It is Sur_Plus
Senior Member
- Sep 28, 2010
- 167
- 7
Habari zenu wanajamvi wa Jf. Kiukweri Mbeya ni mji ambao una wajasiliamali wengi sana. Hawa wajasiliamali ni vijana ambao wameweza kufanikiwa katika umri mdogo na kuweza kumiliki mitaji mikubwa hasa katika maeneo ya Tunduma, mbeya mjini, kyela na sehemu nyingine za mkoa huo. But kuna jambo kubwa ambalo limekua likinitatiza hasa katika ukweli wake. Kumekua na imani kwamba wafanya biashara wengi wamekua wakishukiwa kwenda Tunduma na Malawi kwa waganga kutafuta utajili unaoitwa huku "UTAJIRI WA MANYOKA". Ambapo inasemekana huko huchukuliwa ulezi au mahindi kisha humwagwa chini ili kuku ale. Inasemekana kwamba idadi ya mahindi au ulezi ambao kuku atakula ndio urefu wa maisha mtu atakayoishi mfano kukuakila punje 5 za mahindi basi utaishi katika maisha ya utajili kwa miaka 5 kisha unakufa. Habari hizi zimekua zikisikika hasa wakati wa misiba pindi wafanyabiashara wengi wanapofariki. "JE, Tuta uona ufalme wa kesho?