Mbowe atikisa gereza la Lema

Mbowe atikisa gereza la Lema

Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.

Hapana Mkuu,ktk hili naona ka achieve, unajua kufikia hatua ya Wakuu wa Polisi DCP Kivuyo, SACP Sirro na ACP Paul kwenda kumwona gerezani c haba, hata huo mkutano (kama utafanyika) utatoa ujumbe sana
 
1. Alisema katika mkutano huo,
Chadema itatoa tamko kuhusu mateso yanayowakumba viongozi, wanachama na wapenzi wa chama hicho mkoani Arusha na sehemu mbalimbali nchini kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliopita.
2. VP KUHUSU MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU USHOGA????. Au ndio tuendelee kuipotezea ????.
 
Chaga Development Manifesto

mtoto wa wazir mkuu wa Uk, chama chenu cha masho ga hakina nafasi tz. Labda tumia dawa za kichina na shaarab ili mfanane na pm Uk,la mwisho masaburi on action
 
Chaga Development Manifesto



Prof Safari, Dr. Kitila, Dr. Slaa, Zitto, Lissu, Shibuda, Arfi, Sugu, Vicent Nyerere, wabunge wa Mbozi mashariki, ukerewe, maswa nao ni wachaga!? Peleka ujinga huko....


.
 
ZIARA ya Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, jana ilitikisa gereza kuu la Arusha huku uongozi ukihaha kuita askari wote waliokuwa mapumziko, kurudi kazini haraka kuimarisha ulinzi.

Mbowe alifika gerezani hapo saa 8.05 mchana kwa lengo la kumjulia hali Mbunge wa Arusha Godbless Lema ambaye mapema wiki hii, alikataa dhamana na kuamua kukaa gerezani kufuatia kuahirishwa kesi yake ya kudaiwa kuchochea maandamano bila kibali mjini humo hivi karibuni.

Katika ziara yake, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni , alimwomba Mbunge Lema kulegeza msimamo wake na kukubali kutoka gerezani kesho Jumatatu ili aweze kwenda Dodoma kuwawakilisha wananchi wake kwenye mkutano wa bunge unaonza kesho kutwa, Novemba 8.
.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuonana na Lema katika mahabusu ya gereza hilo lililopo eneo la Kisongo, Mbowe alisema amechukua hatua hiyo ili kumwezesha mbunge huyo kuhudhuria vikao vya bunge na kutumia nafasi hiyo kuueleza umma na jamii ya kimataifa adha anazokumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yake.

“Nimemwagiza atoke Jumatatu, tutakwenda pale mahakamani kumwekea dhamana na tutatoka naye pale hadi Viwanja vya NMC ambako atazungumza na wananchi wake kuwaeleza kilichotokea hadi kuchukua uamuzi wa kijasiri kwenda mahabusu,” alisema Mbowe.

Alisema hawakusudii kufanya maandamano na kuliomba Jeshi la Polisi kutotafsiri mapokezi ya mbunge huyo kutoka mahakamani hadi NMC kama maandamano huku akionya kwamba wasithubutu kuingilia mipangilio hiyo, kwani Lema kama mbunge, ana haki ya kuzungumza na wapigakura wake.

“Tumechagua Jumatatu kwa sababu ya kupisha
ujio wa ugeni mkubwa wa mwana Malkia wa Uingireza, Prince Charles unaotarajiwa kuanza hapa Novemba 9, mwaka huu na polisi wasithubutu kuingilia mipango hii, kwani inaweza kuvuruga hata makubaliano ya msingi tuliyofikiana nao kuhusu ugeni huo,” alionya Mbowe

Alisema kama polisi wanadhani wanaweza kuingilia mapokezi hayo na mkutano wao wa hadhara na Arusha ibaki salama, basi wajaribu.

Alifafanua kuwa awali walipanga kuanza mikutano ya hadhara mjini Arusha kwa siku saba mfululizo kuanzia kesho kutwa na tayari waliwasilisha taarifa kwa Kamanda wa Polisi Wilaya (OCD), Zuberi Mwombeji, lakini baada ya majadiliano na uongozi wa jeshi hilo,walikubaliana kuahirisha kupisha
ugeni wa Prince Charles.

Mbowe alisema majadiliano na makubaliano ya kuahirisha mikutano hiyo yalifikiwa kati yao na OCD pamoja na Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa na akasisitiza kuwa utekelezaji utategemea ushirikiano wa jeshi hilo wakati wa mapokezi ya Lema na mkutano wa hadhara wa kesho.

Alisema katika mkutano huo, Chadema itatoa tamko kuhusu mateso yanayowakumba viongozi, wanachama na wapenzi wa chama hicho mkoani Arusha na sehemu mbalimbali nchini kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliopita.

Alisema kitendo cha Mbunge Lema kukubali kwenda gerezani kwa hiari kina ujumbe maalumu kwa dola inayotumia vitisho vya kubambikia wana mageuzi kesi na kuwafunga jela.

Wakati Mbowe akiingia gerezani hapo jana na msafara wa magari zaidi ya 12 na pikipiki kadhaa zilizopambwa bendera ya chadema, ulinzi uliimarishwa huku askari waliokuwa na silaha wakionekana kutanda kila kona. Mara baada ya kuwasili alilakiwa na uongozi wa gereza hilo.

Katika hatua nyingine, ujumbe mzito wa Jeshi la polisi ukiwa na makamishina wawili kutoka Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam jana ulimtembelea Mbunge Lema gerezani kuzungumza naye na kuwasilisha ombi maalumu ya kumtaka akubali kutoka mahabusu ili kurejesha amani na utulivu mjini Arusha.

Kwa mujibu wa Mbowe, Makamishina waliomtembelea Lema jana ni Peter Kivuyo, Simon Siro na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Leonard Paul
.
source mwananchi jumapili leo

Nadhani ni wazo zuri kabisa. Huyo dogo kwenye red anafuata nini hapa!!
 
1. Alisema katika mkutano huo,
2. VP KUHUSU MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU USHOGA????. Au ndio tuendelee kuipotezea ????.



Tunamzigo mzito wa kulikomboa hili taifa. Cdm hawana muda wa kuzungumzia upuuzi kama huo. Hayo ni mambo yanayojadiliwa na watu wasiokuwa na kazi. Kama unasubiri tamko linalotetea ushoga wako, kalisubiri nccr kwa Mbatia!
 
haki ya mtu haipotei kamwe,lazima makamishina wamuombe,Ni viongozi wawili tu waliokubali kwena gerezani kwa hiari yao wenyewe ili waweze kuwakilisha mawazo na kilio cha wananchi.unapomtisha mtu utafunga ni bora aende mwenyewe huko huko unapomtishia kumpeleka,sasa basi wana wa magamba jitahidini kuandaa plan b ana paln a imekwama.Alut continua mapambano nddo kwanza yameshika kasi
 
Serikali ya vibaka imeshikwa pabaya kudadadek! Mpaka wameamua kuwatumia makamanda wa polisi kubembeleza wameona hali ya Arusha na Tanzania nzima ni tete! Kesho ujumbe mzito kwa IGP pale NMC ni kumwajibisha yule mpumbavu aliyetuita PANYA! Dalili za Ukombozi zimeshaanza kuonekana! God bless Kamanda Lema!
 
hajatishiwa mtu nyau. Msg sent. Zuberi alitumia masaburi kutenda kazi yake sasa linamgarimu tena sana na baya zaidi kesho ndio anaaibika kabisa kama ahamini ajaribu kugusa raia. watu sasa wamechika. nafikiri hata mimi nitaudhuria NMC nimeshalonga na boss wangu keshi nina dharura

Karibu NMC kesho mkuu. Mie nina ED ya leo na kesho.
 
Hawa Polisi wananishangaza sana na ninajiuliza ni kwa nini wanashindwa kufanya kazi kama polisi wa raia wote. Polisi wanajiweka kutetea upande mmoja na kuonea vidagaa kwa vile Chadema hawana jeshi, kwa ajili ya kutekeleza maagizo ya viongozi wao wanaopenda kupandishea vyeo. Kuna siku hii hali itashindwa kuvumilika mapanga yatanolewa nondo zitakatwa vipande kwa ajili ya utendaji wao polisi wa kipumbavu.

Tanzania ni yetu wote kwa nini Mh Lema amefikia hatua ya kunusuru maisha yake gerezani inamaana hapo pana kitu lazima kichimbuliwe kijulikane. Watu wa Arusha wamepiga makelele weee jinsi polisi inavyowanyanyasa lakini hii serikali ya kibepari inachukulia mzaha tu. Lakini polisi imekuwa kikwazo kwa hawa wananchi wa Arusha lazima serikali ielewe imwache chaguo la Arusha lifanye kazi, wananchi wakichoka si kuna kura za kumtoa.

Ninajiuliza hawa polisi wanaweza kumtoa Mh Lema kwenye ubunge sasa hata wakimfunga akigombea akiwa gerezani, wananchi wakiamua watampa kura tu. Hapa polisi ifanye kazi yake kama polisi na Siasa ifanye kazi kama siasa.

Na wale wanaombeza Mh Lema ni wanafiki, wazandiki, wenye wivu wa maendeleo, wabinafsi nk. Lazima tumsifu Mh Lema amefanya kitu cha historia na ni mtu ambaye ameamua kujitoa katika maisha yake kwa ajili ya watanzania sio Arusha tu. Unyama wa hawa polisi na mahakama sasa hivi wanatupeleka dunia nyingine ya mapambani sio ya maendeleo.

Msg ya Mh Lema inaujumbe ambao polisi na serikali lazima ijiulize mara mbili. Mfano sasa watanzania wote wameamua kwenda gerezani wote kwa ajili ya huu unyanyasaji polisi watasema wanavamia vituo vya polisi wakati majambazi yanavamia karibu na kituo askari lakini maaskari wanakimbia wanawaacha majambazi wafanye kazi yao. Polisi wanakazi zao za kufanya sio kila kukicha kupambana na wanasiasa. Kunapokuwa na maandamano au mikutano polisi ihakikishe sheria zimefuatwa na sio kuwa nyima vibali. Kama kutakuwa na Iteligenzia ni vizuri kutoa tahadhari kwa sababu walinzi ni raia na polisi wanaokuwepo katika eneo husika sio kukamata kamata watu kama kuku.

Polisi ijigengee kutoa huduma sehemu hata ya tukio sio lazima kituoni. Kuna mambo mengine hayastahili kupelekwa kituoni, mtu anaweza kukanyaga mtu bahati mbaya lakini kutokana na tofauti za siasa wanachoma mafuta kumpeleka kituoni. Polisi fanyeni kazi yenu kwa amani sio kwa ajili ya kumtetea mtu ambaye wananchi hawampendi. Ni kama baba akichukiwa na watoto nyumbani hata mama asuluhishe vipi watoto bado ule ubaya hautawatoka hata wakikua na wataendelea kumkimbia tu.
 
CCM hivi hamjui kwamba mnavyoendelea kuzuia mikutano yetu kwa kisingizo cha al-shababy na kuwabambikizia kesi za kipuuzi wapinzani, ndivyo mnavyotupa umaarufu mara mbili? Na ndivyo mnavyowazidishia hasira wananchi kwa serikali yenu? Kwa MwanaCCM yoyote mwenye akili anajua kuwa siku zenu zinahesabika, watu uraiani tuna hasira sana.

Waraka wa lema, Naamini unabeba kile kilicho moyoni kwake. Ninaamini jamii ina KIU ya Kutekelezewa kile alichooadika na Kuuamini. Ule waraka usomwe vizuri na serekali na igundue kuwa HAKUNA CHA KUUZUIA USITEKELEZWE .. na Kujaribu kuupigia dana dana .. NI KUONGEZA UMAARUFU kwa upande wasiotaka.

ngoja tuone kama watazuia huo mkutano kwa kisingizio cha allshababu

Ni vema serekali na wanaopinga mahitaji ya Jamii kama yalivyoaninishwa kwenye waraka wa Lema ... wawe makini ... Wakitaka watumie Historia wajaribu kugundua ... Nguvu ya serekali yeyote inaweza vipi kuzuia KIU ya jamii Kutaka Uadilifu na Haki kwenye nyanja kuu za kijamii, kiuchumi, kisiasa na ustawi kwa Ujumla.

Jk na wafuasi wako ujue kuwatenda wapinzani sio kigezo kwamba madarakani hamtaondolewa kuondolewa itabaki palepale na zaidi mnazidi kuwapa umaarufu

BUSARA zote zinaonyesha kuwa, Hakuna haja ya kuleta upinzani pale mtu au kikundi cha watu kweye jamii kinapopigania UTU na HESHIMA zake kwani HIZO ni nguvu kubwa sana kwenye jamii zisizo pingika ..kirahisi. Serekali ingibidi Itumie Busara na Hekima zote kuhakikisha kuwa Jambo hili linawezeshwa na kufanyika salama ...SIO KUWEKA VIZINGITI!!

I thiought Kivuyo anapenda kuwaona wapinzani wametoweka huku nje wawafungie wote so anaenda kufanya nini ? RCO yeye si yuko Arusha na ukweli anaujua kuna shida gani hadi aende gerezani kusema na Lema huko ?Mpwapwa si kasema Lema ana kesi na OCD wake anachunguzwa why tena mhalifu kama walivyo muita Mnaenda kuomba atoke ? Tangia wahalifu wakaombwa kutoka gerezani ? CCM haya mnayo yafanya mnajitakia shida baadaye .

Mkuu Lunyungu, You made a fantastic observation Sir!

Tuliiomba sana serekali watume watu waende gerezani ...waka..RECONCILE.. au wakayamalize na Lema Kwani Kile anachodai Lema though kinaweza kuonekana kama mtu atakavyotaka kukiona.. KINA MSINGI. Hata kama sio Lema atakaye kitekeleza na kukifanyia kazi lakini ..kiukweli kabisa Kwa zama tulizonazo ...TANZANIA UTU NA UBINADAMU kama msingi wa Utendaji kazi, kama sehemu ya Uongozi nk viko chini. Na Sio Lema, Yeyote akaanzisha VUGU VUGU la kuviamsha anaweza kupata wafuasi na watu wa ku m support!

Tukasema Serekali iachane kukimbizana na Lema kama wanafikiri Yeye hana hadhi ya kujenga VUVU VUGU HILO ... Na Serekali ichukue jukumu Hilo!

Tunafikiri sasa Serekali imesikia ushauri, Imekwenda kufanya maongezi ya kuyamaliza ... Na ... BILA SHAKA ... TUTAONA .. YOTE YALIYOANDKWA KWENYE WARAKA WA Hon G LEMA ... yakitekelezwa!

Kwani ni hakika ...UTU NA UBINAADAMU .. Inafika wakati ukadidimia ...na kupotea kabisa ..lakini Mtu makini akiliona hilo na kulifanyia timing ...anaweza kuanzisha vuguvugu lisilopongika .. atakuwa Lema? Tusibiri tuone!!

Lakini CCM na Serekali iliyoko madarakani ...Wanaeweza kuchukua jukumu hilo.. Na kufanya G LEMA kukosa cha kufanya na kumalizikiwa na NGUVU NA UMAARUFU!!

Time is due for this people to surrender,no where to escape.tatizo they never think twice.zaidi they never learn from the mistakes they keep on doing several mistakes.

Josephine ..? You have a great vision Dear!!! ... As far as am concerned ? ...You Just hit the point!!

Its not about G Lema neither CDM ... Its about human dignity, nobility and all about community Credibility .. THESE are Fundamental forces making the sound community ... You can not just come and stop them by whatever means...GUNS and Ammunition ...Stops..The fundamental forces of human and community development? ... A Big Joke..!!!

Ni Jukumu la serakali kusimamia kuwa ustawi wa Utu na Ubindamu unakuwa na kukomaa sambamba na maendeleao ya Vitu na mazingira ya jamii. Ustawi huu hauzuiliki kwa nguvu za Sillaha, Mabomu au Ubabe. NGUVU YA UTU... Inaweza kuzima mabomu yote ya NUKLIA duniani kwa sekunde moja.. Itakuwa risasi na maji ya washwasha...? Hata hivyo busara kidogo tu ... kama ambavyo imesha anza kutumika .. Itamaliza hili tatizo ... IHakikishe ..nadni ya Jamii KUNA KUHESHIMIANA, UPENDO, MATUMAINI NA HAKI ZA BINADAMU, hilo likifanyika ....utashangaa ... Dunia haihitaji ..MIJISILAHA na Makundi makubwa ya wanajeshi wamezagaa kila mahali!! ... Kasomeni tena ule ujumbe wa G Lema .. Unalilia hayo ...Msiupuuziee!! Ukilipuka bila kusimamiwa vizuri ... hakuna mtu atakaye taka kuona kitakacho tokea ..Na Kitajutiwa!!

