Kwa hakika hii ni kauli njema sana kwa kuwa hivi sasa CHADEMA inaonekaana dhahiri kujiridhisha mifumo na taratiz za CCM kwa mfano viongozi wa kuu wa Chama kuwa viongozi wa kuu wa Serikali. Hivi sasa Mbowe ni Mwenyekiti wa Chama na pia ndio Kiongozi wa Kambi Rasim ya Upinzani bungeni (kwa upinzani nafasi hii ni sawa na urais) Kwa maneo mengine Mbowe anaongoza Serikali ya Upinzani na pia anaongoza vikoa vya chama vinavyopaswa kufanya tathmini ya utendaji wake. Hapa hakuna "Checks and Balances" za kutosha na ndio maana katika siku za karibuni CHADEMA imeanza kudorora.
Kwa maoni yangu Mbowe anapaswa kuchagua nafasi moja katia ya Uenyekiti wa Chama na Uongozi wa Kamabi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Hii pia ni kwa wabunge wote wa CHADEMA kuachaia nafasi zote ndani ya chama ikiwemo Kamati Kuu na na Halmashauri Kuu ili wakawatumikie wapiga kura wao la sivyo CHADEMA ijitayarishe kupoteza majimbo mengi 2015. Ikiwa wabunge wa CHADEMA akina Zitto, Mnyika na wengineo wenye nyadhifa ndani ya chama watashindwa kuziachia ili vijana wengiwe waweze kuchomoza na kujulikaan kwa wapiga kura mapema kama ilivyokuwa kwa wao watatuthibitishia kuwa wan tamaa ya madaraka kama wenzao wa CCM.