Mbowe aiuza CHADEMA kwa Lowassa

katika uchuguzi kuna vyama vinapata hasara wakati wa kampeni ila mwenyekiti wa chadema amenufaika kwa kuuza chama mbowe kwa lowasa.
pamoja na nguvu ya wanachama wa
chama hicho.
sasa biashara imefanyika tunataka
kodi.
rais magufuli kishatoa notis siku
saba kwa wakwepaji kodi kulipa

Peleka ujinga wako huko
 
Na kweli baadaye wakaanzisha bendi ya kuzungusha mikono. Nani mkweli gazeti au waliolipinga?
 
katika uchuguzi kuna vyama vinapata hasara wakati wa kampeni ila mwenyekiti wa chadema amenufaika kwa kuuza chama mbowe kwa lowasa.
pamoja na nguvu ya wanachama wa
chama hicho.
sasa biashara imefanyika tunataka
kodi.
rais magufuli kishatoa notis siku
saba kwa wakwepaji kodi kulipa
Kuna mpango wa Mwenyekiti wa Chadema Mh.Freeman Mbowe wa kulipwa mamilioni ya fedha ili Viongozi wa Chadema waache kumsema Mr. Monduli kuwa ni fisadi.

Mh.Zitto Kabwe anajitahidi kwa kila hali kuzuia mpango huo

===========

Mmoja kati ya vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuhusika na vitendo vya ufisadi(jina tunalihifadhi kwa sasa) anadaiwa kuwa kwenye mazungumzo ya siri na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) Freeman Mbowe ili kuingia ubia na chama hicho.

Inaelezwa kuwa ,lengo la kigogo huyo ni kukiziba mdomo chama hicho kisimrushie makombora ya ufisadi kama walivyowahi kumrushia siku za nyuma.

Uchunguzi uliofanywa na timu ya waandishi wa gazeti hili kwa muda mrefu sasa umebaini kuwa kigogo huyo wa CCM amekuwa na mawasiliano ya siri na ya karibu na Mbowe huku vikao vingi vikifanyika ndani ya hoteli moja ya kitalii iliyopo jijini Arusha (jina tunalo)

Imebainika kuwa ndoa hiyo ya siri ni ya wanasiasa hao wawili,lakini ikilenga uchaguzi mkuu wa 2015 ambapo kigogo huyo wa CCM amemuahidi Mbowe kwamba wataunda "serikali ya umoja wa kitaifa" endapo Mbowe atasaidia kuacha kumuandama kwa tuhuma za ufisadi na kuwadhibiti viongozi wengine wa chama chake, kutofanya hivyo kwenye maandamano na mikutano yao ya hadhara, pamoja na kwenye mahojiano na vyombo vya habari.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa tayari kigogo huyo amempa mwenyekiti huyo wa CHADEMA kiasi kikubwa cha fedha ili chama hicho kinapoendelea na kampeni yake ya bomoa-bomoa mafisadi yeye asiguswe kabisa, kama hatua ya kumfikisha ndoto yake ya kutaka chama tawala kumteua kuwa mgombea wa nafasi ya urais.

Chanzo chetu cha uhakika kikiongea na Sauti Huru kwa sharti la kufichwa jina lake kimedai " huu mpango unafanywa kwa siri kubwa na ninajua hata mhusika (anamtaja) akijua habari hii imetoka atafadhaika sana"


Habari zaidi zinadai kwamba kigogo huyo amefikia hatua hiyo baada ya kusoma alama za nyakati na kuona kwamba uwezekano wa mwenyekiti wa chama chake kumuunga mkono ni mdogo, hivyo hatoweza kupenya katika kinyang'anyiro cha uraisi 2015.

" Huyu bwana amesoma alama za nyakati ,ameona kabisa uwezekano wa kuungwa mkono na mwenyekiti wake(wa CCM) ni mdogo sana hivyo ni lazima atafute njia nyingine hata kama njia hiyo itakuwa na madhara kwa chama chake", kilieleza chanzo hicho na kufafanua;

"Si kwamba hajui mwenyekiti atalalia wapi, anajua lakini yuko tayari hata kukisaliti chama ili wote wakose,hivi ninavyoongea nanyi watu hawa wana mawasiliano ya kila mara juu ya suala hili ila Mbowe kaweka ngumu kuwa lazima waandikishiane ajue kabisa endapo (kigogo huyo atafanikiwa kuingia madarakani basi wataunda government of unity(serikali ya umoja wa kitaifa)".

...Aidha imefafanuliwa kwamba habari hizi zimeweza kumgusa hata Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zitto Kabwe, lakini kwa namna ya pekee Zitto ameweza kudhoofisha mkakati huo kwa kile kilichodaiwa kuwa ni 'unafiki kwa Mbowe'

"Mtakumbuka siku za hivi karibuni Zitto alishutumiwa na chama chake kwa madai ya kuwa na uhusiano wa mashaka na Idara ya Usalama wa Taifa. Chadema wamekuwa wakidai kwamba Zitto anatoa siri za chama chao nje na hata kumuundia kamati ya wazee kumshauri?" alihoji.