Lema ni kiongozi shujaa mwenye ujasiri wa ukombozi wa mtanzania,tunamsubiri kesho kwa hamu,CCM inaangamiza maisha ya watu kila siku dola ipo juu,vyakula vimepanda,ajira hakuna now days na kama ikitokea wanapeana wao na watoto wao licha ya kuwa vilaza this is not fair at all,if this is not my I country could leave,but I have to fight till the end,and the freedom is coming.

Kwa ukweli kabisa . Mtanzania anahitaji ukombozi wa aina fulani... Sijui G Lema ametoa wapi yale Matamshi kwenye waraka wake na ana mpango gani kweli na kile alicho andika pale ... lakini ..Ule ujumbe ukiachiwa ukawafikia watanzania wakaamua kuutekeleza ... Unaweza kuanzisha vuguvugu ... ambalo Bora lisimamiwe Kwa Busara!!

Lema awe makini sana sana ndani miaka hii 3 maana ameshakuwa target kama Mwakyembe kama wamemkosa huko selo na kale ka sumu basi akae macho!!!!

Dhana aliyonayo MOYONI na hatimaye kuiweka HADHARANI kama Ujumbe kwenye waraka wake ... Ni mshale wa machungu kwa Mpinga Utu na Mpinga haki za Binadamu yeyote. LAKINI.. Fuatia historia ya ustawi na maendeleo ya jamii Kokote duniani. Kama vuguvugu likianza ... Hata wale viongozi wakiondoka kwa namna yeote .. Hakibadiliki Kitu!! Ni Matumaini Watanzania wana hekima na Busara ya kutosha kusimamia jambo hili liende vizuri.

Ukitaka kujua uwezo wa mtu kiakili mwache aongee. nadhani maneno yako yanaashiria uwezo wako wa kufikiri. Naomba waJF wakusamehe kwa kuwa hujui ulisemalo na wasikuhukumu.

Chieth na kuelewa!

Kuna watu wamesoma na wana digirii zote tatu ... na wakaanza tena nyanja nyingine...wakapata digirii tatu ...jumla sita! Unajua nini?? Wakifika nyumbani ... WANA KULA CHAKULA CHA WATOTO NA WANAKUWA WA KWANZA KUINGIA KITANDANI KULALA!!

Utasema hawajasoma hao? Wamesoma, Shule wamepandisha ... Lakini UTU? SUFURI KABISA... UBINADAMU...? 0% Wanakula chakula cha watoto... AIBU !! Na nikweli ukitaka kuwaelewa vizuri waache waongeee na kuangalia VITENDO vyao...na Tabia zao!

Wasomi hao? Wape kazi ya kuweka mikataba... watakula chakula cha watoto ...kivipi unajua ...anahongwa..ka GX ... anaingia mkataba feki wa mamilioni ya faida kwa mwekezaji kwa miaka mia.. siunaona. Shule ..Kasoma madigirii yote..Lakini kweli ANA UTU NA UBINADAMU Huyo? Yeye kashiba na familia yake lakini jamii nzima ya Kitanzania inakufa njaa ya kila aina. AKILI MINGI lakini UTU NA UBINDAMU 0%. Hawa viogozi hawapooo? Hatutamaliza Kuonyesha udhaifu huu kwa jamii ya Tanznaia kwa Sasa. Ni kweli kabisa UTU na UBINADAMU uko chini sana na hilo halipingiki. Ndio Maana Taka tusitake ..VuguVugu lina kuja...Tunahijati Serekali ilisimamie liwe na AMANI na UTULIVU ... ni VuguVugu la Kurejesha UTU NA UBINADAMU ..soma waraka wa G Lema!!

Hata kama G Lema asingejitokeza kuanzisha vugu vugu hilo ... hakuna namna kwa vyovyote lisingekuja hasa ukitilia maanani kuwa SHINA LA UASISI WA TAIFA HILI NI UTU KUTAWALA KILA NYANJA YA KIJAMII. UTANZANIA NI UTU, UTU hauna DINI, UTU hauna Makabila, UTU hauna ITIKADI, UTU hauna JINSIA, UTU hauna MATABAKA, UTU hauna RANGI ...UTU ni UTANZANIA!!

Sioni ni kwanini CCM na Serekali isichukue jukumu la Kundesha Vuvu Vugu Hili!!!
 


JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA
UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.


Wapendwa wapiga kura wangu na Watanzania wenzangu.

Sina wakati mgumu kuchukua maamuzi haya yanayotokea leo. Upendo huu nilio nao kwa watu wa Arusha na nchi yangu ni sababu ya msingi ya maamuzi haya. Nimetishwa mara nyingi, rafiki zangu wametishwa, jamii ya watu duni imeendelea kuishi kwa
mashaka na matisho kwa muda mrefu.

Katika mazingira haya, nikawaza sana kuwa anatakiwa kutokea mtu mmoja jasiri atakayeweza kuona thamani ya watu wengine. Huyo mtu anaweza kuwa wewe lakini kwa wakati huu siwezi kumsubiri tena na nimechagua kuwa mimi nikiamini kuwa utanikuta nikiendelea na safari ya ukombozi. Tupo wengi sana tunaotaka mabadiliko, haki na ukweli. Hata hivyo hofu, woga na mashaka yamepoteza thamani yetu yote ya maana ya kuishi .

Waliofungwa kwa kuonewa na kuteswa, waliokosa chakula na kulala nje, waliokwenda hospitali na kukosa madawa, waliokosa ajira na kipato mpaka kujikuta wametoroka familia zao, waliopoteza matumaini ya maisha, waliopora utajiri wa nchi yetu kwa
manufaa yao binafsi, walionunua haki na sheria dhidi ya wajane na wanyonge na kuwapora vipato vyao vidogo na mashamba yao, USIULIZE SABABU NINI!.

Nimetafakari sana na nikatambua kuwa sababu ni mimi pale nilipokuwa kimya wakati wajane na wanyonge wanaonewa.

NIliposikia wengine wanaandamana kupinga uovu, uonevu, wizi, ufisadi na ukandamizaji wa haki nikasema ni hao na wala sio mimi, kumbe nilipaswa kuwa mbele katika harakati hizi.

Nilipoona wenzangu hawawezi kupata matibabu nikasema mimi sio mgonjwa, nilipopata taarifa za rafiki zangu kufungwa kwa makosa yasiyo yao, nilipoona watoto wa mitaani wanaomba chakula, nilipoona wazee wamepoteza matumaini ya kuishi katika uzee wao, nilipoona vijana hawana ajira, nilipoona mabinti wasichana wadogo wameamua kufanya biashara ya ukahaba, NIKATAFAKARI,TENA NIKATAFAKARI, dhahabu zetu, almasi yetu, Milima na mabonde yetu, Tanzaninte yetu, samaki wetu, Uranium yetu, makaa ya mawe yetu, utalii wetu, ardhi na kilimo chetu na zaidi utu na mahusiano yetu.

Na sasa siwezi kukaa kimya tena. NI afadhali vita inayotafuta haki na usawa kuliko amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa mwanadamu. Na katika msingi huu hofu na mashaka vimekosa thamani kwangu, sitamwogopa mtu yoyote, mwenye silaha yoyote, mwenye cheo chochote na wala sitaogopa jela yoyote katika kupigania haki, utu wa kweli katika jamii yangu. Wanafikiri wataendelea kutuogopesha kwa sababu wana jela na silaha, wanafikiri tutaendelea kuabudu uoga, wanafikiri wataendela kutunyanyasa bila sababu ya msingi LAKINI SISI TUNAJUA TUTASHINDA KWA SABABU HAKI TUNAYOIPIGANIA NI MAKUSUDI YA MWENYEZI MUNGU.

Leo nitakwenda jela kwa hiari yangu binafsi kwa siku kadhaa na si kwa NIA YA KUJITAFUTIA UTUKUFU WANGU bali ," JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.

Kila mara nilipotishiwa nikagundua wanaonitishia, wananitishia kwa jela na mauti. Na mimi nikagundua na nikatambua ni afadhali kuishi miaka hamsini jela huku sababu ikiwa ni kupinga uonevu na ukandamizaji kuliko maisha ya woga na anasa yasiyo na kusudi katika kutetea utu na heshima ya mwanadamu mwenzangu.

Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu. Watakaotubeza na kututukana wasameheni kwani wanahitaji ukombozi wa fikra,
watakaotupongeza na kutuonea huruma wafundisheni ujasiri na waambieni mapambano bado yanaendelea tunahitaji umoja wao. Nitarudi mapema. MSIOGOPE, MSIOGOPE, MSIOGOPE , MUNGU YUPO UPANDE WETU.

Mhe Godbless Lema (MB) – Arusha Mjini
31 Oktoba 2011.

 
Back
Top Bottom