Kumekuwa na maneno mengi na tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe kuwa anatafuna pesa za Ruzuku za chama,
Tuhuma hizo zimekuwa zikiendelea kila mara na sasa zikichagizwa zaidi na wanaohama kutoka Chadema kwenda kwenye vyama vingine hususani Ccm,
Yafuatayo ni matokeo ya Utafiti;
*NAMNA FEDHA INAVYOTOKA SERIKALINI MPAKA KUFIKA KWENYE AKAUNTI YA CHADEMA*
Serikali hutoa ruzuku kwa Chadema kila mwezi,
Fedha ikitoka Hazina (Serikalini) hupelekwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa,
Msajili huiingiza pesa hiyo kwenye Akaunti ya Bodi ya Wadhamini wa Chadema (Board of Trustee Bank Account),
Bodi ya Wadhamini wa Chadema ndio hupeleka pesa hiyo kwenye Akaunti ya Chama tayari kwa matumizi. Pesa haiingizwi kwenye Akaunti binafsi ya kiongozi yeyote wa Chadema wala mwanachama wa Chadema. Huingizwa kwenye akaunti ya chama,
*NAMNA PESA INAVYOTOKA KWENYE AKAUNTI YA CHADEMA*
Wapo Watia Saini Wanne (4 Signatories) kwenye Akaunti ya Chadema Taifa. Ambapo watu wawili kati ya hao Wanne wanaruhusiwa kusaini Hundi (cheque) kwa ajili ya kufanya Malipo,
Watu hao kwa nafasi zao ni;
i) Mwenyekiti wa Chadema Taifa
ii) Katibu Mkuu wa Chadema Taifa
iii) Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara
iv) Mkurugenzi wa Fedha
Pesa yoyote haiwezi kutoka kwenye Akaunti ya Chadema mpaka Wawili kati ya hao wanne Watie Saini,
*WAKATI GANI PESA INATOKA KWENYE AKAUNTI*
Pesa yeyote ya Chadema haiwezi kutoka kwenye akaunti kama haijathibitishwa na Kamati Kuu,
Kamati Kuu ya Chadema tayari ilishaidhinisha matumizi ya kila mwezi ya chama (Normal Operation expenditures),
Lakini kama kuna matumizi mengine ya ziada ama dharura (mfano Uchaguzi wa marudio, kesi, matibabu), lazima Kamati Kuu ya Chadema ikae, ipime umuhimu wa kufanya matumizi ndio iidhinishe au ikatae matumizi hayo,
Sio Mbowe aidhinishe, sio Mashinji aidhinishe wala yeyote yule. Ni Kamati Kuu.
*CHADEMA INAPELEKA WAPI FEDHA YA RUZUKU WANAZOPATA KILA MWEZI*
i) Zipo fedha ambazo hutumika Makao Makuu kulipa Mishahara na Posho,
Chadema inao wafanyakazi kati ya 60 hadi 70 ambao wapo Makao Makuu ama hulipwa moja kwa moja toka Makao Makuu kuanzia nafasi za Wahudumu wa ofisi, Walinzi mpaka Mwenyekiti wa Taifa,
Mwenyekiti wa Taifa na wafanyakazi wengine walioko Makao Makuu ambao ni wanufaika wa Serikali (yaani wanaolipwa mishahara kutoka Serikalini), hawalipwi mishahara na Chadema,
Freeman Mbowe _(Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Mbunge wa Hai)_, John Mnyika _(Naibu Katibu Mkuu - Bara na Mbunge wa Kibamba)_, hawa wawili ni mfano wa wasiolipwa mishahara kwa sababu ni wanufaika wa Serikali. Badala yake hulipwa posho pale wanapotumwa na chama kwenda kufanya shughuli maalum mikoani au nje ya nchi,
ii) Fedha nyingine hupelekwa kwenye Ofisi 10 za Kanda (Kanda Mbili zipo Tanzania Visiwani na Kanda 8 zipo Tanzania Bara)
Fedha hizo kwenye Kanda hutumika kulipa Mishahara ya Wafanyakazi, Posho na Ruzuku kwenye Majimbo yote 264 ya Uchaguzi,
iii) Kuna fedha hutumika kushughulikia kesi mbalimbali za Viongozi na Wanachama wa Chadema. Fedha hizo hutumika kuwasafirisha Mawakili na kuwalipa Posho.
iv) Matumizi ya dharura ambayo hayaepukiki. Mfano Chaguzi za Marudio za Ubunge (ambazo hugharimu kati ya Milioni 100 hadi 120), chaguzi za Madiwani, gharama za Matibabu na Vifaa vya Uenezi wa Chama.
Kwa kuangali mchanganuo huo hapo juu, utaona kabisa Ruzuku ya Milioni 236 wanayopata Chadema kwa mwezi, haitoshi kwa matumizi yote ya Chama kwa mwezi.
Kitendo cha kumtuhumu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe ama kiongozi mwingine yeyote kuwa anakula fedha za Ruzuku, itabaki kuwa ni propaganda za kisiasa ambazo hazina ukweli wowote,
Na ikumbukwe, hakuna kiongozi yeyote anayeweza kutoa pesa ya ruzuku kutoka kwenye akaunti ya chama mpaka watia saini wawili wasaini hundi ndipo pesa itoke,
Mbowe anakulaje fedha ya ruzuku ya chama???
*Utafiti hupingwa kwa Utafiti. Nasubiri utafiti utakaoupinga utafiti huu.*
Asanteni