Mbowe, Jipime kwa mustakabali wa CHADEMA, Kinusuru Chama

kwanza niambie au taja kwa majina hao chadema asili tuwajuwe na mbona kwa mtazmo wangu kla kitu mbowe kakikuza
 
We mtoa mada usituingilie kwa chama chetu na kamanda wetu. Jishughulishe na masuala la Lumumba. Kura mtupunguzie halafu unakuja kutoa utumbo wako. Tuna imani na Kamanda Mbowe. Mbowe oyee!
 
We fisiem pilpili usiyo ila yakuwashia nini?Tangu lini ukaitakia mafanikio chadema acha ufigisufigisu.
 
Kweli. Chadema si ajabu kikawa ni chama kizuri ila wengine tukimuangalia Mbowe, au Lema tuna conclude ni genge la wahuni illiterate.
Ni kweli, a new chairman is needed. Angalizo... Asiwe Mchaga wala mwenye undugu na Mtei, Mbowe.

Wahuni wanaisumbua ccm kiasi hiki? Nadhani itabidi nitafute dictionary ili nitafute maana halisi ya NENO Mhuni/Wahuni.

Kama tunaifahamu histori ya vyaa vingi vizuri utakua mkweli, ccm mara zote imefanikiwa kuvidhoofisha vyama vingine in less than 3 years,Chadema imeanza kuwasumbua since Mbowe alivyokua mwenyekiti wa chama hicho and this is why wanao omba Mbowe aaichie uenyekiti wa CDM ni wafuasi wa ccm cause wana mjua jamaa kua ni kisiki cha Mpingo
 
Ni utaahira kuwa na fikra hiyo. Mbowe na wanaukawa wote wanastahili pongezi. Kitendo cha kuhimili vishindo ili wasambaratike vimegonga mwamba. Bravo wana mabadiliko!!
 
ndo maana nikasema hufai kujihusisha na vyama vya kisiasa kwani mawazo yako yanakutuma kua anayegombea uraisi kwa chama fulani ndio anashika na kuitawala katiba ya chama. CCM haina sera za kunishawishi nipo ndani ya Chadema kwa zaidi ya miaka 12 sipo kwa ajili ya lowassa..

Awepo au asiwepo bado nitaendelea kua part of Movement for Change kabla ya lowassa kuwepo tumehubiri mabadiliko na itabaki kua hivyo
Twende taratibu kijana. Umewahi kuisoma katiba ya ccm pamoja na ilani ya ccm? Matendo yanayofanywa na baadhi ya wanaccm ni kinyume kabisa cha katiba ya Chama pamoja na ilani.ccm katika katiba yao inaweka utu mbele pamoja na uzalendo wa nchi.naamini hata katiba ya chadema inaelekeza mambo mazuri.watu ndio wanafanya mambo mabaya.nimekueleza haya ili utambuwe kuwa mtu msafi hana Chama.kama ana nia nzuri atatekeleza uongozi wake kupitia Chama chochote. Chadema walifanya makosa makubwa kumchukua mtu ambaye wote tunajuwa Si muadilifu na hakuwa msafi.
 
Kipimo chako cha kushindwa kwa Mbowe ni kipi? Je, ni kwa sababu CHADEMA hawajashinda urais?

Trust me bro; kwa mtindo wa kampeni zilizokuwa zinapigwa na CCM zilizotumia fedha nyingi kiasi kile, amini usiamini kama ni Dr Slaa huyu huyu angesimama badala ya Lowassa, wangeambulia kura za urais chini ya milioni moja na kunyang'anywa majimbo mengi!!

Lazima tukubali jamani kutoka kura milioni 2.6 za urais wa Dr Slaa mwaka 2010 hadi milioni 6.07 za Lowassa mwaka huu, is a big progress!!

Kutoka wabunge wa majimbo 23 hadi 34 na pengine wakaongezeka kwa yale majimbo ambayo uchaguzi haujafanyika, is a big progess!

Sina takwimu za idadi ya madiwani wa CHADEMA kwa sasa, lakini I am sure lazima itakuwa ime double kutokana na ukweli kwamba CHADEMA ikisaidizana na washirika wenzake ktk UKAWA wataongoza Halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji mengi kuliko uchaguzi wa mwaka 2010!!

Kwa kumbukumbu za matokeo ya uchaguzi huu, majiji yafuatayo yataongozwa na CHADEMA/UKAWA;

1. Dar es Salaam

2. Tanga

3. Mbeya

4. Arusha

Manispaa ni ;

1. Bukoba

2. Moshi

Halmashauri za miji na wilaya ni nyingi. Ninazokumbuka ni;

1. Tunduma

2. Karatu

3. Tarime mji

4. Tarime vijijini

5. Serengeti

6. Rombo

7. Hai

8. Siha

9. Moshi vijijini

10. Arumeru

11. Monduli nk

Hizo "leadership ethics" ni nini na ulimaanisha nini bro? Did you mean "good leadership qualities"??

Kama ulimaanisha "kiongozi bora" , then hakuna hoja ya kumtaka Mbowe aachie ngazi kwa sababu kiongozi bora ni yule ambaye huisogeza mbele taasisi anayoingoza na si kuirudisha nyuma!.

Kiongozi bora ni yule ambaye huifanya taasisi anayoingoza kupiga hatua za maendeleo kwenda mbele na si kurudi nyuma!!

So, it is absolutely wrong kumshutumu Mbowe kama mwenyekiti wa CHADEMA, kama kiongozi mkuu wa taasisi hii kwa sababu hajafeli bali amefaulu kwa kiwango kikubwa sana!!

Kwa mfumo wa uchaguzi tulionao huu, hata kama Jakaya Kikwete angejiuzuru Urais wa JMT na kuamua kujiunga na CHADEMA au hiyohiyo ACT Wazalendo yako na CCM wakiwa hawahawa, ni ngumu wakakuacha uchukue nchi!!

Jamaa Edward Lowassa kapata kura nyingi kuliko huyu aliyetangazwa mshindi, lakini wamefungia tayari hata alalamikaje hana mlango wa kutokea!

Huko Zenj si jamaa wa CUF ushahidi wa kimazingira si unaonesha wazi kuwa kashinda? Wamefanyaje?

Ktk mazingira kama haya, Bwana Freema A. Mbowe M/kiti wa CHADEMA taifa kuifikisha CHADEMA ktk hatua hii, ni mafanikio makubwa and he deserves respect and credit!!
 
Chadema itaendelea kuwepo na wanachama Wa ukweli tutaendelea kuwepo,mnafiki kama wewe huwezi kutueleza chochote,utumbo uliouandika ni sawa na kusema umemkuta jamaa na mkeo,then ukaamua kuungana na mgoni uliemkuta kwako na kuhamia kwake kabisa baada ya kutumiwa eti unarudi tena nyumbani na kuwaeleza watu ulichofanya,si wehu huo?
 
Were mawazo yako no duni. Achana na CDM hauna mawazo ya kujenga chama. Unawatumikia waliokuajiri na unachuki ya Burr na Mbowe.

Haa were unajua matokeo game chaos chilies lands use huna akili. Kama no kweenda CCM auACT nenda hakuna anayekuhitaji CDM.
 
Upinzani utashamiri tu ikiwa katiba mpya itapatikana yenye kuondoa umungu mtu na tume huru ya uchaguzi na muungano ufumuliwe na kusukwa upya ikiwa bado twauhitaji anyway. Dola iongezewe watu wenye fahamu kwa kufanya intake zao zipate watu wenye pass za hali ya juu na siyo failures. Hapo ndiyo ubabe utakoma na uchaguzi utakuwa huru na haki..

Uchaguzi huru unakuwaje? Mpaka ushinde ndio unakuwa huru?
 
