Mbeya: Wahamiaji haramu 16 kutoka Ethiopia wakamatwa kwa kuingia Nchini bila kibali

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia wahamiaji haramu 16 raia wa nchini Ethiopia, wote wanaume, umri kati ya miaka 18 - 53 kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Watuhumiwa walikamatwa Novemba 09, 2023 majira ya 2:00 asubuhi huko kijiji cha Kasumulu, Wilaya ya Kyela, wakati Askari wa Kikosi maalum cha kuzuia na kupambana na uhalifu cha Jeshi la Polisi kikiwa doria.

Watuhumiwa walikuwa wanasafirishwa kwa kutumia gari lenye namba za usajili T.392 DCP aina ya Toyota Ipsum ambayo mmiliki wake anatafutwa. Dereva wa gari hilo anatafutwa kwani amekimbia na kutelekeza gari mara baada ya kuwaona askari wakilifuatilia gari hilo. Watuhumiwa walikuwa na lengo la kuvuka kupitia vivuko visivyo rasmi kwenda Afrika Kusini kupitia nchini malawi.

Vile vile katika muendelezo wa misako Novemba 11, 2023 majira ya saa 7:20 usiku huko katika Kijiji cha Kyimo, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa mbeya, Jeshi la Polisi liliwakamata watuhumiwa watatu ambao ni 1. ASAYA ASAJILE [32] Mkazi wa Kyimo, 2. FRANK GOOLUCK [21] Mkazi wa Mpemba na 3. WATSON SIMON [28] Mkazi wa Tunduma wakiwa na vifaa mbalimbali vya kuvunjia majengo kwa lengo la kufanya uhalifu.

Baada ya kukamatwa walifanyiwa upekuzi kwenye nyumba waliyokuwa wanaishi na kukutwa wakiwa na TV moja inchi 32 aina ya Hometech, Godoro moja 5x6, Mtungi mdogo wa Gas, Radio 3 aina ya Subwoofer, Bag 2 ndogo za mgongoni, viatu pea 6 na nguo mbalimbali ambavyo ni mali za wizi.
 
Inaelekea Askari Mbeya wako makini. Wakimbizi wametokea Kaskazini, kote hawakukamatwa (pengine waliachiwa), ila hapo ndio washikwe?

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia wahamiaji haramu 16 raia wa nchini Ethiopia, wote wanaume, umri kati ya miaka 18 - 53 kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Watuhumiwa walikamatwa Novemba 09, 2023 majira ya 2:00 asubuhi huko kijiji cha Kasumulu, Wilaya ya Kyela, wakati Askari wa Kikosi maalum cha kuzuia na kupambana na uhalifu cha Jeshi la Polisi kikiwa doria.

Watuhumiwa walikuwa wanasafirishwa kwa kutumia gari lenye namba za usajili T.392 DCP aina ya Toyota Ipsum ambayo mmiliki wake anatafutwa. Dereva wa gari hilo anatafutwa kwani amekimbia na kutelekeza gari mara baada ya kuwaona askari wakilifuatilia gari hilo. Watuhumiwa walikuwa na lengo la kuvuka kupitia vivuko visivyo rasmi kwenda Afrika Kusini kupitia nchini malawi.

Vile vile katika muendelezo wa misako Novemba 11, 2023 majira ya saa 7:20 usiku huko katika Kijiji cha Kyimo, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa mbeya, Jeshi la Polisi liliwakamata watuhumiwa watatu ambao ni 1. ASAYA ASAJILE [32] Mkazi wa Kyimo, 2. FRANK GOOLUCK [21] Mkazi wa Mpemba na 3. WATSON SIMON [28] Mkazi wa Tunduma wakiwa na vifaa mbalimbali vya kuvunjia majengo kwa lengo la kufanya uhalifu.

Baada ya kukamatwa walifanyiwa upekuzi kwenye nyumba waliyokuwa wanaishi na kukutwa wakiwa na TV moja inchi 32 aina ya Hometech, Godoro moja 5x6, Mtungi mdogo wa Gas, Radio 3 aina ya Subwoofer, Bag 2 ndogo za mgongoni, viatu pea 6 na nguo mbalimbali ambavyo ni mali za wizi.
...Wanaoitwa Wahamiaji Haramu waachiwe waendelee na Safari Yao ya Kutafuta Maisha.
Hawatuhusu, ni Wapita Njia TU !!

Ina maana Hata Barabara zetu haturuhusu zitumiwe na Wapita Njia ?? Tanganyika na Ethiopia, Wote ni WAAFRIKA, waachiwe wakahangaike mbele. Afrika KUsini wanakotaka kwenda, ndio watawakamata Kwa kukosa Vibali vinavyotakiwa Kwa Kutaka kuishi kiharamu Nchini humo !
Sio sisi Tanzania ambayo walikuwa wanapita TU !!
Sana Sana 'tucheze' na Dereva wetu aliyepabdisha Watu 16 kwenye Ipsum ..!!
 
Back
Top Bottom