Mbinu ya wasanii Bongo kunufaika na kazi zao

Mathias Byabato

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
1,020
691
Huu ni ushauri wa bure kwa wasanii wa mziki,movies kwa Tanzania.

Nimekuwa nikifuatilia kilio cha wasanii hao kwamba wamekuwa hawanufaiki na kazi zao hasa baada ya watu kuzitumia ama bila kuzinunua au kuzinunua kwa gharama ndogo sana tofauti na wao wanavyouuza eti wao wanauza ORIGINAL lakini watumiaji wanatumia TOFAUTI NA ORIGANAL.

Nimetembelea baadhi ya maduka ya kuuza cd,dvd za movies na miziki nimegundua kuwa kinachowaua wasanii ni suala la kutolewa namna ya kufanya biashara.

Mfano Katika mji wa Bukoba CD moja tupu ni sh 500,DVD tupu ya one layer ni sh 100,sasa mtu anakwenda katika duka la CD ananunua CD moja tupu na kuchomewa CD au DVD ya movies 10 kwa tsh 3,000 tu tena wanaofanya hivyo ni wale wale wanaouza zile origanal.

Hivi wasanii wakipunguza gharama za CD/dvd KUTOKA TSH 5000 HADI 1000 AU 1500 hakuna mtu atakayeweza kukopy CD,DVD za wasanii kwani gharama ya kufanya hivyo itakuwa sawa na kupata origanal.

wasanii watasema gharama za kutengeza hizo CD/DVD kuwa ni kubwa lakini watambue kuwa iwapo watafanya hivyo watauza sana kuliko hivi sasa ambapo kwa hapa Bukoba ukitaka DVD yenye Movies 10 au 20 ni tsh 5,000 tu.

Nawasilisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom