Katika biashara zangu huwa nafika mikoani.
Mkoa mmoja nafika natembelea ni Mbeya.
Kwa mara tofauti nikaulizia sehemu ya nyama/kuku choma nikaambiwa Carnival (karibu na Mafiati,Mwanjelwa) na Mbeya Pazuri, Sae kuelekea Uyole.
Nilikuwa Mbeya Pazuri wiki iliyopita.
Sehemu zote hizi kuku choma nilizoagiza ni mbaya, mbaya, mbaya mno.
Kuku hajapakwa viungo wala vilainishi nyama na ana shombo.
Nyama inatiwa kwenye mafuta yaliyo chemshwa na kutolewa hivyo hivyo.
Nyama ngumu kama manati.
Mbeya mkoje lakini?
Chakula kinatoka huko kuja Dar lakini hamjui kupika.
Wadau huko tupeni sehemu nzuri kwa vitafunwa na moja baridi.
Sasa mtu umetoka safari Zambia, Malawi na uko kahoteli single star, unatamani kula nyama choma.Sasa si ungechoma mwenyewe chumbani kwako kuliko kutoa watu kasoro
Mkuu kula manati si uanaume!Kabla ya kula uwe unauliza sehemu kali za misosi. Tatzo manataka vyakula vya Daslam ndio siku zote mikoani kuna wanaume Orijino sio wale ya Daresalaam
Warombo mnasikia?Karibu mbeya
Jiji zuri na chakula kibao .
Uliza wenyeji .
Ukiona hawajuie njoo uchome wewe sisi by nature sio wafugaji ni wakulima.
Changamkia fursa kama una ujuzi
Mkuu hapo Ruvuma umenigusa. Pale kuna sehemu mbili, Napenda Mtini na La Chaz, wanachoma vizuri sana. Kuna wamangi pale nafikiri.Fursa hiyo wachaga changamkieni.Mikoa ambayo watu SI wafugaji Kama mbeya nyama choma kweli hawajui.Hata ukienda kagera,Lindi,mtwara, ruvuma, nk Tatizo ni Hilo hilo
Iringa, Rukwa?Kama umezoea misosi ya daslamu huwezi kuridhika na misos inayopikwa mikoa mingi ya Tz kama iringa mbeya, rukwa dodoma nk
Hamna cha Soweto Wala Nini nyama choma wako sifuri anakupotezea muda tu huyo.Kwenye nyama choma mbeya mjini Ni janga la kitaifa wako sifuriMkuu Soweto iko sehemu gani Mbeya mjini.
Taja bar tu, nikirudi huko nitapatafuta.
Kanda ya ziwa sifuri kwenye mapishi kwa ujumla .Choma pekee wanajua kuchoma Ni samaki nyama ya aina yoyote uchomaji sifuri .Ila Mwanza Kuna watu wa Mara na wachaga sehemu.chache wanajitahidi sehemu hizo walipome nadhani suala la nyama choma wangeachiwa watu wa mikoa ya kaskazini na kanda ya ziwa.