Mbowe akizungumza katika hospitali ya Selian jana aliwataka wanachama wa chama hicho watulie kwa sababu tukio hilo ni kubwa na lina mambo mengi ndani yake.
Alisema wanachofanya sasa ni kuhakikisha kuwa watu waliojeruhiwa katika tukio hilo wanapata matibabu kwanza.
Mbowe aliwataka watu wote waliopotelewa na ndugu kufika katika hospitali zote za mji wa Arusha kutambua ndugu zao waliojeruhiwa.
Alisema Chadema itagharimia matibabu ya watu wote waliojeruhiwa katika tukio hilo.
Mbowe alisema chama chake kwa sasa hakiwezi kutoa tamko lolote kuhusiana na tukio hilo la bomu kwa sababu wanafuatiliwa na baadhi ya askari polisi na maofisa wa Usalama wa Taifa.
My take;
Mhe Mbowe, watanzania wote tungependa kujua hayo mambo mengi yaliyo ndani ya tukio la mlipuko uliotokea kwenye mkutano wako wa kufunga kampeni ni yapi hasa.
Ni vyema ukaweka hisia zako juu ya jeshi letu la polisi pembeni, na ushirikiane nao kuwapa ushahidi usio na shaka ili waweze kuwabaini wahusika wakuu wa tukio hilo la mlipuko.
Alisema wanachofanya sasa ni kuhakikisha kuwa watu waliojeruhiwa katika tukio hilo wanapata matibabu kwanza.
Mbowe aliwataka watu wote waliopotelewa na ndugu kufika katika hospitali zote za mji wa Arusha kutambua ndugu zao waliojeruhiwa.
Alisema Chadema itagharimia matibabu ya watu wote waliojeruhiwa katika tukio hilo.
Mbowe alisema chama chake kwa sasa hakiwezi kutoa tamko lolote kuhusiana na tukio hilo la bomu kwa sababu wanafuatiliwa na baadhi ya askari polisi na maofisa wa Usalama wa Taifa.
My take;
Mhe Mbowe, watanzania wote tungependa kujua hayo mambo mengi yaliyo ndani ya tukio la mlipuko uliotokea kwenye mkutano wako wa kufunga kampeni ni yapi hasa.
Ni vyema ukaweka hisia zako juu ya jeshi letu la polisi pembeni, na ushirikiane nao kuwapa ushahidi usio na shaka ili waweze kuwabaini wahusika wakuu wa tukio hilo la mlipuko.