Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,621
- 6,511
Kuna watu wanatoa maneno ya kejeli kuhusiana na ukimya uliotawala nchi nzima siku ya leo 09/12/2025.
Watu wasichojua ni gharama kubwa ambazo serikali na vyombo vyake imeingia siku ya leo kuendesha operation yake.
Kuanzia gharama za kusafirisha watu na vifaa, gharama za malazi ambapo maaskari na wapepelezi wengi sana wamesafirishwa na kulazwa katika maguest house na lodges, posho za watu wao wote. Operation ya leo tu imegharimu mabilioni ya pesa.
Sasa chukulia hii operation iendelee kesho, iendelee wiki nzima, iendelee hadi mwisho wa mwaka. Embu waza matrilioni mangapi yatatumika.
Kumbuka hapo hapo mapato ya kodi yanapungua kutokana na kushuka shughuli za biashara, kupungua watalii, nk. Hapo hapo wahisani wanapunguza sapoti yao katika bajeti ya serikali.
Endapo waandamanaji wakiendelea na mipango ya kukutania mijini kama wanavyopanga, mfano Mnazi Mmoja, Kariakoo, Posta, nk. ina maana hata serikali ikiamua kuwekeza nguvu kudhibiti maeneo hayo, bado athari za kiuchumi zitakuwa kubwa sana.
Mapato yakiendelea kupungua ina maana serikali itabidi ianze kuprint pesa kuendesha hizi operation. Kuprint pesa ina maana kutaanza kuwa na mfumuko wa bei. Wachumi wanajua yanayofuata baada ya hapo.
Ninachotaka kusema ni kwamba vita nyingi duniani, za silaha au zile za kidemokrasia zinapiganwa katika uchumi kwanza kabla hata risasi moja haijarushwa.
Watu wasichojua ni gharama kubwa ambazo serikali na vyombo vyake imeingia siku ya leo kuendesha operation yake.
Kuanzia gharama za kusafirisha watu na vifaa, gharama za malazi ambapo maaskari na wapepelezi wengi sana wamesafirishwa na kulazwa katika maguest house na lodges, posho za watu wao wote. Operation ya leo tu imegharimu mabilioni ya pesa.
Sasa chukulia hii operation iendelee kesho, iendelee wiki nzima, iendelee hadi mwisho wa mwaka. Embu waza matrilioni mangapi yatatumika.
Kumbuka hapo hapo mapato ya kodi yanapungua kutokana na kushuka shughuli za biashara, kupungua watalii, nk. Hapo hapo wahisani wanapunguza sapoti yao katika bajeti ya serikali.
Endapo waandamanaji wakiendelea na mipango ya kukutania mijini kama wanavyopanga, mfano Mnazi Mmoja, Kariakoo, Posta, nk. ina maana hata serikali ikiamua kuwekeza nguvu kudhibiti maeneo hayo, bado athari za kiuchumi zitakuwa kubwa sana.
Mapato yakiendelea kupungua ina maana serikali itabidi ianze kuprint pesa kuendesha hizi operation. Kuprint pesa ina maana kutaanza kuwa na mfumuko wa bei. Wachumi wanajua yanayofuata baada ya hapo.
Ninachotaka kusema ni kwamba vita nyingi duniani, za silaha au zile za kidemokrasia zinapiganwa katika uchumi kwanza kabla hata risasi moja haijarushwa.