Mbowe: Ni ujinga nchi kufikiria ina uwezo wa kukabiliana na COVID-19 kwa utaratibu wake wa ndani bila kujifunza kutoka kwa waliotangulia mapambano

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,035
142,137
Mwenyekiti wa Chadema na KUB Mh Freeman Mbowe anazungumza na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi kuhusu Corona.

UPDATE

Tangu WHO ilipotangazwa ugonjwa wa Corona kuwa ni janga la Kidunia, sisi kama CHADEMA tumeendelea kuamini katika ushirikishwaji wa kila mmoja katika nchi hii kwa pamoja kwenye mapambano

Janga hili linahitaji dunia kupambana pamoja kwa kushauriana na kusaidiana. Watawala wasiotambua hili ni janga kubwa kwa watu wao sasa na siku za usoni, hakika wanajitayarishia na wanastahili anguko kubwa la kisiasa.

Ushirikiano unahitajika kwa kiasi kikubwa, mfano nchi ya Syria kulikuwa na vita kali lakini hivi sasa pande zote mbili zimesimamisha vita ili kupambana kwa pamoja. Huu ndiyo ushirikikiano ambao sisi CHADEMA tunatamani kuuona katika nchi yetu

Tulitii kwa Serikali na tukasitisha mikutano yetu ambayo ilikuwa tuifanye mwezi Aprili, nimezungumza na Mhe. Rais, Waziri Mkuu, Waziri wa Fedha na Spika wa Bunge nimewapa moyo na mawazo kwa niaba ya chama ili tushirikiane kupambana na COVID-19

Nimezungumza Bungeni na hapa tunatoa mapendekezo kwa Serikali ilete hoja ya dharura Bungeni, tuache mambo mengine yote na tujadili janga hili kwa kina. Pia ifanye marekebisho makubwa ya bajeti ya mwaka 2020/21 kwani ikibaki iliyo haitatekelezeka

Tunashauri Mhe Rais asione aibu juu ya janga hili, halikuanzia Tanzania na watumishi wake hawapaswi kuficha chochote, bajeti kubwa itengwe katika kupambana na janga hili haraka iwezekanavyo

Njia kuu ya kisayansi ya kupunguza au kuzuia maambukizi ya Covid-19 ni kuvunja mwingiliano wa watu (breaking the cycle of human interaction) . Wengi wanatambua mfumo huu kama "Lock down" ni njia ngumu na yenye gharama kubwa za kiuchumi hususani kwa nchi masikini

Ni ujinga uliopitiliza kwa nchi yoyote kufikiria ina uwezo wa kukabiliana na janga hili la #COVID19TZA kwa utaratibu wake wa ndani, iwe kwa misingi ya kiuchumi, kisayansi, kitabibu ,kiutamaduni, kwa imani za kidini na mbaya zaidi hata kwa imani za kishirikina"

Ni ujinga zaidi kutokujifunza kwa uzoefu kutoka kwa nchi zilizotangulia kupambana na janga hili la #COVID19, janga hili linahitaji dunia kupambana pamoja kwa kushauriana na kusaidiana

Serikali iunde 'COVID-19 Task Force' na iwashirikishe watu wengine nje ya Serikali na kamati hizo ziwe katika kila ngazi na viongozi wa kamati hizo wachaguliwe kwa kuzingatia uwezo wao na si vyeo vyao

Mimi binafsi, ni Mhanga wa janga hili kwani mwanangu alikuwa miongoni mwa wahanga 10 wa kwanza. Aliambukizwa na kupelekea familia nzima kuwa chini ya karantini huku kijana akiendelea na uangalizi na matibabu hadi leo ikiwa ni takribani wiki zaidi ya 5

Kwa nyakati mbalimbali, binafsi nimezungumza suala hili na namna bora ya kushughulika kwa pamoja kupambana nalo. Nimezungumza na Rais, Waziri Mkuu, Waziri wa Afya, Spika wa Bunge na Naibu wake, Mawaziri kadhaa moja kwa moja au kupitia Kamati mbalimbali za Kibunge.

Tunatambua vile vile juhudi zinazofanywa na vyama vingine vya siasa vya Upinzani, hususan Chama cha ACT Wazalendo na CUF, Taasisi mbalimbali za Dini, Taasisi mbalimbali za Kiraia na Kitaaluma, vyombo vya habari, makundi ya wawekezaji na umoja wa wafanyabiashara.

Nchi nyingi duniani zimeimarisha mahusiano na umoja wa Kitaifa kupitia janga hili, msingi mkubwa ukiwa ni kuweka tofauti zao zozote pembeni, kisha kushikamana na kunia pamoja

Hapa kwetu Tanzania, umoja wetu wa Kitaifa unaelekea kuparaganyika zaidi kwa namna Serikali ya Rais John Pombe Magufuli ilivyolipokea na inavyoratibu mapambano dhidi ya Janga hili. Madaraka na Mamlaka yao yatambue wakati wote kuwa Mamlaka Kuu na ya mwisho hapa Tanzania ni Umma wa Watanzania wenyewe.

Kwa msingu huu, sasa tunaamini pasipo shaka kuwa njia bora zaidi ya kuisaidia Serikali na hatimaye wananchi ni kutokukaa kimya. Tunapotoa ushirikiano kwa kusema ndani ya vikao, Serikali haionyeshi kujali vya kutosha na inapunguza kasi ya mapambano katika vita hii.

Sasa tumeamua kuisaidia zaidi serikali kwa kuanika kwa uwazi maeneo mbalimbali ambayo tunaamini ikiyafanyia kazi itaweza kuthibiti kwa kiwango kikubwa janga hili.

Aidha, tunawasihi wananchi wote sasa wajifunze zaidi kupaza sauti zao katika kutetea uhai wao. Kila mmoja apige kelele kwani ukimya na Upole wa Watanzania ndiyo unaowapa CCM na Serikali yao jeuri ya kupuuza maoni yao.

Sisi kama Chama Kikuu cha Upinzani hatuoni Serikali ikipokea na kutambua ushauri wetu. Tunaamini hali hii iko vilevile kwa vyama vingine na makundi mengine yaliyo nje ya Chama cha Mapinduzi na Serikali yake. Nina vielelezo kadhaa vya ni kwa nini tunaamini hivyo.

Kwa ukubwa wajanga hili, ungetegemea Bunge makini hadi hatua ya sasa,lingekuwa limeshaiamuru Serikali kuleta taarifa rasmi Bungeni ili kuwapa Wabunge,kwa niaba ya wananchi fursa ya kupata taarifa rasmi ya serikali, kuijadili na kuishauri na au kuielekeza hatua za kuchukua.

Katika mazingira ya kutatanisha na kushangaza, Bunge halijatekeleza wajibu huu licha ya kuwepo maombi mara kadhaa toka kwa wabunge hususan wa Upinzani kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji Bunge.

Rai hii ya Upinzani, nimeifikisha binafsi kwenye vikao vyote mahsusi vya Kamati za Kiuongozi za Kibunge, bila kupewa kipaumbele chochote. Hii ni pamoja na Kamati ya Uongozi, Kamati ya Bajeti na hata Tume ya Utumishi wa Bunge.

Zaidi, soma: FULL TEXT: Hotuba ya Mwenyekiti wa CHADEMA (T) na KUB kwa Umma wa Watanzania kuhusu COVID-19 - JamiiForums

 
Hahahaaaa....... Lumumba tumefundishwa ustaarabu bwashee!
... ustaarabu gani wa kuwahi kuanzisha thread then no updates or not detailed? Unajua kabisa wengine watakaoanzisha baada yako mods wataziunganisha na ya kwako na zitakuwa chini huko updates hazitaonekana kirahisi. Umefanya hivyo makusudi wala sio kwa bahati mbaya; communist ideology ni tatizo duniani.
 
April 29, 2020

Live / mubashara
Mbowe anaongea na waTanzania kuhusu Covid-19

Kiongozi wa Upinzani Bungeni (KUB) na mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Mh. Freeman Aikael Mbowe mbunge wa jimbo la Hai anaongea na taifa


Mh. Freeman Mbowe aililia nchi yetu Tanzania kutokana na serikali kukosa mikakati kukabiliana na gonjwa la Covid-19

Mbowe aishauri Tanzania ijitokeze kimataifa na kikanda ikiongozwa moja kwa moja na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuongoza majadiliano na Mataifa mengine, vyombo kama WHO, SADC badala ya kuwaachia mawaziri kuongoza vita dhidi ya Covid-19
Source : millard ayo
c.c : johnthebaptist

Tanzania opposition slams 'state of denial' over coronavirus
Wednesday, April 29, 2020 22:46 WIB

Dar es Salaam, April 29, 2020 (AFP)
Tanzania's main opposition leader on Wednesday accused the government of hiding information on the coronavirus and failing to take the pandemic seriously.
Tanzania is one of few countries in Africa that has not taken extensive measures against the virus, and President John Magufuli is among a handful of world leaders still playing down the seriousness of the disease.

"Our cases are shooting up at an alarming rate while many countries are now flattening the curve," said Freeman Mbowe, of the opposition Chadema party, in a speech broadcast online.

Tanzania recorded its first case of coronavirus on March 16 -- and in a little over two weeks cases have leapt from 32 to 480 with 16 deaths.

While relatively small on a global scale, the growth is among the highest in East Africa, where most countries have implemented lockdowns, curfews, and strict social distanncing measures.

In Tanzania, schools and universities have been shut but markets, bus stops and shops bustle as usual.

Opposition members have also criticised the government for waiting a week to announce new cases, after Magufuli on April 22 said the ministry of health was "causing panic".

"I have information that there are many people who recovered but these are not given priority in announcing. I see they are competing to announce new cases and deaths which are causing panic," the president said.

Prime Minister Kassim Majaliwa provided an update Wednesday amid mounting pressure to do so. Mbowe questioned the veracity of the numbers released.

"We see people dying and their burials are supervised by the government under strict conditions but yet it is not telling us they died of coronavirus. There is no transparency and when people have no information, you provide room for rumours. The government is telling us only 16 died of coronavirus but this is a joke," he said.

Mbowe said that Magufuli, who has been staying in his home town of Chato in northwestern Tanzania since March 28, was in a "state of denial".

Magufuli has claimed God would protect Tanzanians from the virus, and has urged people to keep working as usual. "This is time to build our faith and continue praying to God and not depending on facemasks. Don't stop going to churches and mosques for prayers. I'm sure this is just a change of wind and it will go like others have gone," Magufuli said at a church in Dodoma last month.

Magufuli came to power as a corruption-fighting "man of the people" but has since been criticised for his authoritarian leadership style, with rights groups citing a crackdown on the media and critics during his rule. He is due to run for a second term in polls due in October.

Source : AFP

More info :

April 30, 2020
Dodoma, Tanzania

BUNGE LIVE: CORONA, MBOWE ASHAMBULIWA VIKALI - "WAWEKE CHADEMA LOCKDOWN, UNGESEMEA BUNGENI"

Bajeti ya wizara ya afya imeanza kujadiliwa Bungeni leo Aprili 30, baada ya waziri mwenye dhamana, Ummy Mwalimu, kuiwasilisha Bungeni hapo.. Wizara hii imepata wachangiaji wengi kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona, ambao mpaka sasa umeshagharimu maisha ya watanzania 16...


Source : Global TV online

April 30, 2020
Mbeya, Tanzania

Mkuu wa mkoa wa Mbeya RC Albert Chalamila aongelea hotuba ya Mbowe



Source : millard ayo
 
Back
Top Bottom