Aliendelea:" Kilichotokea katika kamati hiyo siku walipokutana na Zitto ilikuwa tofauti kabisa, Zitto akawabadilishia mada pale alipowaambia wazee,'jamani ugomvi wangu na Mbowe ni pesa za chama, anatumia chama hiki hiki kupata fedha toka nje ya nchi na ndani ya nchi, lakini ninapojaribu kumkosoa kuwa tabia hiyo si nzuri kwa mwenyekiti wa chama ananijia juu,nyie mnajua kuwa amepokea fedha mamilioni kutoka kwa(anamtaja kigogo huyo) kwa ajili ya kutunyamazisha tusipige kelele za ufisadi dhidi yake?' "

"Hivi hamjui tayari anafanya mazungumzo na mtu wa CCM kwa ajili ya power sharing ya mwaka 2015?"

Kwa mujibu wa habari hiyo ni kwamba kigogo huyo atafanya kila liwezekanalo CCM imteue kuwa mgombea wa nafasi ya uraisi; lakini anajua hilo litawezekana endapo kelele za ufisadi dhidi yake zitamalizika.

"Huyu mtu ni mjanja sana na kwa sasa ana nguvu na mtandao mkubwa ndani ya CCM unaoweza kumfanya ateuliwe na chama kuwa mgombea, si hilo tu anajaribu hata kutafuta nguvu nje ya nchi ili endapo akikataliwa aweze kuwa na cha kuieleza jumuiya za kimataifa,"

"Na kwa hatua aliyofikia ni kwamba endapo hatoteuliwa hasa kutokana na ufisadi wake,yuko tayari hata chama chake kipoteze nafasi ya uraisi kitu ambacho kinaonyesha kuwa hana sifa za kiuongozi isipokuwa ni tamaa ya utawala."

Source: Gazeti la Sauti Huru

My Take:
Wale viongozi wa Chadema na wakereketwa waliopo humu JF watuthibitishie hii habari kama ni kweli.
Habari za propaganda, zisizoenda shule, zilizoandikwa na wehu na zinazoaminika na wenye kufanana na walioziandika. Mnajitekenya na kucheka wenyewe. Poleni na aibu kwa CCM - chama cha manyang'au.
 
Habari za propaganda, zisizoenda shule, zilizoandikwa na wehu na zinazoaminika na wenye kufanana na walioziandika. Mnajitekenya na kucheka wenyewe. Poleni na aibu kwa CCM - chama cha manyang'au.
Sasa mkuu hii iliandikwa 2011 na yakatimia 2015 unabisha nini? Hii haikuwa propaganda bali taarifa au progress report. Sisi tulienda kucheki reference tu.
 
Habari za propaganda, zisizoenda shule, zilizoandikwa na wehu na zinazoaminika na wenye kufanana na walioziandika. Mnajitekenya na kucheka wenyewe. Poleni na aibu kwa CCM - chama cha manyang'au.
Usiwe unakurupuka kama unatoka chooni. Habari hii iliandikwa miaka michache iliyopita, na mlengwa kweli kasafishwa na hao waliomchafua na wakampa hadi nafasi ya juu kabisa kwenye chama chao na hadi sasa anategemewa na kuaminika kwa ushauri. Na wote waliomponda ndio waliozungusha mikono kishenzi!
 
Kuna wana chadema wa awali walioupinga Uzi mwaka 2011 sasa hivi kwa aibu wamebadili ID zao.
 
Kwa upande mmoja sitaki kuamini kwamba Mbowe anaweza kukubali kujichimbia kaburi la kisiasa kwa kukubali kupokea vipande thelathini vya shaba. Hata hivyo, nikijua jinsi hawa jamaa walivyo na mbinu na kiu ya kujaribu kununua kila mtu, siondoi uwezekano wa hili kutokea na kwa hili nakubaliana na analysis ya Banyimwa.

Sitaki pia kumuondoa Zitto katika hili kwani ukaribu wa Zitto na hawa mafsadi ni mkubwa kuliko hata ule wa Mbowe na mafisadi. Nakumbuka alivyopigia debe Dowans na baadae Mwanahalisi kumuanika.

Kwa hiyo CDM wachunge hili na kulifuatilia kwa kina lakini vile vile huyu Zitto ni wa kumuangalia zaidi maana ilisemwa humu kwamba much as anaipenda sana CDM, lakini anaipenda sana pesa kuliko CDM.
Nani sasa alikuwa karibu na fisadi....zitto au Mbowe
 
Mbowe= Nick Clegg. lol.

Ukweli ni kwamba mambo kama haya katika siasa yapo haswa katika nchi zetu hizi zakibongo. Ukweli ni kwamba JK will never let Lowassa be president (atatumia CC kukata jina lake, na sababu itakayosemwa ni ile ile iliompoteza Malecela kuwa Mwalimu alikua hamtaki na pia scandal na kujiuzulu kwake kunamfanya asifae).

Kwahiyo kuna logic kubwa hapa. Inawezekana sana hizi zikawa campaign za Zitto kujaribu kumpunguza nguvu Mbowe (kama ni uongo) lakini vile vile inawezekana ikawa kwamba ni mchongo wa CCM kuivunja nguvu CHADEMA (JK and his people might have found that it would be useful to undermine Lowassa through this and at the same time undermine CHADEMA). Lakini kwa kuzingatia jitihada za Lowassa kujisafisha na kujihalalisha kuwa na nafasi ya kiti cha Rais ametoa pesa nyingi kuwezesha wabunge wengi wa CCM na hata wa upinzani kushinda uchaguzi.

Makadirio yasio rasmi kutoka wanasiasa mbali mbali zinasema kuwa ametoa pesa kwa takribani asilimia 75% ya wabunge waliopo Bungeni hivi sasa. Pamoja na kununua viongozi wengine wa CCM, viombo vya usalama ikiwemo TISS na vile vile vyombo vya habari kama tunavyofahamu tayari.

Hii inaonyesha strategy ya huyu bwana ni kucontrol channels zote zinazotumika kuchuja na kuchagua Rais. Bila shaka anawatu wake Central Committee lakini JK anaweza mpoteza aidha kwa kutumia sababu ambazo nimetaja hapo juu haswa kama CHADEMA na vyombo vingine vya kisiasa vikiendelea kumuandama katika miaka hii mitano ijayo. Hivyo kwa kuzingatia tactics it is extremely logical and likely that these allegations are true.

There is a clear motive on Lowassa's part as well as Mbowe ( kama ilivyotokea kwa Clegg, na kama hali ilivyo Kenya kwa mfano). Ukweli ni kwamba hii kitu ni mbaya na inahitaji kuchunguzwa zaidi na kutumia misingi ya kuto kupendelea au kufikiria kwa kutumia hisia za uzalendo wa ki-CHADEMA. In other words, these allegations warrant serious objective investigation and analysis.

Lisemwalo lipo na kama halipo basi linachongwa na 2015 mtaliona.
Mkuu bado upo JF? Hakika una madini ya hatari.....ur truly great thinker
 
Mnajaribu kumpamba Zitto aonekane malaika???? upuuzi mtupu leteni habari za maana watu tujadili, kutuletea habari kama japo mtu anatumia demokrasia, lakini ikumbukwe kuwa ni uharifu wa rasilimali, muda na akili na utayari wa watu katika kushiriki kuchangia mambo.....mtatumia misuli sana kumpamba Zitto bila mafanikio mwenzenu kila kukica anaoga matope kwa hiari yake.

Kuhusu CDM NA mbowe HOJA ZILIZOTUMIKA NI UPUUZI MTUPU WAANDIKISHIANE HALAFU WAKIGEUKIANA WAKSHITAKIANE WAPI LABDA KAMA MNGESEMA WAMEENDA KWA MGANGA KUNCHANJIANA DAMU (KULA YAMINI)
Mkuu bado una mtazamo huu?
 
kwanza sauti huru ndio gazeti gani, lina intelligency service gani kuzidi mwanahalisi na raia mwema mpaka liwe la kwanza kuibua ishue kama hiyo? Hakuna kitu hapo!, hayo ni mambo ya kundi fulani la ccm linalotaka kummaliza mzee wa monduli na chadema
Bado upo JF? Je bado una mtazamo huu huu
 
Habari hii inaweza ya kupikwa lakini imepikwa kwenye mazingira yanayoelekea kuwa kweli:
Tanzania Daima kumpamba ENL
Mbowe yupo kibiashara zaidi
Mbowe hajawahi kumsifia/kumpamba Dr. Slaa hata siku moja (fuatilia), maana yake hapendezewi naye jinsi alivyo moto kwa mafisadi
Mbowe hawajawahi kutoa kauli yoyote ya kumlaani/kumsema ENL au RA

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Truly great thinker
 
Habari hii ina ukweli gani?au kina magamba wanajaribu janja hii kudhohofisha kasi ya watu makini kwenye mapambano.Lakini pia mbona issue ya urais 2015 inaumiza vichwa vya kina magamba wakati tangu wamchague rais hawana hata miaka miwili? wamegundua nini kwa bosi wao?:violin:
Bado una fikra hizi hizi or?
 
Watu walisema toka 2011 wengine wakabisha mwishoe 2015 yakatimia aibu yao aibu yetu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom