Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,153
- 48,396
Freeman Aikaeli Mbowe ni mwanasiasa ambaye huwezi kuzungumzia siasa za Tanzania bila ya kutaja jina lake.
Lakini naona Baada ya uchaguzi wa Januari 21 mwaka 2025, Kuna baadhi ya watu wanapambana kwa kila Hali kuonesha kuwa Mbowe alikuwa mamluki ndani ya CHADEMA na alikitumia chama kwa faida yake.
Mimi nakubaliana na wale wanaosema kuwa baada ya Mbowe kukaa madarakani CHADEMA kwa zaidi ya miaka 20, Kuna mambo alianza kutoyapa umuhimu na umakini wake kwenye kusimamia mambo ya msingi ulipungua.
Lakini ukweli lazima usemwe, CHADEMA hii ya sasa ina mchango mkubwa sana wa juhudi za Mbowe kuifanya iwe imara.
Wengine tunaomfahamu Mbowe tangu mwaka 2004 tunajua ni kwa kiasi gani amepambana kuifanya CHADEMA iwe hivi ilivyo.
Pamoja na mitizamo yetu dhidi yake, lakini tumheshimu yeye kama binadamu na mtu aliyechangia sana uimara wa CHADEMA hii ambayo sote ni wafuasi wake!
Kama tunaona Mbowe hakuna jema alilolifanya ndani ya CHADEMA, Iko siku na Lissu naye tutamdharau hivi hivi tunavyomdharau Mbowe.
Tukubaliane tu kwamba ni watu wachache sana waliopambana kama Mbowe ndani ya CHADEMA wakati akiwa kiongozi. Mbowe apewe heshima yake!
Lakini naona Baada ya uchaguzi wa Januari 21 mwaka 2025, Kuna baadhi ya watu wanapambana kwa kila Hali kuonesha kuwa Mbowe alikuwa mamluki ndani ya CHADEMA na alikitumia chama kwa faida yake.
Mimi nakubaliana na wale wanaosema kuwa baada ya Mbowe kukaa madarakani CHADEMA kwa zaidi ya miaka 20, Kuna mambo alianza kutoyapa umuhimu na umakini wake kwenye kusimamia mambo ya msingi ulipungua.
Lakini ukweli lazima usemwe, CHADEMA hii ya sasa ina mchango mkubwa sana wa juhudi za Mbowe kuifanya iwe imara.
Wengine tunaomfahamu Mbowe tangu mwaka 2004 tunajua ni kwa kiasi gani amepambana kuifanya CHADEMA iwe hivi ilivyo.
Pamoja na mitizamo yetu dhidi yake, lakini tumheshimu yeye kama binadamu na mtu aliyechangia sana uimara wa CHADEMA hii ambayo sote ni wafuasi wake!
Kama tunaona Mbowe hakuna jema alilolifanya ndani ya CHADEMA, Iko siku na Lissu naye tutamdharau hivi hivi tunavyomdharau Mbowe.
Tukubaliane tu kwamba ni watu wachache sana waliopambana kama Mbowe ndani ya CHADEMA wakati akiwa kiongozi. Mbowe apewe heshima yake!