Endeleaaa
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 1,485
- 738
Dr asante sana kwa ufafanuzi mzuri, lakini tuhakikishie kuwa wabunge wetu hawatasusia vikao eti tu kwa vile JK anahutubia. CHADEMA ndio chama kikuu cha ushindani bungeni tunategemea serikali kivuli itaundwa na chadema kwa ushiriki wa vyama vingine. Kumsusia Rais wa NEC itamaanisha mmesusia serikali yake pia na hiyo itamaanisha wabunge wenu kukaa kimya kipindi chote watakapokuwa bungeni. maana wataihoji vipi serikali wasioitambua?
Kitu wananchi tunakisubiri kwa hamu ni CHADEMA kuthibitisha kuwa kweli ushindi wa JK sio halali kwa kutuonesha matokeo ya jimbo kwa jimbo kwa kulinganisha na yale NEC tujue uchakachuaji umetokea wapi na wapi.
Tunaisubiri hiyo BIG SURPRISE DR.
Kitu wananchi tunakisubiri kwa hamu ni CHADEMA kuthibitisha kuwa kweli ushindi wa JK sio halali kwa kutuonesha matokeo ya jimbo kwa jimbo kwa kulinganisha na yale NEC tujue uchakachuaji umetokea wapi na wapi.
Tunaisubiri hiyo BIG SURPRISE DR.
Luteni,
Thanks a lot. Napenda kukushukuru sana. Napenda tu nikuhakikishie kuwa Chadema is not just waiting for something to happen. i) Tulitangaza kutotambua matokeo na kutomtambua Rais aliyepatikana kwa kura kuchakachuliwa. ii) Chadema hatukuhudhuria Kutangazwa kwa matokeo na wala kwenye sherehe ya kuapishwa kwa Rais. Maana yake tulikuwa tunapeleka ujumbe mzito kwa Rais aliyepatikana kwa mchakato usio halali na kwa Tume ya Taifa ya uchaguzi iliyokiri hadharani kuwa "ilifanya makosa mathalan waliponipa kura 3,789 iliyotangazwa na Judge Lewis Makame badala ya 22,021 iliyotangazwa na RO Geita. (Hatimaye walirekebisha). Maeneo mengi yalitangazwa kwa sura hiyo, japo hayakurekebishwa. Hali hii ni dhahiri iliashiria kuwa jumla ya kura za Dr. Slaa zilizokuwakitangazwa na Tume,ilikuwa au inabadilika au haifanani na Kura zilizotangazwa na RO katika Wilaya husika. Kasoro hizi baadhi zilirekebishwa wakati wa kujumlisha matokeo ya jumla, hivyo kasoro hii isiporekebishwa sura ya kura halisi ya nchi hii haiwezi kuwa sawa.iii) Tulilalamikia kubadilika badilika kwa idadi ya Waliojiandikisha kupiga kura mathalan kabla ya uchaguzi Tume ilitangaza idadi ya Wapiga kura 19,670,631 na siku ya matokeo ilitangaza idadi ya waliojiandikisha kuwa 20,137,303. Tumehoji tofauti hii hadharani. iv) Tumehoji idadi ndogo sana ya Wapiga kura 8,626,283 kati ya au 19 Millioni + au 20Millioni +) na kusababisha kiongozi wa nchi yenye watu zaidi ya 43 Millioni kuchaguliwa na idadi ndogo tu ya wapiga kura 5,276,822 kati ya wapiga kura halisi 8,398,394 tu. Hali hii inaashiria nini katika Governance? Hivyo kwa hoja hizi Chadema haikusubiri tu ...jambo literemke from heaven.
Hata hivyo katika mambo mazito kama haya, ambayo Tamko lolote linaweza kulifikisha nchi katika hatua ambayo haikutarajiwa, ni lazima Busara kubwa itumike, uvumilivu mkubwa na subira wakati Tafakuri ya kina inafanyika. Ndiyo hicho kinachofanyika Luteni.
Niseme tu subiri na Taifa lisubiri for a big surprise punde. Chadema ni chama kinachokwenda kwa mahesabu na hakikurupuki na wala hatakurupuka kamwe.