Mbeya hawajui kabisa nyama choma

Mbeya hawajui kabisa nyama choma

Yaani wewe Wa Dar unataka uje kwetu utufundishe kupika urojo wenu wa Dar tungependelea urojo wenu tusingeitwa abanyambala.
Onyo:usirudie kuleta umbeya wako hapa tutakufanya kama tuluvyomfanya DC wako Kule kyela,ukitaka kula kula kama huwezi beba urojo wako toka Dar.
 
Nyama choma tunawaachia nyie wa Dar na DAB wenu Tippu Tip Jr......Mbeya ni mwendo wa kisyesye,kifuge,dona,maziwa,maparachichi,miduhu,mbalaga na makande.
Ndiyo maana wanatabia mbovu kama za DAB wao,wala urojo wote hao.
 
Katika biashara zangu huwa nafika mikoani.
Mkoa mmoja nafika natembelea ni Mbeya.
Kwa mara tofauti nikaulizia sehemu ya nyama/kuku choma nikaambiwa Carnival (karibu na Mafiati,Mwanjelwa) na Mbeya Pazuri, Sae kuelekea Uyole.

Nilikuwa Mbeya Pazuri wiki iliyopita.

Sehemu zote hizi kuku choma nilizoagiza ni mbaya, mbaya, mbaya mno.
Kuku hajapakwa viungo wala vilainishi nyama na ana shombo.

Nyama inatiwa kwenye mafuta yaliyo chemshwa na kutolewa hivyo hivyo.
Nyama ngumu kama manati.

Mbeya mkoje lakini?
Chakula kinatoka huko kuja Dar lakini hamjui kupika.
Wadau huko tupeni sehemu nzuri kwa vitafunwa na moja baridi.
Nilikula nyama choma Mbeya pazuri mbichi kabisa nikaomba warudishe motoni wakagoma nikatulia walivojipindua nikalakona sikulipa.
 
sijui vipi ila mimi nilipelekwa sehemu kama mbili zote fantastic misosi yake moja nakumbuka kama 501point or something nyinngine sihyi city nini sikumbuki kwa kweli ila misosi ya choma choma mbuzi kuku ngombe ilo sawa sana
Hapo hyo 501 soul pale uhindini pale ni matata sana uwaga napamiss sana
 
mkuu habari,
mbeya wachomaji nyama ni wachache,
kuna jamaa anaitwa 501 soul food, wapo mjini uhindini karibia na bhojan duka madawa..
hawa huwa wanahost nyama choma pia once a week,kila jumamosi ya mwisho wa mwezi...
Embu asome hapa pale nimepamiss sana ngoja nijichange niende
 
Wapiishi tumejaa tele ila tunawapikia waume zetu na familia zetu zaga za aina zote hadi vibibi na mikate ya kiajemi inapikwa so sio wote hatujui kupika mbeya
 
Kila jamii ina mapishi yake, ni sawa kumlaumu mtu wa Kanda maalumu kwa kushindwa kupika kisamvu cha nazi au umlaumu mkwere kushindwa kupika kisamvu cha karanga. Nadhani ni tamaduni tu za jamii

Sent from my SM-G925F using JamiiForums mobile app
 
Mshazoea broiler mtawezea wap organic?
Alichoandika mleta mada ni ukweli mtupu

Mimi mwenyewe nilishaenda hapo Mbeya pazuri mara kadhaa, wanapika hovyo hovyo Sanaa

Hata supu wanayouza asubuhi ni ya hovyo

Tatizo sio broiler au Organic, maandalizi mabovu mno
 
me nadhani suala la nyama choma wangeachiwa watu wa mikoa ya kaskazini na kanda ya ziwa.
Kaskazini pia kunazidiana

Mimi nikienda Arusha naenda kula nyama kwa Mmasai mmoja anachoma maeneo ya pale mianzini kwny Bar moja hivi

Sijawahi kula nyama nzuri laini kama ya pale
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom