Mbowe ndani ya Bunge

Mbowe ndani ya Bunge

PrN-kazi

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2011
Posts
2,900
Reaction score
445
Aisee, napita: taarifa ni kwamba Mbowe yuko anatema cheche Bungeni, walioko karibu na TV tune TBC, ushuhudie kinachoendelea Dodoma
 
Huku hakuna umeme ndugu, kama vp tujuze kinachoendelea
 
Aisee jamaa ameshusha nondo za ukweli!anasema hatuwez kuvumilia slogan za kuvua gamba wakat wananch wapo gizan!pia anashangaa makamba na waziri wanaongea lugha tofauti,kamkaribisha aende chadema wafanye kazi!ukumbi wa bunge ulikua kimya hakuna anayegonga bench wala nn!ameongea mengi sana!kasema pia wizara ya nishati igawanywe!nishati iwe peke yake na madini iwe peke yake!pia amehitimisha kwa kusema kuna kampuni inaitwa orca!ni wasanii wanajisifu jins walivyokwepa kodi ya 13bilion.
 
Huku sauti za majenereta zinatuua huku! Hatusikilizani.
 
Tupeni zaidi wakuu, huku tumepigwa unawanted in this country!!
 
hawa wabunge wa ccm wana matatizo, muongeaji Mhe Gaundensi-mbunge kutoka Mbinga aliyefuata kuchangia baada ya Mbowe, badala ya kuchangia mstakabali mzima juu ya nishati na madini; yeye mojakwamoja kaanza kushambulia hoja za Mbowe na kuzitolea majibu mepesi; sielewi nafasi yake hiko wapi ni waziri mbadala wa nishati na madini?
 
kuna huyu mbunge wa jimbo la kwimba!naona hata kiswahili kinampiga chenga!sijui ubunge aliupataje!kaazi kweli kweli.
 
CCM kilichobakia ni kuforce kwa nguvu mambo yao ya kitapeli yapite. Lakini sasa sisi wala hatukipendi tena maaana CCM ni wanafiki ndo haohao wamesababisha tunaishi maisha ya kubahatisha hii leo.
 
Hamna lugha ya matus, wala ufutwaj wa kauli. Acha kupotosha watu.
 
mbowe anatumia lugha ya matusi anaambiwa afute usemi

Unapotosha ndugu yangu sote tumeangalia, kilichofuatia baada ya mda wake kuisha ni Mh Lukuvi kumpa Mh Mbowe taarifa, kwamba kamati ya bunge na nishati sio cha ccm niya bunge na pia Lukuvi katoa ufafanuzi kuhusu legitimacy ya serikali. Ukweli ukuweke huru ndugu yangu.
 
hayo matusi mbona hatujayasikia?utakua unaangalia tv asilia!sasa hv anachangia Nyambari nyangwine!
 
amesema haungi mkono hoja hadi apate majibu ya maswali yake!anasema vijijin kwao hakuna umeme!mbona haongelei lile la kupigwa?
 
la muhimu nililolisikia ni kuwa watatumia nguvu ili umeme unaoenda nyamongo mgodini utatumika na wananchi!kasisitiza wataushusha kwa nguvu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom