Mbowe anusurika kifo mara tatu

Mbowe anusurika kifo mara tatu

ukweli unauma sana kasema ukweli kuwa amenusurika kufa nani anayejiombea kufa? kifo kinaogopwa na wengi sana ila anaposema amekiona ila Mungu kamusuru Uccm wekeni pembeni jamani huyu ni JEMBE na kiongozi wa ukweli mkubali mkatae
 
Wakiuwawa 100 watasimama 1000, wakiuwawa 1000 watasimama 10000.

Viva Chadema.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Baada ya kunusurika mara tatu amini usiamini sasa utakufa kifo cha kawaida tu. Hakuna atakayekuua mheshimiwa endeleza harakati za ukombozi wa mtanganyika ila nakushauri uache kabisa kutishia kususia uchaguzi wa 2015 iwapo daftari jipya la wapiga kura halitaandaliwa na watu kujiandikisha. Uchaguzi lazima tushiriki na tutashinda cha msingi hapa ni kuwa kama serikali itakataa kuandaa daftari jipya la wapiga kura, basi nakushauri uitishe maandamano ya nchi nzima kuhimiza daftari hilo kuwa tayari kabla ya 2015. Hapo ndo patamu kwa hii serikali dhalimu...hiyo ndo dawa yao... peoplesssss powerrrrrr tu
 
Huwa ninazikubali busara na hekima za Mh. Mbowe ukilinganisha na uwezo wake kielimu kwa mazingira ya siasa za Tanzania.

He has no political and personal revenge and vendetta mentality ukilinganisha na viongozi wengine wa vyama vya siasa na hasa CHADEMA. He has what it takes to be politician in unpredictable Tanzania political environment.

Ninaamini kama asingekuwa kati kati ya mgogoro wa Katibu Mkuu na Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA kwa sasa ugonvi, mikwaruzano na majivuno kati yao ingekuwa full blow-up lakini kwa busara na hekima zake, he can suck their venom, hate and revenge between them and take the edge off. He can shuffle either side of their clique to defuse tension and keep them going. Ndiyo maana kwenye mikutano either utamkuta yuko na Mh. Zitto bila Dr. Slaa au utamkuta na Dr.Slaa bila Mh. Zitto.

He's a buffer zone between CHADEMA and government pamoja na baadhi ya watu na wanasiasa kutaka kwa nguvu zote awe hate and bitter politician towards government. Ninafikili elimu aliyoipata kupitia kwenye majukwaa ya biashara bila kwenda darasani imempa uzoefu na kutambua kuwa hakuna business competitor wa kudumu wala customer wa kudumu kwa maana kuwa hakuna adui wa kisiasa wa kudumu na asiye adui wa kisiasa wa kudumu hasa kwenye unpredictable political environment.

Huyu ni binadamu kama walivyo binadamu wengine ambao moja ya jambo linaoufanya ubinadamu wao ni kuwa na mapungufu. Mojawapo ni hili la kupaza sauti kuhusiana na kifo chake.

Mh.Mbowe akiwa ni kiongozi wa kitaifa anatakiwa kuchunga sana maneno yake katika kandamnasi kwa sababu kila neno analolitamka jamii inalisikiliza na kulisoma kwa macho matatu.He'can't afford to stoke fear among Tanzanian kwa faida ya muda mfupi kisiasa.

Kuwa mwanasiasa ni kukaribisha maadui, the last thing you can do is to encourage them and pia kuwaogopesha na kuwavunja moyo wale ambao wako nje ya political bullseye kama maneno yake alivyoyatamka. He has so many political gaffe even though hili ni tatizo la wanasiasa wengi Tanzania.

Mh. Mbowe, keep on learning kwa sababu kila siku ina somo lake.
 
Mkuu, ndani ya CDM, wake za watu ni halali yao. ukiona kiongozi au mfuasi wa CHADEMA, weka mbali mke wako

KIONGOZI hilo nalo neno, kuanzia kwa katibu na sasa m/kiti na Mbunge wa viti maalum Arusha wameoana na sasa bibi huyo yuko Dubai. Angalia mh. wewe kama kioo cha watu unafanya utumbo huo huoni noma. kweli tunaupinzani feki
 
mbowe ni zaidi ya kiongozi ndani ya chadema....viatu vyake vime mtosha..Glory glory Chadema.
kilichosaidia CDM kufika hapa ilipo ni kushindikana kuwafarakanisha hawa viongozi wakuu wa CDM, kwa kutumia mbinu mbalimbali zikiwemo
a) Vitina
b) Fedha
c) Mbinu za kiujasusi

Mkumbuke NCCR ilikufa kwa sababu tu ya Fitna na fedha, kuna watu hapa wamesomea kufitinisha watu. CUF nayo enzi za ngangari ilikuwa ngangari kweli kweli, leo hii ndugu zangu kiko wapi? Mwenyekiti haileweki, katibu mkuu tayari ana cheo kikubwa cha utawala Zanzibar, sasa CUF ipo njia panda, Chama tawala Zanzibar, Chama cha Upinzani Tanzania bara. ( Hii pia ni mbinu ya kisayansi ya kuimaliza)

Kwa hiyo ndugu zangu, CDM imefika hapo ilipo kwa ukakamavu, ukomavu, weredi, uthubutu wa viongozi wake wakuu hasa hii combination ya Mbowe na Slaa ambayo wale wapenzi wa soka basi wanaifananisha na ile tunayoisubiri mwaka huu kati ya Neymar na Messi pale Barcelona.

Mungu Ibariki CDM, Mungu wabariki hawa viongozi tuimalize hii kazi ndogo iliyobakia.
 
Kama hujui kitu ni heri kunyamaza kuliko kuropoka ovyo ingawa ni sahihi pia kusema kuwa 'mwenda wazimu naye huwa hajui kwamba ubongo wake una matatizo'. Hivi wewe Nambalapala, una hakika gani kuwa Mheshimiwa Mbowe ndiye aliyemuua Chacha Wangwe? Usilolijua ni usiku wa giza, wakurya wanajua vizuri sana walioratibu hayo mauaji na ndo maana Mbowe akikanyaga Tarime anapokelewa kama mfalme. Muulize Makamba senior kilichomfanya akimbie tarime saa nane usiku ni nini?
 
afe tuuuu, kwani ye nani??? wamekufa watu wa maana sembuse mjasiriamali wa siasa bana

utakufa wewe na uzao wako bali Mbowe ataishi hata aine kaz ya mikono yake pale nchi itakaporud mikononi mwa wana nchi na utawala wa sheria kutamalaki,enyi wadhalimu tubun mana ghadhabu ya Mungu ii karibu kuwafutilia mbali,ole wenu.
 
Pompo, wala usimtetee Mbowe. yeye alimuua CHACHA WANGWE, na yeye ipo siku atakufa tu. iwe kwa ajali au kuumwa

kama una ushahdi kwann usepeleke mahakaman ili sheria ichukua mkondo wake?hv nchi hii haina polisi na mahakama?mbona nyie maccm mna roho za kishetani hv kwann mauaj mfanye nyie then msingzie wapinzan??ole wenu cku inakuja mtalia na kusaga meno
 
sasa Mbowe anadanganya watu ili aonewe huruma? yeye kama amenusurika kufa Ponda naye atasemaje?
Mbowe kasema kinachomhusu na Ponda nae atasema kinachomhusu,kwani umeambiwa Mbowe ndo msemaji wa Ponda?
 
wananchi hawalazimishwi kuchangia hizo miamia bali ni kwa mapenzi yao tu kwa chadema na kwa kutambua kuwa ukombozi ni gharama. Hata Mwalimu Nyerere wakati anautafuta ukombozi dhidi ya mabeberu alichangiwa pesa na wananchi akiwemo mzee mbowe (baba yake freeman) ambaye alikuwa akimchangia mwalimu nyerere nauli ya ndege kwenda umoja wa mataifa kudai uhuru. Hivyo cha ajabu ni nini wakati huu tunapotafuta ukombozi kutoka kwa mafisadi na vita hivi ni vigumu mno kuliko vita vya kujikomboa kutoka kwa mabeberu kwani mabeberu walikuwa wahamiaji tu lakini mafisadi ni watanzania wenzetu ambao wamejimilikisha hii nchi pamoja na rasilimali zote na kuwafanya watanzania wenzao kuwa ni wahamiaji. Ndo maana tumefika mahali ambapo sasa wananchi hawachangii mia mia tu bali wanachangia mpaka damu kutokana na vifo vinavyoratibiwa na hao mafisadi.
 
Abarikiwe sana Mwenyekiti Mbowe... Ingawa anaongoza mapambano ya CDM kuingia ikulu, lakini ni wazi kwamba ameongoza vyema harakati za upinzani nchini. Hata kama CDM haitaingia ikulu, au hata kama yeye hatashuhudia ikiingia ikulu, lakini historia itabaki kuwa alikuwa mmoja wapo wa viongozi mahiri wa upinzani aliyewahi kutokea Tanzania hadi sasa...
Nchi inakuwa na raisi mmoja tu kwa wakati mmoja, lakini inakuwa na viongozi wa vyama vya upinzani kadhaa wakati wowote... Kwa sasa, na kwa historia ya nchi hii, Mbowe ndiye kinara kati ya wenyeviti wa vyama vya upinzani zaidi ya 18. Pamoja na kuwapo na wenye elimu kubwa sana zaidi yake, Mbowe amewapiku wote na kudhihirisha kipaji kikubwa cha kuongoza alicho nacho.

Namuombea maisha marefu na afya njema, ili siku moja apate nafasi ya kushuhudia kwa macho yake mabadiliko yale ambayo amekuwa akitapigania.

Viva Mwenyekiti wa ukweli...

Umenena vema Mkuu, nafikiri sifa za Mboye ni nyingi mno kiasi huwez kuandika moja baada ya ingine! Mbowe atabaki kua Kamanda wa Ukweli na kiongozi na mwanasiasa thabiti ndani ya taifa letu! Viva Chadema na keep it up Mbowe Kamanda wa Ukweli!
 
hapo mbowe anataka kumfanyaje mke wa mtu ???
Du mimi ni hii Signature yako tuu
unafanya ziara jimboni kwa helikopta halafu unawachangisha wananchi mia mia zao eti unajenga chama, wizi mtupu!!!!!!!!


yaani BABANGU nakomaGA kabisa kuijua Siasa kumbe ni biashara!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Sasa Africa na hiyo habari hapo juu vinahusianaje?
Siasa za Jembe ne Nyundo ndo hatari, maana hata ile itikadi ya wakulima na wafanyakazi haizungumziwi kabisa siku hizi.
Ni mwendo wa madawa ya kulevya na biashara haramu tu!

Umenikumbusha mbali sn, siasa za jembe na nyundo?!!!!!!!! Alafu sera ya wakulima na wafanyakazi!!!!! Duh, hiyo ilikua Sera ya Mzee Nyerere, alipoenda na hizo sera zikafa kabisa! Ila siku hizi wanasema Eti kilimo Kwanza! na haohao wanapingana katika hiyo sera wengine wanasema Elimu kwanza then kilimo ndo kifate! Sasa hapo tunabaki njia panda Sisi wananchi! Ila ya Jembe na Nyundo na wakulima na wafanyakazi zilikua Kali sana!
 
Huwa napata shida sana nikimfikiria mrithi wa Mbowe

Usipate shida kumfikiria mrithi wa Mbowe kwani misingi ya Chadema imejengeka imara kila kitu! Hakuna makundi ndani ya chama, hakuna udini ndani ya chama, hakuna ukabila wala Ukanda ndani ya chama! Siasa ya Chadema ni safi na ya umoja na kujali maslahi ya wananchi, uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika kila jambo, haki, na kutetea haki za kwa wananchi, usawa wa haki na mengine mengi! Hiyo ndo misingi ya Chadema! Sasa Kama Kiongozi yeyote akimrithi Mbowe na akisomamia misingi ya chama ipasavo chama kitasonga mbele zaidi na Zaidi! Viva Chadema........!
 
Huwa napata shida sana nikimfikiria mrithi wa Mbowe

Wewe angalia ata mfumo wa "intelinjesia" yani usalama ulivo imara ndani ya chama hii inaonyesha kua mfumo wa chama na misingi ya chama iko vizuri! Mara ngapi wanaumbuka na mambo Yao ya kutengeneza? Na Mara ngapi hao mamruki au wanaumbuka?
 
Back
Top Bottom