Mbowe ana hekima sana!

Mbowe ana hekima sana!

Lukolo

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
5,143
Reaction score
3,209
Nimesoma kauli ya Mbowe kama ilivyonukuliwa katika gazeti la Tanzania daima, kwa kweli nimefarijika sana. Na nimejiridhisha kwamba Mbowe ni kiongozi wa ukweli. Maneno haya ya Mbowe, hayawezi kusemwa na kiongozi mwingine yeyote anayeheshimika ndani ya CCM. Wakati Mbowe akitoa kauli yenye hekima ya hali ya juu, kule upande mwingine tungeshuhudia mwenyekiti wake akiongea mipasho. "Za kuambiwa....", "Ukitaka kula ukubali kuliwa" etc. Sasa msome Mbowe hapa: Ndipo ujue kuwa uwingi wa degree za darasani si kipimo cha hekima.


"Sitamuogopa rais, lakini nitamheshimu, sitaogopa polisi lakini nitawaheshimu, sitaogopa Jeshi lakini nitaheshimu Jeshi. "Kuanzia sasa sitamheshimu mtu yeyote asiyeheshimu ubinadamu wa mtu mwingine.

Uchaguzi wa juzi wa kata, tumeshinda kwa mapambano ya damu. Watu wetu wamepigwa kila mahali, wamekatwa mapanga na mashoka na vijana wa CCM, Green Guard. "Katika hali kama hiyo siwezi kucheka na polisi, ndiyo maana juzi tumetangaza kuwapatia vijana wetu mafunzo ya ukakamavu ili tujilinde na vitendo hivi. Hatujaanzisha jeshi, tulichokisema na kukisimamia ni hiki.

"Wananchi wa Songea, huu ni mkutano wangu wa kwanza kuhutubia hadharani tangu nilipokoswa koswa kuuawa kwa bomu, risasi za SMG na risasi za bastola kwenye tukio la Soweto, Arusha siku ya kuhitimisha kampeni.

"Lakini napenda niwaambie kitu kimoja, miye kama kamanda wenu mkuu, sitaingiwa hofu. Sasa tuna usongo zaidi na wametuongeza charge (nguvu) ya kuing'oa CCM katika chaguzi zijazo, maana tunajua tunasimamia haki, ukweli na matumaini ya Watanzania wote," alisema.

Huku akiwatoa machozi baadhi ya waliohudhuria mkutano huo wa juzi, baada ya kuona kitabu kimojawapo chenye picha za watu aliouawa na kuteswa na vijana wa Green Guard ya CCM, Mbowe aliuita ushindi wa kata nne za jijini Arusha kuwa ni wa damu zilizomwagika za wanachama wake.

"Kama kuna mtu alifikiri kuwa kumuua au kutaka kumuua Mbowe atamtia hofu...huyo mtu ameshindwa. Kwa kweli siku ile mimi na wengine tuliokuwa walengwa kabisa wa lile tukio tulinusurika kwa mipango ya Mungu tu. Ni kwa sababu tunaongozwa na Mwenyezi Mungu, tutaendelea kupigania haki hadi kieleweke.

"Huko Serengeti, kwenye Kata ya Machila, watu wetu wake kwa waume wametekwa nyara, wakapelekwa na kufichwa kwenye nyumba ya CCM, wengine wamebakwa, wengine wamewekewa chupa sehemu za siri, kwa sababu tu ya CHADEMA," alisema.

Mbowe alidai kuwa amesikitishwa na upotoshaji mkubwa unaofanywa kwa makusudi na CCM na serikali kwamba chama chake kimeanzisha jeshi, kiasi cha kuvisukuma vyombo vya dola kuanza kuwakamata viongozi wa juu wa chama hicho.

"Hatuwezi wala hatuna mpango wa kuanzisha jeshi kama ambavyo polisi wanataka kupotosha kwa kusoma habari zinazoandikwa na magazeti ya CCM na kutangazwa na TBC. "Nani hajui kuwa CCM wana kikundi kinaitwa Green Guard ambacho kiko nchi nzima, kinapiga
wananchi, kinaumiza wapinzani na ushahidi tunao wa kutosha, kinapewa mafunzo ya kijeshi na ushahidi tunao.

"CHADEMA tumeshalalamika na kulia mara chungu nzima kuwa si sahihi vitendo hivi kuendelezwa, hakuna anayetusikiliza, si polisi wala si serikali. Wote wamekaa kimya. Wakati mwingine vitendo hivi vinafanywa mbele ya usimamizi au macho ya polisi, kila siku wanaoumizwa ni
CHADEMA. Sasa tukasema basi, kuendelea kulialia ni uendawazimu," alisema.

Mbowe alisema walichokiamua ni kufanya ulinzi shirikishi au ulinzi jamii kama ambavyo polisi wamekuwa wakiasa na kusihi kila siku.
"Tulichokisema wala si kitu kipya kabisa. Kimo ndani ya katiba yetu. Naomba mtu yeyote hapa anayeweza kusoma apande hapa juu asomehii katiba ya chama hapa, inazungumzia Red Brigade. Tunachofanya sasa hivi ni kuwapatia vijana ukakamavu.

Hatuanzishi jeshi, wala hatutakuwa na mabomu, wala bunduki, shoka, wala mapanga kama walivyo wenzetu, lakini kama ni mchaka mchaka au karate tutapiga. "Mtu yeyote mwenye nia mbaya na nchi yake hawezi kutangaza hadharani, na sisi kwa kuwa nia yetu ni njema na yenye lengo la kujilinda ndiyo maana tulitangaza mchana kweupe," alisema Mbowe.

Source:
Tanzania daima
 
Asante Lukolo! kwa kutujuza. NAMKUBALI SANA MBOWE. Miaka 22 katika Siasa si Mchezo.
 
Asante Lukolo! kwa kutujuza. NAMKUBALI SANA MBOWE. Miaka 22 katika Siasa si Mchezo.

unajua hawa akina Mbowe wanapaiswa na ccm wenyewe!
ILE KAULI ALIPOITOA TU LILIKUWA GUMZO KWA KILA MTU NA INAFIKIA ATUA CHADEMA WANAFAFANUA MALENGO YAO WAKATI TUMEWAFANYIA MATANGAZO MAKUBWA NA TUNAZIDI KUWAPA SIFA HAWA!
 
ukiona nchi masini duniani usiangalie mazingira yake au rasilimali,angalia aina ya viongozi wake.

Hii ni kweli kabisa. Maana utashangaa nchi kama Botswana ambayo miaka ya tisini tu tulikuwa na umaskini unaolingana, hivi sasa ni ya 129 kwa umaskini huku Tanzania ikiendelea kuwa ya 26, wakati zote zinafahamika kwa uzalishaji mkubwa wa dhahabu baada ya Africa kusini. Sasa hapo utajiuliza Tanzania ina nini? Dhahabu yetu ndiyo inaisha hivyo, na umaskini wetu bado upo kama ulivyokuwa? Tatizo ni kuwa na viongozi ambao ni nusu maiti. Hawana reasoning kabisa. Kila wanachofanya wanatanguliza kwamba maslahi yao.
 
Nimefarijika na kunipa ujasiri mkubwa maneno ya kamanda Mbowe aliyoyatoa songea juu ya uonevu unaofanywa na serikali ya mafisadi.Katika hali ya kawaida hupaswi kumuogopa mtu bali kumheshimu,lakini hata huyo unayemheshimu akikufanyia umafia hauna budi kumdharau na kumbeza kadri yalivyokufanyia huo umafia.Na napenda kusema tu kuwa kumuogopa mtu kisa ana madaraka ni utumwa wa hali ya juu,kinachotakiwa ni kuheshimiana bila kujali itikadi ya mtu,kabila,dini au mahali anapotokea.
Nina kila sababu ya kumpongeza mh Mbowe kwa kauli yake hiyo inatoa ujasiri wa hali ya juu.Na ikumbukwe tu kuwa katiba ya JMT ibara ya 12(2) inasema, " kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake" Pia ibara ya 13(1) inasema,"watu wote ni sawa mbele ya sheria,na wanayo haki,bilaubaguzi wowote,kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria"ibara hiyo hiyo ibara ndogo ya 4 inasema,"ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya mamlaka"
kutokana na ibara mbili hapo juu nidhahiri kuwa ccm na serikali yake wamevunja katiba waliopa kuilinda na kutekeleza.
Kamanda mbowe ongoza jahazi tupo nyuma yako,mbinu chafu za ccm za kuua watu katika mikutano ya chadema ,kuteka watu,na kubambikiza kesi hazitafanikiwa kamwe.CHADEMA ndio tumaini pekee la watz.
 
