Mbowe: Lowassa ni dhaifu, ni bubu

Status
Not open for further replies.

Tumia fikra kabla ya kuandika. Hao CCM mara ngapi wameongelea kuhusu wagombea wa UKAWA na kuwatukana pamoja na mambo mengine? ACT haijawahi kuongelea kuhusu Lowassa kujiunga nao? Uwe na tabia kufuatilia siasa zinazovyoendelea sio unapayuka tu bila kufikiri. Pia ,Mbowe aliulizwa hilo swali ulitaka akae kimya?
 

kwani yeye Lowasa alipomtaja Mbowe juzi kwenye press conference inamaana anamuogopa? Tumia ubongo unapotoa post.
 
Lowasa toka nianze kumfahamu hajawahi kukemea rushwa wala ufisadi.bado anasema ooh nautaka urais
Lowasa akemee rushwa ataanzia wapi? Yeye mwenyewe anaona aibu.watu watamuuliza hata wewe?
 
sizitaki mbichi hizi duuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu???
.
Yani umejuaje Kababu....tuliwaandikia thread humu mwanzo kabisa..tukifikilia watakuwa SMART kungamua kusudio la MCHEZA SINDIMBA WA CCM, wao wakaganda kusubilia uenda akaja kwao.Na CCM kwa kung'amua hilo wakawa wana nunua muda ili wasije Wakatengeneza mpasuko kwa gharama ya huyo Mwanaccm wao.

CDM walikuwa na nafasi njema sana ya KUMKANA mtajwa KABLA ye yeye kuja na DONGO la ATOHAMA CCM...wakati macho ya WATANZANIA nzima walikuwa wanajua CCM watamfukuza MWANACHAMA WAKE huyo na KUNDI lake.Yani ata kama PLAN hiyo ilikuwepo UKIMYA wa CDM/UKAWA kupangua KUTOKUWA TAYARI kumpokea MWANACCM huyo na kundi lake unaweza kuwa ULIVULUGA PLAN yote ya CCM na hivyo uenda ikajikuta INATAFUTA PLAN B.

Yani sipati picha kama CDM/UKaWA haya anayosema Kamanda wao MBOWE angeyamwaga mapema Kabisa kabla LOWASA ajasema leo hii CDM wangekuwa vifua mbele.Matokeo yake yakawa ya FISI kutembea nyuma ya mtu kusubilia MKONO wa binadamu UDONDOKE.Wamekosa POINTI nyingi sana tena sana ...manake kwenye SWALA la UFISADI wangekuwa MBELE ya CCM kwa kuonyesha kuwa ATA pale RUMORS zilipokuwa ZINAIBUKA kuwa Kuna WANACCM kindakindaki wanataka kufukuzwa na hivyo wanategemewa kupokewa na CDM/UKAWA wao wangekuwa MBELE kuwa WALIKWISHA kataa hawapokei MAFISADI na makapi ya CCM.

Tuliwaonya sana mwanzoni semeni mapema ...wakakaa kimya UKICHEKA NA KIMA UTAVUNA MABUA.Nilitoa thread hii hapa Tetesi za CHADEMA/UKAWA kupokea Watakaotemwa Na Kaango La CCM Hakika Ni Kweli.
 

unamaana tumpe mda wakukaa ikulu hahahaaa never on earth
 
CDM na nyie muwe na huruma kwa CCM. Yaani mnajua kabisa 'wenzenu' wapo katika hali mbaya bado mnaendelea kuwa "djambisha" tu. Yaani hawajui wamfanye nini huyu EL...."ukikimbia nchale na ukichimama nchale".
 
Mbowe kakasirika sana Lowassa aliposema mimi siami CCM kwa akili ya Mbowe alikuwa anajua Lowassa atakuja Ukawa.
 
Mbowe ni mfalme pale UKAWA aweza kuhukumu mtu bila hata kumsikiiza na NCCR na CUF wakawa speachlesss nielewavyo mimi kiutaratibu lowasssa anayonafasi UKAWA vinginevyo.ithibitishwwe kwamba Hawezi kufanya hvyo

nafasi ipi wakati umeshaambiwa UKAWA hakuna nafasi yamafisadi na watoa rushwa?
 
Hapa mbowe kasema kweli pengine nilidhani anamuogopa kumwambia ukweli,lazima tujue kuwa Lowasa hawezi kukemea ufisadi kwakuwa naye ni fisadi.
 
Tatizo amekwisha achwa bandarini meli imeshang'oa nanga muda haupo upande wake tena,Lowasa ni fisadi aliyekubuhu na juzi alisema anataka Nchi iwe na matajiri 20 ndio watalisha masikini wote,anakwenda kuwa dalali balaa kuzidi hata kikwete.
 
Mbowe kakasirika sana Lowassa aliposema mimi siami CCM kwa akili ya Mbowe alikuwa anajua Lowassa atakuja Ukawa.

Wala hatumtaki mafisadi UKAWA na hakika mkimchagua mtaja mkumbuka nape Wakati mkilia na kusaga meno,wakati mnamsugua na dodoki auzike Ukawa tunasubiri kuapishwa!!
 
Lowassa akishika madaraka, tujiandae kula nyasi! Kwanza hizi gharama anazotumia kuhonga sasa, na mawsahiba zake wanazomchangia, akiingia iklu, lazima arudishe kwanza, ndio aanze kuwafikiria Wamasai wenzake, ndio aanze kuangalia na Watanzania....

Tusifanye makosa kumuuingiza EL Ikulu, tutajuta maisha yetu yote!
 
Mbowe kakasirika sana Lowassa aliposema mimi siami CCM kwa akili ya Mbowe alikuwa anajua Lowassa atakuja Ukawa.

Acha kujidhalilisha na wewe , Lowassa ndio aliyesaini MOU na kanisa kuwakandamiza waislamu , leounampigania akiwa rais si atasaini makubwa zaidi ? Mbowe kamchana Lowassa , kilio Lumumba yote ....
 
Yote uliyoandika tunayafahamu. Njoo na mengine
 
We mtu gani hata bungeni hachangii chochote...ina maana hayaoni matatizo ya watz na Hana njia mbadala ya kuyatatua? Bora alivokuwa waziri tungemtetea kuwa anaogopa kuikosoa serilali yake, lakini tangu 2008 Ni mbuge hadi Leo na hajawahi kukosoa chochote wala kukemea ufisadi na rushwa ina maana ye anaona kila kitu kipo sawa...kwahyo akiwa rais ataendeleza hayahaya sasa sijui hayo matumaini anayotuambia Ni ya nini wakati kila kitu kipo sawa..mbona wakina esta bulaya huwa wanakosoa na kupendekeza njia mbadala?
 
Lowassa ni dhaifu na Bubu.......hatuhitaji rais dhaifu tena na kibaya zaidi Bubu .......
 
Mwenyekiti wako JK kawaambia kuwa msiwe madalali na makuwadi wa wasaka urais. Wewe unafanya nini sasa?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…