Mbeya hawajui kabisa nyama choma

Mbeya hawajui kabisa nyama choma

ndo maana watu ni wa nguvu kumbe mpaka kula ni nguvu
Katika biashara zangu huwa nafika mikoani.
Mkoa mmoja nafika natembelea ni Mbeya.
Kwa mara tofauti nikaulizia sehemu ya nyama/kuku choma nikaambiwa Carnival (karibu na Mafiati,Mwanjelwa) na Mbeya Pazuri, Sae kuelekea Uyole.

Nilikuwa Mbeya Pazuri wiki iliyopita.

Sehemu zote hizi kuku choma nilizoagiza ni mbaya, mbaya, mbaya mno.
Kuku hajapakwa viungo wala vilainishi nyama na ana shombo.

Nyama inatiwa kwenye mafuta yaliyo chemshwa na kutolewa hivyo hivyo.
Nyama ngumu kama manati.

Mbeya mkoje lakini?
Chakula kinatoka huko kuja Dar lakini hamjui kupika.
Wadau huko tupeni sehemu nzuri kwa vitafunwa na moja baridi.
 
Kabla ya kula uwe unauliza sehemu kali za misosi. Tatzo manataka vyakula vya Daslam ndio siku zote mikoani kuna wanaume Orijino sio wale ya Daresalaam
 
Kama umezoea misosi ya daslamu huwezi kuridhika na misos inayopikwa mikoa mingi ya Tz kama iringa mbeya, rukwa dodoma nk
 
Fursa hiyo wachaga changamkieni.Mikoa ambayo watu SI wafugaji Kama mbeya nyama choma kweli hawajui.Hata ukienda kagera,Lindi,mtwara, ruvuma, nk Tatizo ni Hilo hilo
Mkuu hapo Ruvuma umenigusa. Pale kuna sehemu mbili, Napenda Mtini na La Chaz, wanachoma vizuri sana. Kuna wamangi pale nafikiri.
 
Habari bila picha/video clip sawa na taka taka tu
 
me nadhani suala la nyama choma wangeachiwa watu wa mikoa ya kaskazini na kanda ya ziwa.
Kanda ya ziwa sifuri kwenye mapishi kwa ujumla .Choma pekee wanajua kuchoma Ni samaki nyama ya aina yoyote uchomaji sifuri .Ila Mwanza Kuna watu wa Mara na wachaga sehemu.chache wanajitahidi sehemu hizo walipo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom