwa wewe unaleta matamko yasiyo na tija. Hakuna hata tamko moja limeleta faida. If you cant beat them join them achia chama watu wa kazi
 

Kwa hiyo kama amechoka sisi tufanye nini sasa? Mwambie aende Dubai likizo kupumzika! Halafu pia mwambie awaache Askari wetu wafanye kazi yao, Askari wetu wana uwezo wa kuingia popote pale ndani ya ardhi ya TanZania hivyo hata yeye Mbowe pia ajitayarishe tu siku wakimpigia hodi atoe ushirikiano!
poor you
 
Sasa kama Mwenyekiti wetu anaishia kulalamika, sisi mashabiki tutafanyaje? Haya ndo madhara ya chama chetu kuongozwa na mtu ambaye hajapevuka kisiasa. Bora Mwenyekiti awe Lowasa, mzee wa maamuzi mahumu
Eti anasema amechoka, si ajiuzuru sasa.
 
Makada tuwe waungwana japo kwa muda mfupi. Kikwete alikuwa mwepesi sana wa kuzungumza pindi ishu kama hizi zinapojitokeza. Tukamuona punguwani na dhaifu. Sasa tunaanza kulia ia ili rais aingilie. Sasa ujinga tufanye sisi tumlaumu Rais wetu? Kwa lipi?
Ushauri wapelekee walokutuma wakuongezee malipo. Huna hoja
 
Huu ni uhuni wa kisiasa tu na inashangazwa sana pm, vice na preda wote wapo lkn no say...
 
Back
Top Bottom