Mbowe akifungwa CHADEMA inakufa?

Mbowe akifungwa CHADEMA inakufa?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,253
Reaction score
16,171
Mbowe yuko maabusu, Lissu na Lema wako uhamishoni.

Je, huu ndio mwisho wa CHADEMA?
 
Chama ni watu, watu hufanya taasisi taasisi huongozwa na mifumo, na mifumo husinamiwa na watu. Sasa umeelewa eehhh ?
Nilikuwa nami najua hivyo, lakini kumbe sivyo bhana, chadema inaonekana kama imeparalyse kabisa, haishiriki kwenye chochote eti kwakuwa mwenyekiti wao Yuko mahabusu na akina Lisu wako uhamishonii. Hawashiriki kwenye chaguzi ndogo Wala kwenye mazungumzo na hayo sio maamuzi ya mkutano mkuu wa chadema bali ni maamuzi ya viongozi wachache wa chadema.

Mh. Lisu kasema harudi mpaka ahakikishiwe kupewa na serikali ma body guards wa kumlinda binafsi, je sharti hili lisipotimizwa na mbowe akifungwa ndiyo chadema imekufa?
 
Nilikuwa nami najua hivyo, lakini kumbe sivyo bhana, chadema inaonekana kama imeparalyse kabisa, haishiriki kwenye chochote eti kwakuwa mwenyekiti wao Yuko mahabusu na akina Lisu wako uhamishonii. Hawashiriki kwenye chaguzi ndogo Wala kwenye mazungumzo na hayo sio maamuzi ya mkutano mkuu wa chadema bali ni maamuzi ya viongozi wachache wa chadema.

Mh. Lisu kasema harudi mpaka ahakikishiwe kupewa na serikali ma body guards wa kumlinda binafsi, je sharti hili lisipotimizwa na mbowe akifungwa ndiyo chadema imekufa?
Tuliza akili huenda ukawaelewa chadema kuliko wengine wote na hata ukawa mwanachama mwaminifu na mzalendo, wasichotaka chadema ni kushiriki chafuzi badala ya uchaguzi, dai la msingi ni katiba mpya ya wananchi ambayo ndani yake inapatikana tume huru ya uchaguzi. Kurudi bila wasiojulikana kujulikana na hatua kuchukuliwa bado inaweza isiwe salama, kwani anayokumbukumbu ya ulemavu aliosababishiwa na ambao hakuna aliyefanya chochote hadharani hata tu kukemea uhalifu ule wa viwango vile, zaidi ya kejeli na kebehi za wazi. Na zaidi kejeli na kebehi zikachagizwa na dhuluma ya haki zake za msingi Kwa visingizio vya wachache sijui kwa utashi wao au kwa maelekezo. wewe unasemaje mwenzetu kama binadamu wa kawaida bila kuzingatua mamlaka au wadhifa ulionao🤔.
 
Nani aliyekuambia kuwa Mbowe ,Lissu na Lema ndio Chadema?

Muwe mnashirikisha vizuri kichwa na ubongo.
Wewe huoni au unataka sifa TU. Chama hakishiriki kwenye chochote Sasa hivi hadi mbowe aachiwe bila mashariti, Sasa hata mnyika ni haramu kishiriki kwenye chochote hadi mwenyekiti atoke bila mashariti, Use and disuse effect. Asiyekuwepo machoni na moyoni hatakuwepo.

Chama ni Imani na Imani inarithiwa na vizazi. Hawa watoto ambao ndo wanaanza kupata akili Sasa hivi hawajui kama Kuna chadema, maana hakionekani mitaani Wala kwenye media. Kimebakia kuwa Chama Cha kwenye yu-tube.

Lisu na Lema kuishi nje ya Nchi kunaua chama, vijana wanakata tamaa, hasa wale ambao hawana uwezo wa kwenda kuishi nje ya Nchi kama Lema na Lisu kama mambo yataharibika nchini. Watasema present is known and secure.
 
Wewe huoni au unataka sifa TU. Chama hakishiriki kwenye chochote Sasa hivi hadi mbowe aachiwe bila mashariti, Sasa hata mnyika ni haramu kishiriki kwenye chochote hadi mwenyekiti atoke bila mashariti, Use and disuse effect. Asiyekuwepo machoni na moyoni hatakuwepo.

Chama ni Imani na Imani inarithiwa na vizazi. Hawa watoto ambao ndo wanaanza kupata akili Sasa hivi hawajui kama Kuna chadema, maana hakionekani mitaani Wala kwenye media. Kimebakia kuwa Chama Cha kwenye yu-tube.

Lisu na Lema kuishi nje ya Nchi kunaua chama, vijana wanakata tamaa, hasa wale ambao hawana uwezo wa kwenda kuishi nje ya Nchi kama Lema na Lisu kama mambo yataharibika nchini. Watasema present is known and secure.
Ila kutaka kuwauwa siyo kuuwa chama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom