middo lulyheart
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 260
- 98
Wanaume wa kinondoni bhna....
Yani umekutana na kuku orijino unasingizia hawana viungo sema huna meno umezoea broila ndugu kuku wa mbeya huna haja ya kurembea na make up ili upate radha
Yani umekutana na kuku orijino unasingizia hawana viungo sema huna meno umezoea broila ndugu kuku wa mbeya huna haja ya kurembea na make up ili upate radha
Katika biashara zangu huwa nafika mikoani.
Mkoa mmoja nafika natembelea ni Mbeya.
Kwa mara tofauti nikaulizia sehemu ya nyama/kuku choma nikaambiwa Carnival (karibu na Mafiati,Mwanjelwa) na Mbeya Pazuri, Sae kuelekea Uyole.
Nilikuwa Mbeya Pazuri wiki iliyopita.
Sehemu zote hizi kuku choma nilizoagiza ni mbaya, mbaya, mbaya mno.
Kuku hajapakwa viungo wala vilainishi nyama na ana shombo.
Nyama inatiwa kwenye mafuta yaliyo chemshwa na kutolewa hivyo hivyo.
Nyama ngumu kama manati.
Mbeya mkoje lakini?
Chakula kinatoka huko kuja Dar lakini hamjui kupika.
Wadau huko tupeni sehemu nzuri kwa vitafunwa na moja baridi.
