Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

Tuliyokua tunayashuhudia kule Soweto Africa ya kusini sasa ndio haya hapa Tanzania? kumbe mkoloni sio lazima awe mzungu?
 
naripoti nikitokea tunduma kuelekea mbeya jamaa kaniambia bora ulale huko huko
 
Kutumia Jeshi ni kosa kubwa sana. Wajaribu kukumbuka kwa Mubarak
Ukitumia jeshi umetangaza vita.
 
Yote hayo kwa sababu ya mtu mmoja tu Kandoro kujitia amekuja na mbinu mpya ya kusafisha jiji!
 
Watakuwa wamfeanya kosa kubwa sana kama wameamua kutumia jeshi liwasaidie polis.....huilo kosa alilifanya Mubarak
nakuunga mkono kabsa jeshi kazi yake si kutuliza ghasia ni kuua na kumaliza vita. hata kubembeleza watu huwa hawajui. na ukimuita mjeda aingie mtaani yeye kwake anaweka akilini kuwa anaenda kupanbana na adui kuua kwake iatkuwa jambo la kawaida sana. hivyo si busara kuwaruhusu kuingia mtaani
 
Picha kwa hisani ya member figganigga

BREAKING NUUZ: Polisi wapiga Risasi wananchi Mbeya washindwa tuliza Vurugu.. Sasa zimefika uyole wananchi wanashusha Bendera za CCM




majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo hii akiwa kapigwa kichwani. Hadi sasa kuna majeruhi wanne wa risasi, wawili kichwani, mmoja kwenye paja na mwingine mkononi

Mmoja wa majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo, Abel Mwalukali akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa risasi kwenye mkono.
 

Polisi wakijaribu Kuzuia Ghasia katika eneo hilo na kufukuza Wamachinga

Baadhi ya wananchi wakiwa wameokoka katika eneo hilo

Wamachinga Mbali mbali wakikimbia katika eneo la tukio wakati wa machafuko hayo yamepamba moto


Watu Mbali Mbali wakiwa wanakimbia ili kujiokoa na Hatari katika eneo hilo

Picha zote na Mpiga picha wetu maalum​


Aminiania Figaniga mia.
 
Noambeni rasmi mtu anayefahamiana na JK amuombe anipe majukumu ya kuwa mshauri wake wa kisiasa! Ninaamini nina hekima kuliko waliopo kwa kweli.

Unless......
Juzi nilianzsiha thread ya JK'S options wakaifuta,maybe kuna ambao mungempa ushauri.Waliifuta tu ki dictator bila hata kuniambia why the did it.Nina amini kabisa kuwa kuna mods ambao hawana hekima,just kama viongozi wetu na washauri wao...Kufanya mambo kwa kukurupuka.
 
Hivi inakuaje hayo mabomu ya machozi hao askari hayawaathiri!!!!
 
Kuna siku hayo manguo ya polisi yatawaka moto na kuvua taabu.
 
Back
Top Bottom