Naomba ku-declare interest, mimi siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa lakini nina mapenzi na cdm kwa wakati huu. Wakikengeuka nami nageuka.

Kuna watu ukiwasikiliza na/au kusoma maandiko yao unafarijika kwamba tz bado tunao watu wenye upeo na uzalendo na wanaofahamu aina ya tanzania tuitakayo. Katika orodha hiyo ya watu wachache, MBOWE yupo. Mbowe ni kiongozi, akizungumza masikio yanasikia na moyo unapokea. Watu wa aina hii ni wachache, ni mfano wa Mwalimu
 
Naomba ku-declare interest, mimi siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa lakini nina mapenzi na cdm kwa wakati huu. Wakikengeuka nami nageuka.

Kuna watu ukiwasikiliza na/au kusoma maandiko yao unafarijika kwamba tz bado tunao watu wenye upeo na uzalendo na wanaofahamu aina ya tanzania tuitakayo. Katika orodha hiyo ya watu wachache, MBOWE yupo. Mbowe ni kiongozi, akizungumza masikio yanasikia na moyo unapokea. Watu wa aina hii ni wachache, ni mfano wa Mwalimu
[MENTION][JFMP3][/JFMP3][/MENTION]

nikweli mkuu kunawatu wakiongea utatamani waendelee kuongea mda wote, wanajua wanachokiongea mstakabali wa nchi ilipofikia hauhitaji mipasho watu wanata wakwamuliwe kwenye umaskini mzito wengine wanaleta mzaha.
 
Ni bahati mbaya Tanzania hatuna utamaduni wa kutunza kumbukumbu za hotuba za viongozi wetu, kama ungepata kumsikiliza Mh.Mbowe wakati ule alipo gombea Uraisi mwaka 2005, ungejua jinsi alivyo na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo na hoja zenye mashiko. Leo hii ukubwa na umaarufu wa CDM unaweza kuonekana kama umeibuka bila maandalizi, Mbowe ni kiongozi anayepaswa kupewa heshima kati ya viongozi wanaofanya vizuri Africa Mashariki
 
.....can't agree more.....i very much respect Hon. Mbowe for that....my district's MP....
 
Huku karatu tumempa sifa moja 1 kuna uwanja wa mikutano unaitwa "uwanja wa mbowe"hata mtoto mdogo ukimwuliza atakupeleka.
 
Nimesoma kauli ya Mbowe kama ilivyonukuliwa katika gazeti la Tanzania daima, kwa kweli nimefarijika sana. Na nimejiridhisha kwamba Mbowe ni kiongozi wa ukweli. Maneno haya ya Mbowe, hayawezi kusemwa na kiongozi mwingine yeyote anayeheshimika ndani ya CCM. Wakati Mbowe akitoa kauli yenye hekima ya hali ya juu, kule upande mwingine tungeshuhudia mwenyekiti wake akiongea mipasho. "Za kuambiwa....", "Ukitaka kula ukubali kuliwa" etc. Sasa msome Mbowe hapa: Ndipo ujue kuwa uwingi wa degree za darasani si kipimo cha hekima.


"Sitamuogopa rais, lakini nitamheshimu, sitaogopa polisi lakini nitawaheshimu, sitaogopa Jeshi lakini nitaheshimu Jeshi. "Kuanzia sasa sitamheshimu mtu yeyote asiyeheshimu ubinadamu wa mtu mwingine.

Uchaguzi wa juzi wa kata, tumeshinda kwa mapambano ya damu. Watu wetu wamepigwa kila mahali, wamekatwa mapanga na mashoka na vijana wa CCM, Green Guard. "Katika hali kama hiyo siwezi kucheka na polisi, ndiyo maana juzi tumetangaza kuwapatia vijana wetu mafunzo ya ukakamavu ili tujilinde na vitendo hivi. Hatujaanzisha jeshi, tulichokisema na kukisimamia ni hiki.

"Wananchi wa Songea, huu ni mkutano wangu wa kwanza kuhutubia hadharani tangu nilipokoswa koswa kuuawa kwa bomu, risasi za SMG na risasi za bastola kwenye tukio la Soweto, Arusha siku ya kuhitimisha kampeni.

"Lakini napenda niwaambie kitu kimoja, miye kama kamanda wenu mkuu, sitaingiwa hofu. Sasa tuna usongo zaidi na wametuongeza charge (nguvu) ya kuing'oa CCM katika chaguzi zijazo, maana tunajua tunasimamia haki, ukweli na matumaini ya Watanzania wote," alisema.

Huku akiwatoa machozi baadhi ya waliohudhuria mkutano huo wa juzi, baada ya kuona kitabu kimojawapo chenye picha za watu aliouawa na kuteswa na vijana wa Green Guard ya CCM, Mbowe aliuita ushindi wa kata nne za jijini Arusha kuwa ni wa damu zilizomwagika za wanachama wake.

"Kama kuna mtu alifikiri kuwa kumuua au kutaka kumuua Mbowe atamtia hofu...huyo mtu ameshindwa. Kwa kweli siku ile mimi na wengine tuliokuwa walengwa kabisa wa lile tukio tulinusurika kwa mipango ya Mungu tu. Ni kwa sababu tunaongozwa na Mwenyezi Mungu, tutaendelea kupigania haki hadi kieleweke.

"Huko Serengeti, kwenye Kata ya Machila, watu wetu wake kwa waume wametekwa nyara, wakapelekwa na kufichwa kwenye nyumba ya CCM, wengine wamebakwa, wengine wamewekewa chupa sehemu za siri, kwa sababu tu ya CHADEMA," alisema.

Mbowe alidai kuwa amesikitishwa na upotoshaji mkubwa unaofanywa kwa makusudi na CCM na serikali kwamba chama chake kimeanzisha jeshi, kiasi cha kuvisukuma vyombo vya dola kuanza kuwakamata viongozi wa juu wa chama hicho.

"Hatuwezi wala hatuna mpango wa kuanzisha jeshi kama ambavyo polisi wanataka kupotosha kwa kusoma habari zinazoandikwa na magazeti ya CCM na kutangazwa na TBC. "Nani hajui kuwa CCM wana kikundi kinaitwa Green Guard ambacho kiko nchi nzima, kinapiga
wananchi, kinaumiza wapinzani na ushahidi tunao wa kutosha, kinapewa mafunzo ya kijeshi na ushahidi tunao.

"CHADEMA tumeshalalamika na kulia mara chungu nzima kuwa si sahihi vitendo hivi kuendelezwa, hakuna anayetusikiliza, si polisi wala si serikali. Wote wamekaa kimya. Wakati mwingine vitendo hivi vinafanywa mbele ya usimamizi au macho ya polisi, kila siku wanaoumizwa ni
CHADEMA. Sasa tukasema basi, kuendelea kulialia ni uendawazimu," alisema.

Mbowe alisema walichokiamua ni kufanya ulinzi shirikishi au ulinzi jamii kama ambavyo polisi wamekuwa wakiasa na kusihi kila siku.
"Tulichokisema wala si kitu kipya kabisa. Kimo ndani ya katiba yetu. Naomba mtu yeyote hapa anayeweza kusoma apande hapa juu asomehii katiba ya chama hapa, inazungumzia Red Brigade. Tunachofanya sasa hivi ni kuwapatia vijana ukakamavu.

Hatuanzishi jeshi, wala hatutakuwa na mabomu, wala bunduki, shoka, wala mapanga kama walivyo wenzetu, lakini kama ni mchaka mchaka au karate tutapiga. "Mtu yeyote mwenye nia mbaya na nchi yake hawezi kutangaza hadharani, na sisi kwa kuwa nia yetu ni njema na yenye lengo la kujilinda ndiyo maana tulitangaza mchana kweupe," alisema Mbowe.

Source:
Tanzania daima

kumbe ukiwa muuza dawa za kulevya na kuendesha kumbi za muziki na kuuza pombe unakuwa na busara,

Halafu kumbe ukipanga na kusimamia mauaji ya watu unakuwa na busara kweli tanzania daima hakuna waandishi,
 
kama isingekuwa makeneza angalau kidogo lakini makengeza.
 

“Sitamuogopa rais, lakini nitamheshimu, sitaogopa polisi lakini nitawaheshimu, sitaogopa Jeshi lakini nitaheshimu Jeshi. “Kuanzia sasa sitamheshimu mtu yeyote asiyeheshimu ubinadamu wa mtu mwingine.


Source:
Tanzania daima
Haya maneno yamebeba tani kadhaa za dhahabu kwa thamani.
 
Back
Top Bottom