zambez
JF-Expert Member
- Dec 28, 2013
- 2,071
- 255
Tanzania sasa imechupa mbali na inazidi kupokea mabadiliko makubwa sana haswa ya kifikra. Kilasiku tunaona mikutano ya hadhara ya wanasiasa ikifanyika kuna inayotia moyo kwa wanasiasa wanaotumia muda wao kuandaa hoja za msingi na kuongelea mambo yanayowagusa wananchi moja kwa moja, wapo wengine wanaoandaa viloja vya kwenda kutajataja majina ya watu na pumba ambazo hazina mantiki yeyote kwa wananchi. Na hii ni dharau kubwa sana kwa wananchi kuwapotezea muda wao kuja kwenye mikutanoa na hakuna wanachokipata.
Hapa nasema lazima tuwapime wanasiasa wetu kwa hoja wanazoongea je kile anachokiongea kina tija kwa wananchi, pia wanasiasa wetu lazima wabadilike zile siasa za viloja mwisho ilikuwa 2010.Watanzania wa leo hawatakubali kuuziwa Mbuzi kwenye gunia watataka kumuona anafananaje na ana ubora gani.
Wachambuzi wa masuala ya siasa tusaidieni watanzania muwe mnajitahidi kuchambua yale ambayo yamezungumzwa na wanasiasa hao katika majukwaa yao, waanikieni viloja na hoja za wanasiasa wetu. Rai kwa wanachama na washabiki tuanze sasa kutoka vifua mbele kwa hoja anazozitoa mwanasiasa tunayempenda tusiangalie tu ujazaji watu tu jukwaani hii nchi imevimba changamoto ni nyingi sana.
Wakati huu ni kuwapima wanasiasa hawa wawili kwa hoja zao wakiwepo kwenye mikutano na nje ya mikutano.
Dr. Maji marefu umeharisha hapa.....