msafwa93
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 4,840
- 6,141
Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
kaumbuka nini sasa.?
Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
2. VP KUHUSU MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU USHOGA????. Au ndio tuendelee kuipotezea ????.Chadema itatoa tamko kuhusu mateso yanayowakumba viongozi, wanachama na wapenzi wa chama hicho mkoani Arusha na sehemu mbalimbali nchini kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliopita.
Chaga Development Manifesto
Alipiga,alipigia Ccm,ila 2015,hatarudia kosa,hata kupiga kura haukupiga
Chaga Development Manifesto
Ushoga kawaulize CCM ndio sera yao.1. Alisema katika mkutano huo,
2. VP KUHUSU MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU USHOGA????. Au ndio tuendelee kuipotezea ????.
Kilichomuumbua hapo nini?Peter Kivuyo,Simon Siro na Leonard Paul walienda kufanya nini Kisongo?Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
ZIARA ya Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, jana ilitikisa gereza kuu la Arusha huku uongozi ukihaha kuita askari wote waliokuwa mapumziko, kurudi kazini haraka kuimarisha ulinzi.
Mbowe alifika gerezani hapo saa 8.05 mchana kwa lengo la kumjulia hali Mbunge wa Arusha Godbless Lema ambaye mapema wiki hii, alikataa dhamana na kuamua kukaa gerezani kufuatia kuahirishwa kesi yake ya kudaiwa kuchochea maandamano bila kibali mjini humo hivi karibuni.
Katika ziara yake, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni , alimwomba Mbunge Lema kulegeza msimamo wake na kukubali kutoka gerezani kesho Jumatatu ili aweze kwenda Dodoma kuwawakilisha wananchi wake kwenye mkutano wa bunge unaonza kesho kutwa, Novemba 8.
.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuonana na Lema katika mahabusu ya gereza hilo lililopo eneo la Kisongo, Mbowe alisema amechukua hatua hiyo ili kumwezesha mbunge huyo kuhudhuria vikao vya bunge na kutumia nafasi hiyo kuueleza umma na jamii ya kimataifa adha anazokumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yake.
Nimemwagiza atoke Jumatatu, tutakwenda pale mahakamani kumwekea dhamana na tutatoka naye pale hadi Viwanja vya NMC ambako atazungumza na wananchi wake kuwaeleza kilichotokea hadi kuchukua uamuzi wa kijasiri kwenda mahabusu, alisema Mbowe.
Alisema hawakusudii kufanya maandamano na kuliomba Jeshi la Polisi kutotafsiri mapokezi ya mbunge huyo kutoka mahakamani hadi NMC kama maandamano huku akionya kwamba wasithubutu kuingilia mipangilio hiyo, kwani Lema kama mbunge, ana haki ya kuzungumza na wapigakura wake.
Tumechagua Jumatatu kwa sababu ya kupisha ujio wa ugeni mkubwa wa mwana Malkia wa Uingireza, Prince Charles unaotarajiwa kuanza hapa Novemba 9, mwaka huu na polisi wasithubutu kuingilia mipango hii, kwani inaweza kuvuruga hata makubaliano ya msingi tuliyofikiana nao kuhusu ugeni huo, alionya Mbowe
Alisema kama polisi wanadhani wanaweza kuingilia mapokezi hayo na mkutano wao wa hadhara na Arusha ibaki salama, basi wajaribu.
Alifafanua kuwa awali walipanga kuanza mikutano ya hadhara mjini Arusha kwa siku saba mfululizo kuanzia kesho kutwa na tayari waliwasilisha taarifa kwa Kamanda wa Polisi Wilaya (OCD), Zuberi Mwombeji, lakini baada ya majadiliano na uongozi wa jeshi hilo,walikubaliana kuahirisha kupisha ugeni wa Prince Charles.
Mbowe alisema majadiliano na makubaliano ya kuahirisha mikutano hiyo yalifikiwa kati yao na OCD pamoja na Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa na akasisitiza kuwa utekelezaji utategemea ushirikiano wa jeshi hilo wakati wa mapokezi ya Lema na mkutano wa hadhara wa kesho.
Alisema katika mkutano huo, Chadema itatoa tamko kuhusu mateso yanayowakumba viongozi, wanachama na wapenzi wa chama hicho mkoani Arusha na sehemu mbalimbali nchini kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliopita.
Alisema kitendo cha Mbunge Lema kukubali kwenda gerezani kwa hiari kina ujumbe maalumu kwa dola inayotumia vitisho vya kubambikia wana mageuzi kesi na kuwafunga jela.
Wakati Mbowe akiingia gerezani hapo jana na msafara wa magari zaidi ya 12 na pikipiki kadhaa zilizopambwa bendera ya chadema, ulinzi uliimarishwa huku askari waliokuwa na silaha wakionekana kutanda kila kona. Mara baada ya kuwasili alilakiwa na uongozi wa gereza hilo.
Katika hatua nyingine, ujumbe mzito wa Jeshi la polisi ukiwa na makamishina wawili kutoka Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam jana ulimtembelea Mbunge Lema gerezani kuzungumza naye na kuwasilisha ombi maalumu ya kumtaka akubali kutoka mahabusu ili kurejesha amani na utulivu mjini Arusha.
Kwa mujibu wa Mbowe, Makamishina waliomtembelea Lema jana ni Peter Kivuyo, Simon Siro na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Leonard Paul.
source mwananchi jumapili leo
1. Alisema katika mkutano huo,
2. VP KUHUSU MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU USHOGA????. Au ndio tuendelee kuipotezea ????.
Lema kaumbuka na siasa zake uchwara. Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
hajatishiwa mtu nyau. Msg sent. Zuberi alitumia masaburi kutenda kazi yake sasa linamgarimu tena sana na baya zaidi kesho ndio anaaibika kabisa kama ahamini ajaribu kugusa raia. watu sasa wamechika. nafikiri hata mimi nitaudhuria NMC nimeshalonga na boss wangu keshi nina dharura
Lema kaumbuka na siasa zake uchwara.
Alikuwa anatishishia nyau. Chamtemakuni kakiona.
CCM hivi hamjui kwamba mnavyoendelea kuzuia mikutano yetu kwa kisingizo cha al-shababy na kuwabambikizia kesi za kipuuzi wapinzani, ndivyo mnavyotupa umaarufu mara mbili? Na ndivyo mnavyowazidishia hasira wananchi kwa serikali yenu? Kwa MwanaCCM yoyote mwenye akili anajua kuwa siku zenu zinahesabika, watu uraiani tuna hasira sana.
ngoja tuone kama watazuia huo mkutano kwa kisingizio cha allshababu
Jk na wafuasi wako ujue kuwatenda wapinzani sio kigezo kwamba madarakani hamtaondolewa kuondolewa itabaki palepale na zaidi mnazidi kuwapa umaarufu
I thiought Kivuyo anapenda kuwaona wapinzani wametoweka huku nje wawafungie wote so anaenda kufanya nini ? RCO yeye si yuko Arusha na ukweli anaujua kuna shida gani hadi aende gerezani kusema na Lema huko ?Mpwapwa si kasema Lema ana kesi na OCD wake anachunguzwa why tena mhalifu kama walivyo muita Mnaenda kuomba atoke ? Tangia wahalifu wakaombwa kutoka gerezani ? CCM haya mnayo yafanya mnajitakia shida baadaye .
Time is due for this people to surrender,no where to escape.tatizo they never think twice.zaidi they never learn from the mistakes they keep on doing several mistakes.
Lema ni kiongozi shujaa mwenye ujasiri wa ukombozi wa mtanzania,tunamsubiri kesho kwa hamu,CCM inaangamiza maisha ya watu kila siku dola ipo juu,vyakula vimepanda,ajira hakuna now days na kama ikitokea wanapeana wao na watoto wao licha ya kuwa vilaza this is not fair at all,if this is not my I country could leave,but I have to fight till the end,and the freedom is coming.
Lema awe makini sana sana ndani miaka hii 3 maana ameshakuwa target kama Mwakyembe kama wamemkosa huko selo na kale ka sumu basi akae macho!!!!
Ukitaka kujua uwezo wa mtu kiakili mwache aongee. nadhani maneno yako yanaashiria uwezo wako wa kufikiri. Naomba waJF wakusamehe kwa kuwa hujui ulisemalo na wasikuhukumu.
Nadhani ni wazo zuri kabisa. Huyo dogo kwenye red anafuata nini hapa!!