Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Status
Not open for further replies.
CHADEMA KUITOSA UKAWA

Baada ya mwenendo wa Kampeni kuonekana kuwa mgumu huku kila alichoahidi Lowassa kutotimia mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe aamua kukutana na aliyekuwa katibu wake Dkt. Wilbroad Slaa nchini Marekani.

Taarifa za uhakika ni kuwa Mbowe aliondoka nchini toka juzi na kupokelewa na wanachama wa Chadema tawi la DMV aliposhuka Uwanja wa Kimataifa wa Dulles huko Marekani ambapo Dkt. Slaa alimtangulia muda kidogo.

Taarifa zilizopatikana toka kwa moja ya viongozi wa tawi hilo aliyejulikana kama Kalley Pandukizi amesema ni kweli Mbowe na Slaa tumewapokea na wapo hoteli moja hapa Ohio kwa ajili ya mazungumzo binafsi. Amekiri baada ya kumpokea Mwenyekiti wao Mh. Mbowe walimpeleka moja kwa moja hotelini ambapo ndipo walipomkuta Dkt. Slaa.

Tetesi zaidi zinasema Mbowe amemuomba msamaha sana Dkt. Slaa na kumueleza walipotoka kwani mgombea waliomchukua anadhoofika kiafya kila kukicha kiasi kwamba mikutano mingine wananchi hawamsikii anapohutubia vile vile hakuna hata moja alilotimiza katika makubaliano kabla hatujampokea zikiwemo fedha za kampeni hivyo chama kinapata wakati mgumu wa kufanya kampeni kikamilifu.

Inasemekana Mbowe amemueleza Slaa kuwa ujio wa Lowassa umeigharimu Chadema kwani mpaka sasa John Mnyika hajakubali kupanda majukwaani kumnadi Lowassa kitu ambacho ni tabu zaidi kwao. Pamoja na vijana wa Lowassa kuuteka mchakato mzima wa kampeni hali inayokiuka makubaliano tuliyompa.

Kikubwa ni kuwa taarifa za ujumbe mfupi toka kwa Bi. Helen Ongara ambaye ni katibu wa BAWACHA tawi hilo la DMV ni kuwa Mwenyekiti huyo amepoteza tumaini hasa alipowapa video ya Mgombea akiomba kura kwa kigezo cha ulutheri kimewagharimu zaidi hivyo amedai watapigana ili wapate viti vya ubunge ila urais watapoteza.

Hata hivyo aliwadokeza kuwa kampeni zinaratibiwa na Lissu lakini wanafikiria kuchukua maamuzi magumu ya kuwatosa UKAWA ili wabaki wao kama wao kuliko sasa ambapo wanavibeba vyama vya NCCR MAGEUZI, NLD na CUF. Ambapo hata hivyo hali ya mpasuko imeanza kuonekana kupitia vyama vya CUF na NCCR MAGEUZI.

Walisahau Majuto ni mjukuu huja baadae!

1442587065344.jpg
 
Dk. Slaa na Prof. Lipumba hawawezi kumsahau Mbowe kwa kile amewafanyia katika harakati za kisiasa.

Mbowe amewaingiza kwenye mkenge.
 
Moderator kuweni waungwana tetesi za Ukawa juu ya Ccm mnazifuta mara zote.
Na mambo ya tetesi na hisiya JF tushayakataa
Futeni huu upuuzi la sivyo mvumilie tetesi za Ccm zitakazo poromoshwa hapa.

Mkuu nilisikia wale maccm yametenga bilioni 150 hivi zinatumikaje vile!!
 
Last edited by a moderator:
Liambie gamba naona limeukimbia uzi wake baada ya kuona kila anayechangia anamtwanga ngumi za shingo na magamba wenzake wamelala mbele
Juzi kajisaidia kwenye nguo ipo siku atazoma kabisa hii zama siyo ya mafisadi ndugu.
 
Unataka uone mishemishe gani? Kwani wageni wote wanaoingia hapo lazima wakutaarifu?

Ungejibu swali badala ya kutetea ingetusaidia sana .............. Dulles iko Ohio ............. na DMV area ni Ohio.................!!?
 
Juzi kajisaidia kwenye nguo ipo siku atazoma kabisa hii zama siyo ya mafisadi ndugu.

Hata akiwa ni kiwete tumeamua kumchagua tu na ccm na makomeo wenu mpiganie kuongoza kambi rasmi ya upinzani bungeni
 
Moderator kuweni waungwana tetesi za Ukawa juu ya Ccm mnazifuta mara zote.
Na mambo ya tetesi na hisiya JF tushayakataa
Futeni huu upuuzi la sivyo mvumilie tetesi za Ccm zitakazo poromoshwa hapa.

Bora na wewe umeliona hilo, nimesha weka nyuzi kadhaa zikatokewa na hata kuungwa kwenye nyuzi nyingine, ninapata hisia kwamba viongozi wa JF huenda wakawa hawapo huru yani si tofauti sana na star tv. Jambo hili si lakiungwana

Kama inawezekana ni vema wangesema wazi ni nyuzi zipi pendwa kwao ili nasi tuzingatie japo itakua imekiuka uhuru wetu.
JF tusaidieni katika hilo.
 
Last edited by a moderator:
Unajua maana ya kauli hii kijana??? "..a point of no return." maana yake ni kwamba ilipofika ukawa kwa sasa hata ajitoe muasisi wa chadema au nani hakuna kitakachobadilika..........
 
Wataisoma naba ccm mbele kwa mbele.

Hata hujui unacho kiandika masikini baada ya kutojua hatima ya maisha yako,,,,WATAISOMA...NABA....Teeeeeeeh,teeeeeeeh,gamba limedata jamanieeeee
 
Acheni kudanganya watu, Mbowe hana hadhi ya kuwa hata obsever wa kamati ya ulinzi na usalama UN, tatizo lenu mnashabikia pasipojitambua, subilini mtayapata majibu hivi karibuni.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom