CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kesho kutwa kinatarajia kufanya mkutano mkubwa wa hadhara mkoani Mwanza kutoa tathmini ya mapambano ya vita dhidi ya mafisadi.
Mkutano huo unaotarajiwa kuhutubiwa na Mwenyekiti wake, Bw. Freeman Mbowe, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu CHADEMA itangaze orodha ya mafisadi 11 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Mwembeyanga, Dar es Salaam, Septemba 15, mwaka jana.
Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa CHADEMA, Bw. David Kapalila, alisema mkutano huo pia utahudhuriwa na viongozi wengine wa kitaifa wa chama hicho.
"Katika mkutano huo viongozi wa CHADEMA wataeleza mwelekeo wa vita dhidi ya ufisadi na jinsi CCM ilivyoshindwa kupambana nayo,"alisema Bw. Kapalila.
Alisema kutokana na CCM kushindwa kupambana na vitendo hivyo, chama chake kitatumia mkutano huo kutangaza mkakati maalumu wa kupambana na mafisadi ili kutokomeza vitendo hivyo.
Mbali na Bw. Mbowe, alitaja viongozi wengine watakaohutubia mkutano huo kuwa ni pamoja na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, naibu wake, Bw. Zitto Kabwe na Mwanasheria wa chama hicho, Bw. Tundu Lisu
Bw. Kapalila alisema mkutano huo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Kamati Kuu kilichokutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Katika mkutano uliofanyika viwanja vya Mwembeyanga, mwaka jana Dkt. Slaa akisaidiwa na Bw. Lisu walitaja orodha ya vigogo 11 waliodaiwa kuhusika na vitendo vya kifisadi.
Baadhi ya viongozi hao ni aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi, Katibu Mkuu Hazina, Bw. Gray Mgonja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa.
Baadhi ya vigogo waliotajwa kwenye orodha hiyo walitishia kumburuta Dkt. Slaa mahakamani, lakini hadi leo hakuna aliyethubutu kuchukua hatua hiyo.
Kama ni kurudia yale yale ambayo kila mtu anayajua hakuna hata haja ya mkutano, ishu ingekuwa kutumia nguvu, shinikizo na msaada wa nchi zinazosaidia katika bajeti kuhakikisha kuwa mafisadi wote wamechukuliwa hatua, short than that ni kumpigia mbuzi gitaa.
habari imeandikwa tangu juzi usiku itakuwaje BREAKING NEWS au ndio unazi wa CHADEMA umekujaaa tuu?
Hivi hawa bado wanazo politics za kulipua mabomu? washamsahau huyu mwenzao?
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbrod Slaa ameendelea kuibana serikali na sasa ameibuka na jipya kuwa fedha zilizoibwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zilitumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendeshea kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.
Dk Slaa alitoa tuhuma hizo jana akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam.
Alisema fedha hizo bado hazijarejeshwa ndio sababu serikali imeshindwa kuwataja waliozirejesha au kuwachukulia hatua za kisheria.
Dk Slaa alisema fedha hizo za EPA hususan za Kampuni ya Kagoda na Deep Green Finance zilitumiwa na CCM kuendeshea uchaguzi mkuu wa 2005 uliomuweka madarakani Rais Jakaya Kikwete.
"Hatujawahi kusema maneno haya lakini leo tunatangaza rasmi kwamba fedha za EPA hususan za Kagoda na Deep Green Finance zilitumiwa na CCM kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa 2005 ulioiweka madarakani serikali hii ndio maana inashindwa kuwachukulia hatua za kisheria wahusika," alsema Dk Slaa.
Alisema kauli za kurejeshwa kwa fedha hizo ni za kujikanganya na kwamba hazijarejeshwa, jambo ambalo limeifanya serikali kushindwa kueleza kiasi kilichorejeshwa na wahusika waliozirejesha.
"Hazijarejeshwa kwani hata Rais hakuwa tayari kusema ziko wapi alipotoa hotuba yake bungeni, Akaunti maalum za serikali zipo sita na hakuna hata moja kati ya hizo ambayo imeingiza fedha za EPA au Rais atuambie ni ipi kati ya hizo iliyotumika kurejesha fedha hizo," alisema.
Alisema Kamati Kuu ya Chadema imesisitiza kuwa uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuwafikisha mahakamani wezi wa EPA ni mfano mbaya wa utawala.
Alifafanua wezi wote wa EPA wanakabiliwa na kosa la wizi na sio deni na hivyo kuwataka warejeshe fedha hizo ni sawa na kuvunja sheria kwa kubadilisha kesi ya jinai na kuwa kesi ya madai.
Hata hivyo CCM kwa nyakati tofauti iliwahi kukana tuhuma za kuhusika kwake na kueleza kuwa wananchi wasubiri uchunguzi wa timu ya Rais ambayo hata hivyo haikuwekwa hadharani.
Kuhusu wajibu wa Chadema kupambana na ufisadi, Dk Slaa alisema Kamati Kuu ya chama hicho, imeagiza kuwa kazi hiyo iendelee mpaka hapo serikali itakapoamua ama kuondoka madarakani au kuwachukulia hatua mafisadi.
''Ili kupanua wigo wa mapambano dhidi ya ufisadi nchini, Kamati Kuu imeazimia kuwa viongozi wote wa chama kuanzia ngazi ya tawi wanapaswa kuchukua hatua za kupambana na vitendo vyote vya kifisadi vinavyofanywa na serikali katika maeneo yao na kuwasilisha taarifa hizo katika uongozi wa juu wa Chama,'' alieleza Dk Slaa.
Aidha Dk. Slaa alisema Chadema inaendelea na mashtaka dhidi ya watu na vyombo vyote vya habari vilivyohusika katika kuwachafua viongozi wa chama hicho kwa kuandika habari zilizolenga kuharibu sifa ya chama na viongozi wake mara baada ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime Chacha Wangwe.
''Kamati Kuu imeiagiza Secketarieti kuwasiliana na jeshi la polisi kutoa ufafanuzi iwapo kwenye upelelezi wao kuhusu kifo cha Wangwe kuna sababu nyingine zaidi ya ajali iliyosababisha kifo hicho na kama ipo Kamati Kuu itaomba uchunguzi kufanyika," alisema Dk Slaa.
Alisema Kamati Kuu ya Chadema imeunda kamati ndogo ikiongozwa na Muasisi wa chama hicho,Bob Makani kufanya uchunguzi dhidi ya viongozi na wanachama wanaotuhumiwa kukihujumu chama katika ngazi mbalimbali.
Alifafanuwa kuwa taarifa ya kamati hiyo itawasilishwa kwenye kikao kijacho kwa ajili ya hatua zaidi kuchukuliwa kwa wote watakaobainika kuhusika.
Akizungumzia kuhusu matumizi ya ruzuku, Dk Slaa alisema kutokana na hisia kuwa fedha za ruzuku zinaishia Makao Makuu, Kamati Kuu inamtaka Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG), kuiweka hadharani taarifa yake ya ukaguzi wa fedha za vyama vya siasa ambavyo vinapata ruzuku ya serikali kuanzia 2005 hadi mwaka huu.
Kuhusu shutuma za ubaguzi na ukabila ndani ya chama, alisema ni mkakati wa dhahiri uliolenga kukichafua chama unaofanywa na wapinzani wao na kutokana na hali hiyo wametoa orodha ya viongozi wakuu, wakurugenzi na maafisa waandamizi wa chama makao makuu kwa majina na maeneo wanayotoka.
''Tunafahamu kuwa uongo ukiachwa utamalaki Watanzania wanaweza kuamini uongo huo kuwa ndio ukweli, mfano kati ya viongozi watano wa ngazi ya taifa ni mmoja tu anatoka Kilimanjaro (Mchaga), na kati ya wakurugenzi 10 walioteuliwa na kamati kuu ni watatu tu wenye asili ya Mkoa wa Kilimanjaro (Wachaga) huku kati ya Maofisa waandamizi 12 ni mmoja tu Mchaga" alisema Dk. Slaa.
Kiasi kwani wameishiwa na sasa sera zao ni kulipua mabomu, bahati mbaya hayalipuka yanbaki ardhini na accidentally yanakuja walipukia wenyewe!