Hapana Mkuu, ACT unayoisema inapata wapi ongezeko la wanachama ilhali ina Mbunge mmoja tu !! Mbowe kafanya mengi katika kikijenga chama, katika uchaguzi huu amefanikiwa kviweka pamoja vyama vinne vyenye itikadi tofauti na wote tumeshuhudia kilichoendelea na idadi ya wabunge wa upinzani walipatikana pamoja na mazingira yasiyo sawa ambayo wamekabiliana nayo.

Hata kama CDM haijashinda Urais, lakini kuna chembe ya mbegu imepandwa kwa Watanzani na itaendele akuchipuka taratibu miyoni mwao ili mradi tu wabunge wa UKAWA waisimamie Serikali ipasavyo. Pamoja na mazuri aliyofanya Mhe. Mbowe bado kuna umuhimu wa kufanya Uongozi wa Chama uwe wa Kitaifa ambao wananchi wa Tanzania wanajiona kama sehemu ya chama kupitia viongozi kutoka maeneo yao.

Kwa mfano chama kama ccm Mwenyekiti anatoka Pwani, Makamu - Iringa, Itikadi na Uenezi - Mtwara; Katibu Mkuu - Arusha; Meneja Kampeni - Mara. Unaona kabisa kuwa chama kina utaifa na hao watu wanaisadia kuoneza hicho chama katika maeneo hayo. Bulembo akismama kuongea, watu wa Mara wanaona kuwa wanawakilishwa katika hicho chama.

Sasa bila kumumunya maneno angali nyumba ya pili (CHADEMA) ambayo wanategewa kuwatoa kimasomaso husasan Uongozi wakati wa kampeni ulikuwaje: Mwenyekiti - Arusha; Mgombea - Jirani; Meneja Kampeni- Jirani; Mkurugenzi wa Fedha - Jirani; Mwenyekiti Mwenza aliyekuwa anaongea sana na vyomba vya habari-Jirani.

Katika hali kama hiyo mwananchi. Katika hali kama hii, chama kinawezaje kushika nchi ? Hebu fanyeni chama kuwa cha Kitaifa acha kulalamika ilihali mnajidhoofisha wenyewe.

Mnategemea kweli mwananchi wa kawaida kutoka kijijini akiambiwa kuwa hiki chama ni cha Kikanda atashindwaje kuamini kama kipewa mifano hiyo !!!

mkuu katibu mkuu wa ccm anatoka arusha au Somalia?
 
Binafsi nilikuwa fan wa CHADEMA O.G ila baada ya Mbowe kuleta upuuzi wa gia angani sikuona jipya zaidi ya kubaki CCM O.G

Mwaka 2010 cdm ilipata kura 2 million, mwaka huu 6 million +. Gia ya angani imeleta kura 4 million + na kashkash kubwa kwa ccm. Kama watu hawaoni hili pamoja na ujumlishaji wa kura usiokuwa na hata chembe ya credibility, basi tumekwisha
 
Mwaka 2010 cdm ilipata kura 2 million, mwaka huu 6 million +. Gia ya angani imeleta kura 4 million + na kashkash kubwa kwa ccm. Kama watu hawaoni hili pamoja na ujumlishaji wa kura usiokuwa na hata chembe ya credibility, basi tumekwisha

Ndugu yangu ukibishana na kiraka wa ccm utajipotezea muda bure achana nao.muda mfupi ujao utawakuta wanalalama kama mbwa mwitu.
 
Wakifanye chama kiwe cha kitaifa zaidi. Viongozi wake watoke pande zote za nchi. Bado kwa sasa haina wapambanaji Wa kukikuza chama Kama akina Dr. Slaa sasa ndo nimejua nini maana ya asset and liabilities
 
ukawa itaimarika zaidi na zaidi idadi kubwa ya wabunge itawafanya wawe imara zaidi na kuongeza ruzuku...cha msingi kupigania katiba mpya ambayo itafanyia marekebisho sheria kandamizi ikiwemo ya tume ya uchaguzi kuwa ndio chombo cha mwisho ktk kuamua mambo ya uchaguzi
 
Back
Top Bottom